Sunday, December 28, 2014

VPL: Matokeo ya Yanga vs Azam FC haya hapa.

Siku moja baada ya Kagera Sugar kuishushia kipigo Simba katika uwanja wa taifa, ligi kuu ya Tanzania bara maarufu kama Vodacom Premier League imeendelea tena jioni hii kwa mchezo kati ya Yanga SC vs Azam FC.

Katika mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa taifa, Azam ilikuwa ya kwanza kupata bao lililofunga na Didier Kavumbagu dakika 6, Yanga walisawazisha kupitia Amiss Tambwe (7) na kupata la pili lililofungwa na Simon Msuva (57), kabla ya John Bocco aliyeingia akitoa benchi alisawazisha Azam dakika 65.

Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi 14, sawa na Azam, wakati Mtibwa Sugar imebaki kileleni ikiwa na pointi 16, baada ya kulazimishwa sare 1-1 na Stand United jana asubuhi mchezo huo juzi ilivunjwa kutokana na mvua kubwa kunyesha.

Mbeya City imejiondoa mkiani baada ya kuichapa Ndanda FC 1-0, wakati Polisi Morogoro imeinyuka Mgambo JKT kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri.

Morogoro: Polisi Morogoro wameutumia vizuri uwanja wake wa nyumbani kwa kuichapa Mgambo JKT kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Polisi ilipata bao kwanza dakika 22, lililofungwa na Nicolaus Kabipe kabla ya Iman Mapunda kupachika bao la pili kwa kichwa dakika 85, akiunganisha kona ya Kabipe.

Mbeya: Deus Kaseke aliwainua mashabiki wa Mbeya City dakika pili kwa kufunga bao pekee akiunganisha kwa shuti lililomshinda kipa wa Ndanda FC, Salehe Marande na kujaa wavuni.

MTOTO ASOMBWA NA MAJI NA KUFARIKI.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Saturday, December 27, 2014

Naibu Waziri Mhe. January Makamba azindua Kundi la Kaone Sanaa Group Dar Live.

  Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia .Mhe. January Makamba amezindua Kundi la Kaone Sanaa Group Dar Live usiku huu, hapa akiwa katika picha ya pamoja baada ya uzinduzi huo.

Wasanii wa Kaole wakiwa stejini

...akiongea na wanahabari mara baada ya kuwasili Dar Live

...akiwa katika picha ya pamoja na Kaone

...akiongozwa na Meneja Mkuu wa Dar Live, Abdallah Mrisho kwenda meza kuu

...akiwa meza kuu na viongozi wa Kaone

....msanii Msaga Sumu akifanya vitu vyake jukwaani.

BREAKING NEWS: Mtu mmoja afariki dunia baada ya kulipuliwa na bomu aliotaka kuwarushia askari polisi.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

MTOTO ASOMBWA NA MAJI NA KUFARIKI.

MTOTO wa miaka sita, Bernard Benjamin ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Nyamunge, wilayani Ilemela jijini Mwanza, amesombwa na mafuriko na mwili wake kukaa siku kumi na tano bila kuharibika.

Mafuriko yaliyosababisha kifo cha marehemu mtoto Bernard Benjamin.

Tukio hilo lilijiri Desemba 2, mwaka huu kwenye Mto Kenge jijini hapa, maeneo ya Mabatini, Wilaya ya Nyamagana baada ya kujaa maji ambapo marehemu alisombwa na mafuriko hadi pembezoni mwa Ziwa Victoria.

Baba mzazi wa marehemu Bernard, Benjamin David alisema siku ya tukio yeye alikuwa safari na mama wa mtoto alikuwa kazini, watoto walibaki na msichana wa kazi nyumbani.

Baba wa marehemu Bernard Benjamin akihuzunika.

“Ilikuwa Jumanne asubuhi, mvua kubwa sana ilinyesha kwa saa moja na nusu hivi na kusababisha mafuriko. Watoto wangu wote walikuwa nyumbani, lakini mvua ilipokatika walitoka nje na kuanza kucheza.

“Marehemu alikuwa anaondoka bila kuaga kama mara tatu na kila alipofuatwa alikutwa akicheza pembezoni mwa mto huo ambao  umepita jirani na nyumba yangu.“Katika hali ya kushangaza mara ya tatu wenzake walimfuata na kuanza kurudi naye wakati huo marehemu alikuwa yupo nyuma ndipo aliteleza na kutumbukia kwenye maji ya mto.

Mwili wa marehemu Bernard Benjamin ukiwekwa kaburini.

“Alipiga kelele na wenzake walivyosikia sauti nao walipiga mayowe, mmoja wao alijitosa kwenye maji ili amuokoe lakini kasi ya maji ilimshinda na kujikuta akijiokoa mwenyewe kwa kushika mti, watu wakamuwahi na kumuokoa.

“Tuliutafuta mwili tangu siku hiyo hadi Jumatano ya Desemba 17. Saa 10 jioni mke wangu alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni muumini wa kanisa kwetu, akasema kuna mwili wa mtoto umekutwa ufukweni mwa Ziwa Victoria eneo la Miti Mirefu.

Mama mzazi wa marehemu Bernard Benjamin akiweka mchanga kaburini.

“Nilikwenda na kukuta polisi wameshafika. Nilipouona mwili niliutambua kuwa ni wa mwanangu akiwa ameshafariki dunia lakini haukuwa umeharibika.“Bado alikuwa na nguo alizovaa siku ya tukio, viungo vyake vyote vilikuwa salama ila mwili ulikuwa mweupe sana kutokana na kukaa muda mrefu kwenye maji.

Mtoto Bernard Benjamin enzi za uhai wake.

“Tuliupeleka mwili Hospitali ya Rufaa ya Bugando, madaktari walimfanyia uchungzi na kusema mwili haukuharibika kutokana na kufukiwa na mchanga mwingi kwenye maji, nilimshukuru Mungu kwa hilo,” alisema baba wa marehemu.Mazishi ya mtoto huyo yalifanyika Alhamisi ya Desemba 18, mwaka huu katika Makaburi ya Nyakato Sokoni jijini Mwanza.

BREAKING NEWS: Mtu mmoja afariki dunia baada ya kulipuliwa na bomu aliotaka kuwarushia askari polisi.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Friday, December 26, 2014

BREAKING NEWS: Mtu mmoja afariki dunia baada ya kulipuliwa na bomu aliotaka kuwarushia askari polisi.

Mtu mmoja ambaye hajatambulika jina lake na anakotoka amefariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu huku utumbo wake ukiwa nje na mkono wake kukatika alilotaka kuwarushia askari polisi waliokuwa doria usiku wa kuamkia leo na kujeruhi askari polisi wawili ambao hali zao zinaendelea vizuri.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu ameiambia ITV kwa njia ya simu kuwa watu wa nne waliokuwa na mtu huyo wamekimbia huku polisi wakikamata simu za watu hao pamoja na ya marehemu huyo na kwamba hili ni tukio la tatu la mabomu dhidi ya askari Polisi na amasema kukamatwa kwa simu hizo ni mwanzo mzuri wa kuwabaini walipuaji mabomu kwa askari polisi mjini Songea.

Mkuu huyo amesema kuwa kutokana na uzito wa tukio hilo mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini CP Isaya Mungulu anafanya safari kuja Songea leo na atazungumza na vyombo vya habari.

Mwandishi wa habari hii aliyekuwepo eneo la tukio aliweza kushuhudia mabaki ya bomu hilo pamoja na mzula wa kuziba sura aliokuwa akiutumia mtu huyo.

PATCHO MWAMBA AKANUSHA KUFUMANIWA NA KUPIGWA.

UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

BALAA LA KRISMASI MREMBO APOTEZA FAHAMU BAADA YA KUZIDISHA MAMBOZIIIIIIIIIII.

Mwanamke(Jenipher ) ayeanayedaiwa kujiuza akiwa hoi hajitambui.

MSICHANA mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Jenipher, anayedaiwa kujiuza katika maeneo ya Shivaz na Kaloleni jijini hapa, amekutwa akiwa amepoteza fahamu kando ya barabara, katika harakati za kujipatia chochote kipindi hiki cha sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.

Akiwa pembeni ya barabara, Jenipher anayeelezwa kuwa maarufu mjini hapa, anadaiwa kuwa siku hiyo alizidisha idadi ya wanaume aliotoka nao, kwa ajili ya kujipatia kipato cha kutosha ili aweze kuburudika vizuri wakati wa sikukuu ya Krismasi.

Baadhi ya mashuhuda wanaomfahamu msichana huyo walisema kwamba katika kipindi cha wiki nzima iliyopita, alikuwa akisaka wanaume kwa bidii na kwamba alikuwa tayari kwa ajili ya kutoa huduma hiyo mahali popote.

“Unajua hapa kila mtu na mambo yake, huyu Jenipher siku zote tupo naye ila wao huwa hawaendi kulipia gesti, ila wanafanya ngono popote hata mtaroni, kwenye ukuta ilimradi huyo mwanaume yupo tayari, ila usiku alizidiwa na wanaume na hakuwa amekula,’’ alisema mmoja wa dada poa aliyekataa kutaja jina lake.

Mmoja wa wamiliki wa baa iliyo maeneo hayo, aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema wasichana wengi wanaojihusisha na biashara hiyo wamekuwa na tamaa kiasi cha kushindwa kujali afya zao, kwani baadhi yao huacha hata kula chakula, badala yake, hunywa pombe aina ya viroba.
Hadi paparazi inaondoka eneo hilo, bado binti huyo alikuwa yupo eneo hilo akiwa hajitambui.

PATCHO MWAMBA AKANUSHA KUFUMANIWA NA KUPIGWA.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

PATCHO MWAMBA AKANUSHA KUFUMANIWA NA KUPIGWA.


Picha ya Patcho iliyozua utata mitandaoni.

Patcho Mwamba akiwa katika ofisi za Global Publishers Ltd leo.

Patcho akipozi na mwandishi Nyemo Chilongani wa Global.

MWIGIZAJI na mwanamuziki wa Bendi ya FM Academia, Patcho Mwamba hivi punde ameibuka katika ofisi za mtandao huu na kukanusha vikali taarifa zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kuwa amefumaniwa akiwa na mke wa mtu na kupokea kipigo.

Akiongea na mtandao huu, Patcho amesema picha iiliyozagaa mitandaoni aliipost mwenyewe juzi baada ya kupata aleji ya macho ambapo baadaye ilisambaa mitandaoni ikidaiwa kuwa kapigwa baada ya fumanizi.

"Unajua nina aleji na pombe pamoja na vumbi, nikitumia tu pombe lazima macho yangu yavimbe
juzi nilikunywa Windhoek mbili na usiku hali yangu ikabadilika na macho kuvimba, baada ya tukio hilo niliamua kujipiga picha na kuipost katika mtandao wa Instagram na hapo ndipo balaa likazuka" Alisema Patcho akiwa katika ofisi za mtandao huu zilizopo Mwenge-Bamaga, Dar.

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA, DIWANI CCM ANUSURIKA KIPIGO.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Monday, December 22, 2014

ALICHO POST ZITTO KABWE, BAADA YA RAIS KUMWAJIBISHA WAZIRI ANNA TIBAIJUKA NA KUBAKIZA KIPORO.

Nimemsikiliza Mhe Rais. Ninachoweza kusema ni kwamba maazimio yale hayakuwa ya Zitto Kabwe, PAC, CAG au PCCB. Yalikuwa ni maamuzi ya Bunge zima. Bunge la vyama vyote kikiwamo chama cha Rais Kikwete yaani CCM. Sisi kama Bunge tulitoa maazimio yale kwa maridhiano, uzalendo na bila kutaka kumuonea mtu yeyote. Suala hili sasa naliacha kwa wananchi. Bunge limefanya kazi yake na Serikali ambayo ndiyo tulikuwa tunasubiri maamuzi yake imeamua hivyo. Wananchi wataamua wenyewe.

MDAHALO WA KATIBA WAFANYIKA LEO MWANZA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

HAWA Ndo MAPROF BWANA!!!! PROF. TIBAIJUKA AOMBWA KUPISHA NAFASI, PROF MUHONGO AWEKWA KIPORO.

 Rais Dk. Jakaya Kikwete.

--Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo tumemuweka kiporo, kuna uchunguzi nimeagiza ufanywe na nikipata majibu nitafanya uamuzi, tume ya maadili pia wanafanya kwa ajili ya kupata maamuzi kwa misingi ya haki.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Tibaijuka.

--Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Tibaijuka, tumekaa nae na kuzungumza. Pesa hizi ni za nini na kwa ajili gani na amesema ni za shule, mengi yameelezwa. Maswali makubwa kwa nini hazijaenda shuleni moja kwa moja na zikawa kwa jina lake, akasema ndo masharti ya mtoaji, tumelitafakari sana na tumeona msingi mkubwa wa kimaadili kuhusu kupokea hizi pesa, tumeshazungumza nae na tumemwambia atupe nafasi tumteue mwingine.

--Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Fredreck Werema ameshajiuzulu na amesema amebeba dhamana hiyo pia kwa niaba ya waliojiuzulu.

--Kuhusu watu kuwawajibisha, bodi ya TANESCO bahati nzuri imemaliza muda wake na tumeanza mchakato wa bodi, na tutaipata siku chache zijazo. Katibu mkuu wa wizara ni mtumishi wa umma, hivyo kuna taratibu na nimeshaagiza zianze.

----Serikali iandae muswada wa sheria ulioleta TAKUKURU, ni wazo zuri, Mchakato wa kufanya mageuzi TAKUKURU tumeuanza tangu 2008. Sheria ya kwanza ya PCCB ilikua na makosa manne tu ya rushwa tukayaongeza mpaka 24.

--Kuhusu mabenki kuwekwa kama zinatakatisha fedha, pendekezo uchunguzi ufanyike ni pendekezo zuri na intelligence unit ndio watakaofatilia

--Rais aunde tume ya kijaji kuwachunguza majaji(Mujulizi na Luangisa), nimelipokea lakini utaratibu wa kisheria kushughulikia linatakiwa lianzie kwenye mahakama na sio linaanzia kwa rais au bunge. Mahakama inaporidhika amepoteza sifa, inaletwa kwa rais maana ndie anaeteua majaji. Lazima kushirikiana na muhumili wenyewe. Nilichosema tumwachie jaji mkuu na wakiridhika watakuja kwa raisi endapo wataridhika wahusika wamekosa sifa.

--Kamati za bunge kuwavua nyadhifa wenyeviti wa kamati za bunge tunaliachia bunge lenyewe

--TAKUKURU na jeshi la usalama vichukue hatua, nimeshaeleza hatua zinaendelea.

--Kuhusu uwazi wa mikataba na mapitio, tutafanya na lipo moja tutafanya kuhusu usiri wao wa biashara, kuweka wazi zinaweza kutumiwa na wapinzani wa kibiashara, hivyo tutaangalia namna ya kulifanya.

--Niwahakikishie mimi na wenzangu serikalini hatuna upungufu wa dhamira katika kutimiza maazimio ya bunge.
Kutaifisha mitambo ya IPTL, tunahimiza sekta binafsi kuwekeza, tunapotaifisha habari tunayopeleka si nzuri, sisi tuliotaifisha mwanzo siku hizi tunasema hatuna sera ya ujamaa hivyo waje kuwekeza. Watasema wale jamaa wamerudia tena wanataifisha. Mahakama imefanya maamuzi kwa IPTL, kwanza waibadili mitambo yao ibadili itumie gas badala ya mafuta, tukiyafatilia yanaweza kutufikisha mahali. Haya ya kutaifisha yananipa wasiwasi

--Maazimio ya bunge
Kwanza niseme serikali imayakubali na niwapongeze waheshimiwa wabunge. Nashukuru kamati ya bunge chini ya Zitto na Filikunjombe, watu wa upinzani kufanya yale maamuzi yao, kwamba CCM ni mafisadi. Ni kweli watu hawa wanatoka CCM ila sio kwamba CCM inaridhia. Ntashangaa mbunge kulipinga hili eti kisa tu yuko CCM, bunge wengi ni CCM, kama ni kweli walikuwa hawataki hakuna azimio lingepita? Na kuna baadhi ya wabunge wa CCM waliudhika na maovu haya, wenzetu wanatafuta sifa laini kwa jambo ambalo ni letu sote.

--VIP walipouza na kupata dola milioni 78, wamelipa kodi bilioni 38. Kulikua na tuhuma za rushwa katika mchakato mzima. Yamesemwa mengi na bado hatujamaliza kuyasoma, rushwa ni kosa la jinai. Nilielekeza taarifa walizozipata wazipeleke PCCB. Nimeambiwa wanaendelea na mchakato wao. Kwa miamala, serikali inashughulika na watumishi wa umma kwa mujibu wa taratibu, maaskofu na masheikh kupewa kitu hawatuhusu, mtumishi wa umma ana masharti ya kupokea fedha. Watahojiwa na PCCB. Hushtuki asubuhi akaunti ina bilioni 1.6, milioni 80 etc. Zimeanguka kutoka juu ya mti. Huo ndo utangulizi.

--Tulitaka kufanya uchunguzi sisi wenyewe na mamlaka zetu na taarifa zimeshakuja, tunazifanyia kazi. Kuna vitu vimetokea, kuna vilivyofanyika nje na taarifa hazikuja na sasa tunalaumiana, hivyo tunafanya uchunguzi na wote waliohusuka tunawahoji na mahakama kuu ipo kesi ya PAP kumiliki hisa za IPTL, ipo kesi ya uhalali wa PAP kupokea pesa za IPTL. Hatutaki kuwaingilia ila sisi tutafanya uchunguzi wetu kwa ajili ya taarifa zetu. Tuwe na uhakika hizi hisa zimeuzwa kwa bei gani, tunataka kujiridhisha kwa sababu ipo kodi ya serikali(capital gain) na inalipwa na alieuza na sio alieuziwa. Kodi hulipwa na aliepata na sio aliepoteza (Alienunua).

--Fedha zilizotoka imelipwa PAP, akitokea mtu ana madai, serikali mnaikinga vipi. Ingetokea mtu ana madai yoyote angepelekwa PAP kulingana na makubaliano. Kukawa kuna hoja kuwa hata PAP umiliki wake wa hisa 70% unatia mashaka kutoka Mechmar, lakini waliziuza kwanza kwa kampuni ya Uingereza ambayo yenyewe ndo ikaziuza PAP. Kampuni ilikua chini ya ufilisi na kwa mujibu wa taratibu huwezi kuuza ukiwa chini ya ufilisi, kwa mujibu wa taarifa sio kweli.

--Kwa upande wa kodi ya serikali ambazo hazikulipwa, AG alipoulizwa alisema hakuna kodi iliyochelewa kulipwa. Mgogoro ni baina ya IPTL na TANESCO havyo uamuzi wa standard charted haukuweza kuingia, kwa vile haikuhusishwa, ilienda kuzuia maamuzi hayo.

--Kabla ya mzozo wa ukokotoaji TANESCO ilikuwa inailipa ITPL Moja kwa moja. Lakini hata ulipotokea mzozo bado IPTL haikuacha kupeleka madai na Tanesco haikuacha kulipa. Kuwepo kwa akaunti ya escrow haibadili mwenye fedha yake.

--Nilipokutana na mwanasheria mkuu, alisema hakukosea katika ushauri wake na wala mahakama haikufanya makosa, na kuhusu ile hasara amesema hakuna hasara yyte iliyopatikana kwa sababu pesa imelipwa kwa mtu halali.

--Jambo moja ambalo ni bahati mbaya, ilijengeka dhana kuwa akaunti kufungwa ni jambo lililoanzishwa na maafisa wa serikali kwa manufaa yao binafsi.

--Na hata TANESCO alipewa ushauri huo huo, uamuzi ule umetiliwa shaka na kuonekana haukuwa sahihi na umeitia hasara nchi. Ukaibua hisia na ni kwa sababu nzuri tu kwamba si bure na iko namna kama ya rushwa na watu kunufaika binafsi. Mara kuna watu wameenda benki na kubeba pesa kwenye sandarusi, lumbesa na mengineyo.

--Mfilisi aliagizwa kuhamisha kwa PAP kutoka IPTL ikiwemo Akaunti ya Escrow, ilizua mjadala mkali. Wizara ya nishati ilimwandikia mwanasheria mkuu kuomba ushauri, Mwanasheria akasema lipeni, uamuzi uko sawa na hauna matatizo na benki kuu wakauliza maswali hayo hayo na majibu yakawa yaleyale. Kuzingatia ushauri huo akaunti ikafungwa na pesa kukabidhiwa PAP. Mjadala ukaendelea bunguni na kwenye mablogu.

--CAG aliwaelekeza TANESCO kuacha kuhesabu pesa walizolipa kwenye akaunti ya escrow kama pesa zao, pesa hazikufikia sifa kuhesabika kama mali ya TANESCO(Asset). Mahakama kuu ya Tanzania ilifanya uamuzi katika shauri la maombi ya VIP, kusimamisha mchakato wa ufilisi wa IPTL na mahakama ikakubali.

--Kama katika fedha hizo ipo kodi ya serikali, kwa mujibu kulikua na kodi ya ongezeko la thamani ambayo haikulipwa, IPTL hawakuilipa na uthamini ulikua bilioni 21 na ushee, TRA imepeleka madai yake kwa PAP.

--Kama mgogoro ungetatuliwa na madai ya TANESCO yakakubali ya tozo kupunguzwa, kiasi kilichopunguzwa kuna pesa za TANESCO ambazo lazima zirudi kwa kiasi kilichopunguzwa. Bahati mbaya miaka saba baadae halikuwa limefanyika.

--Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, mdhibiti wa hesabu alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL, Nilipomuuliza maana, akasema zamani walikua wanalipa moja kwa moja lakini baada ya mzozo walikubaliana kwanza waziweke BoT.

--Akaunti ikafunguliwa BoT kwa ajili ya kuweka tozo ya uwekezaji, zinahifadhiwa ili kutoa nafasi kwa pande mbili kushughulikia tofauti zao lakini kabla ya hapo TANESCO walikua wanalipa moja kwa moja.

--Fedha hizi mwenyewe nani, umma au IPTL
Nianze kuelezea ya Escrow ni kitu gani, ni tofauti kidogo na akauti zetu tatu tulizozizoea, na akauti maalumu na kazi maalumu pia ikiisha na yenyewe inafungwa, inasimamia na wakala na wakala pia anajukumu la kumlipa mwenye fedha wakati ukifika.

--Kwa mujibu wa mkataba, TANESCO isipolipa inatozwa riba ya 2%, kwa mujibu wa taarifa akaunti ilikua na 202.9 bilioni na sio 309.7, hizi zilipaswa kuwepo endapo TANESCO ingelipa zote kwa wakati.

--Masharti ilikuwa kampuni ya IPTL itaendelea kupeleka madai yake TANESCO ya tozo ya uwekezaji na TANESCO itaendelea kulipa lakini yataenda escrow akaunti badala ya IPTL lakini ya umeme yaliendelea kwenda IPTL na ilifunguliwa 2006 na mpaka kesi kuamuliwa 2013 wakati IPTL inachukuliwa na PAP walikua hawajamalizana. (They decided to manage the crisis rather than resolve it)

--TANESCO na IPTL walikubaliana kuanzisha Akaunti ya Tegeta Escrow benki kuu na kuingia mkataba, wizara ya madini kwa niaba ya TANESCO na IPTL na benki kuu kama wakala.

--Rais Kikwete anaelezea kuhusu mgogoro kati ya Tanesco na IPTL mpaka kupelekea kufunguliwa kwa Akaunti ya Escrow

--Aeleza kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Rushwa naye aliagizwa na serikali kufuatilia mihamala ya Escrow na kuchukua hatua stahiki.

--Aaanza kuelezea uamuzi wa Serikali kumtaka CAG kufanya uchunguzi kuhusu akaunti ya Escrow na taarifa kupelekwa bungeni.

--Asema amelitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua kwa wale wote waliochangia vurugu katika uchaguzi huo.

--Aelezea furaha yake kuhusu uamuzi wa Mhe. Wassira kuwachukulia hatua wote waliochangia kasoro za uchaguzi wa Serikali za Mitaa ikiwemo baadhi ya watendaji kufukuzwa kazi huku wengine wakishushwa vyeo.

--Aongelea kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

--Mhe Kikwete aanza kwa kumshukuru Mkuu wa Mkoa kwa zawadi ya ujenzi wa maabara pamoja na kumtakia heri kuhusu afya yake.

--Rais Kikwete ameanza kuongea na wazee wa Mkoa wa Dar katika Ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo Watanzania wanataraji atoe mwongozo kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

MDAHALO WA KATIBA WAFANYIKA LEO MWANZA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Saturday, December 20, 2014

MDAHALO WA KATIBA WAFANYIKA LEO MWANZA.


Aliyekuwa Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akiwasili jioni ya leo katika Ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest jijini mwanza.

Umati wa watu waliojitokeza katika mdahalo wa Katiba katika Ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest jijini mwanza.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Jaji msitaafu Joseph Sinde warioba amewahutubia wananchi jijini Mwanza kuhusiana na katiba inayopendekezwa na kuwashauri wananchi hao kuisoma kwa umakini kwanza kabla ya kuipigia kura kwani kuna baadhi ya vipengele vimentofolewa katika katiba hiyo.

Akizungumza  katika mdahalo maalum ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika hotel ya Gold Crest Warioba amesema kuwa watanzania kwa pamoja wapige kura ya ndiyo kama yale waliyoyapendekeza yamo kwenye katiba na wapige kura ya hapana kutokana na kuwa yale waliyoya pendekeza hayapo katika katiba hiyo.

OFFICIAL VIDEO: ALIKIBA - MWANA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

FT: Manchester City 3-0 Crystal Palace.


David Silva scored twice as Manchester City beat Crystal Palace 3-0 to move level on points with Premier League leaders Chelsea.

The Spain midfielder struck twice in the second half on his 200th appearance for the club at the Etihad Stadium on Saturday, as the champions stretched their winning run to eight games in all competitions.

City had been toothless in the first half, with James Milner employed in an unfamiliar advance role in the absence of all of the club's recognised strikers due to injury.

They raised their game after the break, though, and Silva delivered the end product they had previously been lacking with two goals in the space of 12 minutes, before Yaya Toure added a third goal to cap another impressive display.

In the end a routine afternoon for Manchester City, though for 45 minutes it looked as if their lack of a striker was going to see them frustrated in front of their own fans.

David Silva provided the key to unlocking the Crystal Palace defence, and though he needed a deflection to open the scoring, his knowledge of playing in a system without an out-and-out frontman was plain for all to see. Without Sergio Aguero, his role in the side becomes even greater, and on this evidence he is more than ready to carry that burden.

For Palace's part, they battled bravely, but once Yannick Bolasie was shackelled they had very little to offer in the final third. Neil Warnock will no doubt be looking for a striker once the transfer window opens in 12 days.
Victory for Manuel Pellegrini's men - their sixth in succession in the top flight - ensures they join Chelsea on 39 points, with the latter facing a trip to Stoke City on Monday.

Palace were unfortunate to have a James McArthur goal disallowed for offside after Silva's second goal and Neil Warnock's team have now won just one of their last 11 games.

Pellegrini made six changes to the side that won at Leicester City last weekend, with Milner among the players to come in, while Fraizer Campbell replaced the injured Marouane Chamakh in the Palace starting line-up and Jason Puncheon was preferred to Wilfried Zaha.

Warnock said his Palace side had nothing to fear at the Etihad Stadium and they made a positive start as City struggled to get going.

Yannick Bolasie proved a real threat early on and Joe Hart did well to palm away the winger's cross as the onrushing McArthur was poised to finish from close range.

Mile Jedinak ought to have headed home an inviting corner, before Campbell spurned a great chance to open the scoring when Bolasie headed the ball on and the former Manchester United striker failed to hit the target with an acrobatic overhead kick.

City started to get into their stride with some slick passing and movement, but Silva was unable to make Julian Speroni work after Samir Nasri had burst into the penalty area and cut the ball back to the Spain midfielder.

Bolasie shot into the side-netting 10 minutes before the break as City continued to look vulnerable at the back.

Pablo Zabaleta then came agonisingly close to putting the home side in front when Toure picked him out with a sublime pass and the marauding defender scooped the ball over Speroni, but his effort was just wide.

It was a frustrating first half for the champions, but they were in front four minutes after the break courtesy of a strike from Silva.

Zabaleta was the architect, with the right-back again surging forward and unselfishly cutting the ball back for Silva, whose shot hit Scott Dann and looped into the far corner of the net.

Palace were struggling to live with City's passing and movement and Silva doubled their lead 61 minutes in, sweeping the ball home first time after Aleksandar Kolarov had picked him out with a fine cross.

The visitors had the ball in the back of the net after 66 minutes, but McArthur was wrongly adjudged to be offside after he headed home a fine cross from the impressive Bolasie.

Toure added to Palace's misery with nine minutes remaining when he fired a powerful left-footed shot past Speroni after receiving a fine pass from Milner following a swift break, as City marched on in ominous fashion.

OFFICIAL VIDEO: ALIKIBA - MWANA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

OFFICIAL VIDEO: ALIKIBA - MWANA.


MZAZI MWENZIYE NA SUGU AVAA PEMPASI UKUMBINI, JIONEE MWENYEWE HAPA.


MCHINA AMLA MATE DADA WA KIBONGO MBELE ZA WATU.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

MZAZI MWENZIYE NA SUGU AVAA PEMPASI UKUMBINI, JIONEE MWENYEWE HAPA.

Kituko! Katika hali ya kushangaza, msanii wa filamu Faiza Ally ambaye amezaa na Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, aligeuka kituko baada ya kuingia ukumbini akiwa amevalia mavazi wavaayo watoto kuhifadhi haja zao maarufu kama ‘pempasi’.

Faiza akiwa na pempasi ukumbini.

Tukio hilo lilitokea juzikati katika Hotel ya Sea Cliff iliyopo Masaki jijini Dar, ambako walialikwa watu wachache kwa ajili ya kula chakula cha jioni pamoja.

Wakati wageni waalikwa wakiwa tayari ukumbini huku wakifikiria jinsi mwenyeji wao atakavyotinga hotelini hapo, ghafla walimuona Faiza akiingia ukumbini akiwa ndani ya mavazi hayo yaliyosindikizwa na kishati kidogo alichovaa juu na kuwafanya waalikwa wote kuangua kicheko.

...Akiwa na rafiki yaake.

“Nimefikiria sana kwa nini nianze kujipa gharama za nguo na nilipomuangalia mwanangu Sasha anavaaga pempasi na mimi nikasema ngoja nifanye hivyo,” alisema Faiza.

Faiza akiwa na Sugu.

Faiza na Sugu waliodumu katika uhusiano kwa miaka mingi na kufanikiwa kupata mtoto mmoja, Septemba, mwaka huu walimwagana na sasa kila mmoja amechukua hamsini zake.

Unaambiwa Zari ampokea Diamond Kampala kwa mbwembwe zote...jionee hapa!



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

MPAMBE WA MGOMBEA URAIS AVISHWA SHANGA BAADA YA KUFUMANIWA AKINANILII KWENYE GESTI.


 JAMAA anayedaiwa kwamba ni mpambe mkubwa wa mmoja wa wagombea urais mwakani ambaye ni fundi wa kufunga madishi, mkazi wa Magomeni-Makanya jijini Dar es Salaam, almaarufu Mgosingwa, amejikuta akivishwa shanga baada ya kunaswa na mke wa mtu chumbani kwake.

Mgosingwa akivishwa shanga baada ya kufumaniwa na mke wa mtu.

FUMANIZI
Tukio hilo la aina yake la kufungia mwaka 2014 lilijiri kwenye fumanizi la jamaa huyo lililochukua nafasi nyumbani kwake maeneo ya Magomeni-Makanya, Dar, Jumanne iliyopita ambapo alifumwa na mke wa jamaa aliyejitambulisha kwa jina moja la Faki aitwaye Mwanahamisi akidaiwa kumrubuni kwa nguo za Sikukuu ya Krismasi.

Kwa mujibu wa mwenye mke, baada ya Mgosingwa ambaye mkewe alikuwa safarini, kunaswa laivu alitaka kuchoropoka kupitia dirishani lakini jamaa alimkamata miguu na kumrudisha ndani.

OFM
Kama kawa, makamanda wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publisher wanaotumia bodaboda ziendazo kasi, walitonywa na kufanikiwa kufika eneo la tukio ndani ya dakika sifuri.



OFM walipofika walikuta mtiti umeshika kasi ambapo kabla ya kufikia hatua ya kudhuriana, polisi waliokuwa doria mtaani waliitwa na wasamaria wema na kwenda kuokoa jahazi.

AVISHWA SHANGA
Polisi walipofika walimkuta mwenye mke akiwa na shanga mkononi akimvalisha Mgosingwa ambaye tayari hakuwa na ujanja.Hata hivyo, polisi hao walifanya kazi ya ziada kumdhibiti mwenye mke ambaye alikuwa akipambana nao akitaka aachiwe apambane na mgoni baada ya kumvisha shanga.

MAYOWE
“Niacheni jamani lazima na mimi leo nim….(tusi), haiwekani kabisa mtu atake kumdhalilisha mke wangu.
“Mke wangu nitajua cha kumfanya tukifika nyumbani, yaani ukweli nampenda sana mke wangu,” alisikika mwenye mke akipiga mayowe.

Dk. Wilbrod Slaa,

WAAMRISHWA WAVAE NGUO
Tukio hilo lilisababisha mjumbe wa nyumba kumi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Mama Vicky na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Makanya (hakutaja jina) wafike eneo hilo na kuwaamrisha waliofumaniwa wavae nguo kwanza.

SERIKALI YA MTAA
Baada ya kuvaa, wahusika wote walipelekwa kwenye ofisi ya mtendaji wa mtaa huo ili wazungumze na ikiwezekana wayamalize kwani wahusika hao walikuwa ‘hawajaduu’ bado.

January Makamba.

MSAMAHA
Baada ya kufika ofisi ya mtendaji, Mgosingwa alimpigia magoti mwenye mke na kumuomba msamaha huku akikiri kuwa alikuwa akitaka kula tunda la mkewe lakini alikuwa bado hajathubutu kufanya hivyo hata siku moja.

“Chondechonde kaka, mimi ni mwanaume mwenzako na wote, mimi, wewe na mkeo tunatoka pamoja pale Makorora (Tanga) na familia zetu zinajuana fika.“Naomba unisamehe ndugu yangu niko tayari kukulipa fidia ya kunishika ugoni,” aliomba Mgosingwa.

Mgosingwa aliendelea kuomba radhi ambapo mjumbe wa nyumba kumi na afisa mtendaji walimshauri mwenye mke kupunguza jazba kisha akubali kuzungumza na mgoni wake, wasifike mbali na kuyamaliza ili kuepusha usumbufu.

Benard Membe.

FAINI MIL. 1.5
Baada ya kushauriwa kwa muda mrefu, mwenye mke aliiheshimu mamlaka hiyo ya serikali na kukubali kulipwa faini shilingi milioni moja na nusu za Kitanzania ili kumsamehe mgoni na kumpa onyo kali endapo wataendeleza kamchezo hako.Baada ya hapo, Mgosingwa aliendelea kuwapigia simu ndugu zake wamtumie fedha kwenye simu ili amalize tatizo hilo.

NI MPAMBE WA MGOMBEA GANI?
Kwa mujibu wa majirani wa Mgosingwa ni mpambe wa mmoja wa wanasiasa maarufu anayedaiwa kuwa kwenye ‘resi’ za kugombea urais mwakani, kufumaniwa kwake kumetajwa pia kama ni njia mojawapo ya kumchafua mgombea huyo.Mgosingwa alipoulizwa kama ni mpambe wa mgombea gani hakuwa tayari kutaja.

Waziri mkuu Mizengo Pinda.

WANAOTAJWA URAIS 2015
Baadhi ya vigogo wanaotajwa kutaka kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 ambao wana wapambe kila kona Bongo ni pamoja na Mizengo Pinda, Benard Membe, January Makamba, Frederick Sumaye, Dk. Khamis Kigwangala, Dk. Wilbrod Slaa, Wiliam Ngeleja, Steven Wasira, Dk. Mohamed Shein, Dk. Emmanuel Nchimbi, Dk. Asha-Rose Migiro na Edward Lowassa.

Unaambiwa Zari ampokea Diamond Kampala kwa mbwembwe zote...jionee hapa!



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Wednesday, December 17, 2014

Unaambiwa Zari ampokea Diamond Kampala kwa mbwembwe zote...jionee hapa!

Zari baada ya kumpokea Diamond

Diamond Platnumz ametua Kampala jijini Uganda tayari kwaajili ya kutumbuiza Alhamis hii kwenye show ya Zari All White Ciroc Party? jijini humo. Diamond alipokelewa kwenye uwanja wa ndege na mpenzi wake Zari Ttale aka The Bosslady.
Wawili hao wamekutana kwa mara nyingine baada ya hivi karibuni kuwa pamoja kwenye tuzo za Channel O.

HII NDIO MOJA YA GARI ANAYOMILIKI HUDDAH MONROE YENYE THAMANI YA MILLION 92.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Tuesday, December 16, 2014

HII NDIO MOJA YA GARI ANAYOMILIKI HUDDAH MONROE YENYE THAMANI YA MILLION 92.


Muhalaiki Huddah Monroe anaingia tena kwenye headline baada ya kuonyesha picha ya gari lake jipya aina ya Range ambayo inathamani ya million 92 kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram na aliandika hivi
“Ombea adui yako aishi siku nyingi . Ili unapo barikiwa ajioneeeee!…. No one can block the blessings that God has planned for you because Who Jah bless , no man curse! This is a GIFT from GOD! MY Aphrodisiac,My Dime Piece, my Husband, . Christmas just came early! #Thankful!. #RangeRover #Anon #SexOnWheels #Blessings #BossChick!“– @huddahthebosschick

Wema Sepetu Alisusa Gari Aina ya Murano Alilopewa Kama zawadi na Diamond Platnumz.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Breaking news!! MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI, JAJI WEREMA AJIUZULU.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema (pichani) leo amejiuzulu nafasi yake na tayari amemwandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Jakaya Kikwete.

Rais Kikwete asema amepokea barua yake na kumshukuru kwa ushirikiano aliouonyesha katika kipindi cha utumishi wake.

Sababu ya kujiuzulu ni kwamba ushauri alioutoa kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka vizuri.

UPDATES ZA MATOKEO MIKOA MBALIMBALI YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA YALIYOKWISHA TANGAZWA HADI SASA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Wema Sepetu Alisusa Gari Aina ya Murano Alilopewa Kama zawadi na Diamond Platnumz.


LILE ndinga aina ya Nissan Murano alilozawadiwa supastaa Wema Sepetu na aliyekuwa mchumba wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’, limeanza kumchefua mrembo huyo kiasi cha kulisusa.

Tukio hilo lilijidhihirisha wazi mbele ya paparazi wetu juzikati nyumbani kwa staa huyo, Kijitonyama jijini Dar, ambapo Wema alitamka hadharani kuwa kwa sasa analichukia kupita maelezo gari hilo alilozawadiwa na Diamond kwenye sherehe yake ya kuzaliwa.

“Bwana acha nitumie hili gari lingine kwenda airport hilo Murano sitaki hata kulisikia, sijui najisikiaje hata nikiliona,” alisikika Wema.Paparazi wetu baada ya kusikia Wema akionesha wazi kuwa analichukia gari hilo, alimuuliza sababu inayomfanya alichukie ambapo alisema hajui ni kwa nini analichukia ingawa ni mali yake.

“Siku hizi sipendi kutumia hili Murano tena nalichukia kweli, inafikia kipindi nakosa raha nikiliona lakini ukiniuliza sababu ya kulichukia kiasi hicho hata sina sijui nimezoea sana kutumia BMW, ndiyo maana najikuta nalichukia gari hili,” alisema Wema.

Kwenye bethidei yake iliyofanyika Septemba, mwaka huu, Wema alizawadiwa magari mawili. La kwanza lilikuwa ni BMW 545i (Sh. Milioni 56) ambalo liliibua utata juu ya mtu aliyemzawadia na la pili ni Nissan Murano (Sh. milioni 36) alilopewa na Diamond

Inasemekana Beyonce na Jay Z wameiba wimbo wao wa ‘Drunk in Love’.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Inasemekana Beyonce na Jay Z wameiba wimbo wao wa ‘Drunk in Love’.

Mwanamke mmoja nchini Hungary amewalalamikia mastaa Beyonce  na mumewe Jay Z akidai wamemwibia wimbo wake wa ‘Drunk in Luv‘ ambao tayari aliurekodi na kwa sasa umeonekana kama wa kwao.

Mwanamuziki Monica Miczura maarufu kama Mitsou alisema Bey na Jay Z pamoja na Producer wao Timbaland waliuchukua mashairi ya wimbo huo aliourekodi mwaka 1995 kisha kuutumia bila ruhusa yake.

lovvvvvMitsou alisema hakuwapa tuhusa ya kutumia wimbo wake na mbaya zaidi wimbo huo ulitumika bila ya yeye kujua ..”Waliubadilisha sehemu ndogo sana katika mashairi yake na badala yake wakaongeza vionjo vya mapenzi,ni wimbo wangu unajulikana kwa jina la Bja,Bja Pelem“.

Mwimbaji huo alisema ana nithibitisho vyote na anataka alipwe na pia amemtaka mwanasheria wake kuzuia wimbo huo kuendelea kuchezwa mpaka hapo mashtaka yake yatakaposikilizwa.

UPDATES ZA MATOKEO MIKOA MBALIMBALI YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA YALIYOKWISHA TANGAZWA HADI SASA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Yaya wa Uganda aliyemchapa mtoto wa mwajiri wake, amehukumiwa jela miaka minne kwa kosa la kumtesa mtoto.

Yaya wa Uganda aliyejipata pabaya kwa kumchapa mtoto wa mwajiri wake, amehukumiwa jela miaka minne kwa kosa la kumtesa mtoto.

Kisa cha yaya huyu kilizua hasira miongoni mwa watu wengi katika mitandano ya kijamii pale kanda ya video iliibuka mitandaoni ikimwonyesha yaya huyo akimchapa na kumkanyaga mtoto mwenye mwaka mmoja unusu.

Jolly Tumuhirwe, mwenye umri wa miaka 22, alinaswa kwa kamera ya siri akionekana akimchapa na kumkanyaga mtoto huyo pamoja na kumzaba kofi.

Mnamo siku ya Ijumaa, Jolly alikiri kumshambuilia mtoto akisema alikuwa analipiza kisasi kwani mamake mtoto huyo naye alikuwa amezoea kumchapa.

Hata hivyo mama huyo alikanusha madai ya Jolly ambaye polisi walikuwa wamesema wangemshitaki kwa kosa la jaribio la mauaji ila kiongozi wa mashitaka akasisitiza kuwa ingekuwa vigumu kuthibitisha hilo.

Hakimu mkuu Lillian Buchan aliambia Tumuhirwe kwamba alitenda uhalifu ambao hauna hata kisingizio.

Alisema adhabu aliyompa inamtosha kulingana na makosa yake kwa kumtesa mtoto ambaye hana hatia.

Babake mtoto huyo, Eric Kamanzi alisema aliweka kamera ya siri nyumbani kwake baada ya kuwa na shauku kumhusu mfanyakazi huyo.

Kanda ya video iliyomuonyesha Jolly akimtendea unyama mtoto, ilitoka kwenye kamera ambayo Bwana Kimanzi aliweka nyumbani kwake baada ya kushuku kuwa mtoto wake alikuwa anatendewa unyama na pia baada ya kumapata mtoto wake akiwa na alama za majeruhi mwilini mwake.

Alimshitaki mwanamke huyo kwa polisi na kisha kuisambaza kanda hio kwenye mitandao ya kijamii.

Baada ya hukumu kutolewa,Kamanzi alisema: "sio juu yetu kuamua adhabu anayofaa kupewa Jolly. ''

"tunatumai kuwa hili ni funzo kwa wafanyakazi wengi wa nyumbani kwamba huwezi tu kwenda kwa nyumba ya mtu na kumtesa mtoto na kutarajia kuondoka tu kama ulivyoingia. ''

UPDATES ZA MATOKEO MIKOA MBALIMBALI YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA YALIYOKWISHA TANGAZWA HADI SASA.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

UPDATES ZA MATOKEO MIKOA MBALIMBALI YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA YALIYOKWISHA TANGAZWA HADI SASA.

 Mbozi; Mtaa Masaki: CHADEMA 99, CCM 44

Kigoma Mjini; Mtaa wa Gezaulole: CHADEMA 240, CCM 198

Ukonga- Mtaa wa Kivule Majohe: CHADEMA 231, CCM 77

Musoma Vijijini- Kijiji cha Muhoji: CHADEMA 197, CCM 464

Ubungo- Mtaa wa Msewe: CHADEMA 683, CCM 356

Kinondoni- Mwenge Nzasa: CHADEMA 344, CCM 318

Tarime Forodhani boda (kitongoji): CHADEMA 289, CCM 90

Tarime Forodhani Kijiji: CHADEMA 312, CCM 99

Monduli Mto wa Mbu Kijiji Jangwani: CHADEMA 147, CCM 124

Mwanga Kitongoji Mgagao: CHADEMA 56, CCM 32

Rorya- Mtaa Ngasaro: CHADEMA 480, CCM 360

Arumeru Mash. Mtaa wa Manyata: CHADEMA 168, CCM 91

Ubungo- Mbezi Yusuph: CHADEMA 190, CCM 163

Mwanga- Mtaa Mtahang’a: CHADEMA 116, CCM 73

Ilemela- Mtaa wa Pasiansi: CHADEMA 689, CCM 247

Karatu- Mtaa Mazingira: CHADEMA 290, CCM 130

Karatu Mtaa wa Maliasili: CHADEMA 240, CCM 77

Karatu- Mtaa wa Manyara: CHADEMA 220, CCM 170

Tarime Mtaa wa Bugosi: CHADEMA 438, CCM 138

Tarime Mtaa wa Regoryo: CHADEMA 191, CCM 75

Segerea Mtaa wa Migombani: CHADEMA 547, CCM 225

Mamlaka ya Mji mdogo Shirati-Rorya ina mitaa 9: CHADEMA mitaa 7, CCM mitaa 2

Mererani mitaa 8: CHADEMA mitaa 7, CCM mtaa 1

Magu Mjini: CHADEMA mitaa 10, CCM mitaa 7

Manispaa ya Bukoba: Mitaa 66 ndani ya Manispaa ya Bukoba, CCM wamepata mitaa 35 huku upinzani ukijinyakulia mitaa 31.

Jumla ya Wajumbe 330 walitakiwa ambapo wapinzani wamepata WAJUMBE 205 dhidi ya CCM waliopata WAJUMBE 125.

Wilayani Karagwe: Wilaya ina jumla ya mitaa/vijiji 18, Upinzani wamejinyakulia vijiji/mitaa 12 huku CCM wakipata vijiji/mitaa 6

Wilaya ya Nachingwea: Kitongoji cha Raha Leo, CCM 60 na Chadema 59.
Kitongoji cha Amani: CCM 35 na CDM 9.

Kijiji cha Mnyune: CCM 207 na CDM 20.

Monduli Magharibi: CDM 76, CCM 199.

Monduli Mjini Mashariki: CDM 57, CCM 88 na Mtaa wa Sabasaba CDM 84, CCM 172.

Kitongoji cha Mandela, Kata ya Mkalama: CCM imeshinda kwa kura 240 na CDM 196.

Kitongoji cha Kichangani Kata ya Gairo Mjini: CCM 260, CDM 115 zilozoharibika 2.

Wilaya ya Kyela: Orodha ya Vitongoji na chama kilichoshinda
Butiama- CHADEMA
Kyela kati -CHADEMA
Roma -CHADEMA
Mikoroshoni -CCM
Mbugani -CHADEMA
Nazareti -CHADEMA
Unyakyusa -CCM
Kapwil- CCM
Itunge mashariki -CCM
KEIFO -CCM
OROFEA -CHADEMA
SAMA B -CCM
Mikumi -CHADEMA
Mwaikambo -CHADEMA
Kilasil- CCM
Mkombozi -CHADEMA
Bondeni A-CCM
Bondeni B-CHADEMA
Itunge-Mundekesye CHADEMA

Tarime; Mtaa wa Bhughucha: CHADEMA 135, CCM 123

Tarime; Mtaa wa Buhemba: CHADEMA 104, CCM 50

Tarime; Nyarusahi: CHADEMA 197, CCM 54

Tarime; National: CHADEMA 170, CCM 130

Tarime; Kijiji Nyabitocho: CHADEMA 899, CCM 315

Segerea; Migombani: CHADEMA 547, CCM 225

Huko Mvomero hadi sasa kati ya Vijiji 20 vya awali

CHADEMA Vijiji 15
CCM Vijiji 5

Vijiji hivyo 15 ni; Sarawe, Lungo, Kidudwe (nyumbani kwao mbunge wa Mvomero), Mndelwa, Masili, Ndugutu, Lukunguni, Mwalavi, Mvomero, Bumu, Madizini, Doma, Mlali, Tchenzema na Nanyinga (nyumbani kwa Mwenyekiti wa Halmashauri- CCM).

VURUGU SIMIYU: Watu 600 wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chadema wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Simiyu wakihusishwa na vurugu za uchaguzi wa serikali za mitaa jana.

Kabla ya kukamatwa hapo jana kati ya saa 2 – 3 asubuhi, polisi walilazimika kuwatawanya wafuasi hao wa Chadema kwa mabomu ya machozi walipokuwa wakipinga uchaguzi kufanyika leo badala ya kufanyika jana kama ilivyopangwa.

Kutokana na kulipuliwa mabomu ya machozi, huduma za usafiri wa mabasi kutoka na kuelekea Mwanza, Musoma, Bunda, Tarime, Simiyu zilisimama.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Charles Mkumbo alipopigiwa simu kutoa kauli kuhusu sakata hilo, hakupokea simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu hakujibu.

Takwimu uchaguzi: Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa taarifa ya Takwimu ya mambo yaliyotokea wakati wa kampeni za Uchaguzi Serilali za Mitaa.

Takwimu hizo zinaonyesha kuwa Mkoa wa Tabora unaongoza kwa ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi ukifuatiwa na Kagera wakati Shinyanga na Mbeya wakifanya vizuri.

Kwa upande mwingine takwimu zinaonyesha kuwa kukosekana kwa mwamko wa kisiasa 19%, kampeni kuisha baada ya muda 18%, ratiba za kampeni kuwa wazi 12%, rushwa kwa wapiga kura10%, huku kampeni kuzuiwa na mamlaka 1% na vitisho kutoka kwa watu wasio vyombo vya dola 1%.

Mgombea Chadema atumbukia shimoni, afariki: Aliyekuwa mgombea ujumbe katika Kituo cha Msalala Road, Geita kupitia Chadema, Bethar Nchimani Ngosha amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye shimo la choo lililokuwa limejaa maji.

Baada ya kutangaziwa kuwa ameshinda, marehemu alikuwa anaelekea uani, karibu na choo kulikuwa na shimo la choo lililokuwa wazi ndipo alipodumbukia na mauti kumpata.

Akataa kusaini: Mtaa wa Katoma Geita Mjini wananchi wamekesha kusubiri matokeo.Mgombea wa CCM ameshindwa na amekataa kusaini matokeo.

Mabomu yatumika: Jeshi la Polisi limeamua kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi mkoani Mwanza katika maeneo ya Pasians, Mji Mwema, Kirumba, Ibungiro na Kitangiri baada ya vurugu wakati wa kusubiri kutangazwa matokeo.

Kijiji cha Muungano Kata ya Chahwa mkoani Dodoma: CHADEMA 196, ADC 38

Mbozi; Mtaa wa Masaki: CHADEMA 99, CCM 44

Kigoma Mjini; Mtaa wa Gezaulole: CHADEMA 240, CCM 198

Ukonga; Mtaa wa Kivule Majohe: CHADEMA 231, CCM 77

Musoma Vijijini; Kijiji cha Muhoji: CHADEMA 197, CCM 464

Ubungo; Mtaa wa Msewe: CHADEMA 683, CCM 356

Kinondoni; Mwenge Nzasa: CHADEMA 344, CCM 318

Mwanga Mtaa wa Lwami: CHADEMA 55, CCM 35

Mererani: CHADEMA imeshinda mitaa 7 kati ya 8

Kitongoji cha Endulele: CHADEMA 170, CCM 130

Monduli; Kitongoji Kambi ya Mkaa: CHADEMA 27, CCM 13

Mwanga Mtaa wa Lwami: CHADEMA 55, CCM 35

Arumeru Magharibi, Kitongoji Endulele: CHADEMA 170, CCM 130

Ushirombo Mjini: CHADEMA inaongoza vitongoji 10, CCM inaongoza vitongoji 4

Moshi Manispaa, Kitongoji Longuo A: CHADEMA 206, CCM 66

Mbozi Mtaa wa Mbugani: CHADEMA 227, CCM 160

Kata ya Mji Mpya, Morogoro yenye mitaa 12, CCM imeshinda mitaa 9, CHADEMA wakishinda mtaa 1 huku mitaa miwili mpaka sasa bado vurugu zimetanda baada ya kura kudaiwa kuzidi huku watu kadhaa wakituhumiwa kupiga kura mara mbili.

Kagondo, Kata ya Muhutwe, Kagera: CHADEMA imeshinda mitaa 4 kati ya 5

Kufungwa Vituo: Katika maeneo mengi vituo vya upigaji kura tayari vimefungwa huku wananchi wakisubiri kwa hamu kujua matokeo.

Uchaguzi Migombani: Uchaguzi wa Serikali za Mitaa eneo la Migombani, Segerea jijini Dar umeingia dosari baada ya Afisa Mtendaji Kata ya Segerea kutangaza kusitisha uchaguzi huo kimyakimya bila sababu za msingi ambapo wananchi waliamua kumweka mtu kati mpaka akaruhusu uchaguzi huo kuendelea kwa maandishi. Akijitetea afisa huyo alidai kuwa ameagizwa na Mkurungenzi wa Uchaguzi wa Manispaa ya Ilala kufanya hivyo.

Mazimbu, Morogoro: Eneo la Mazimbu, Moro kimenuka mpaka wanajeshi wamelazimika kuingilia kati kutuliza ghasia wakati wa zoezi la upigaji kura.

Kawe, Dar: Uchaguzi wadaiwa kuingia dosari baada ya mgombea wa CCM kutoa amri ya vitabu kufungwa kabla ya muda ulipangwa.

Kigogo, Dar: Mgogoro umezuka katika Kituo cha uchaguzi Kigogo jijini Dar baada ya wananchi kudai kuwa baadhi ya watu wamepelekwa kama mamluki eneo hilo kwa ajili ya kugipa kura.

Sokoine-Kibaoni, Morogoro: Wananchi eneo la Sokoine-Kibaoni, Wilaya ya Mvomero, Morogoro mpaka sasa bado hawajaanza kupiga kura mbali na wengi wao kujitokeza huku wengine wakiwa wamekodi magari kutoka Bwawa la Kihonda umbali wa kilomita 20 kwenda kupiga kura lakini mpaka sasa bado hawajapiga kura.

Amana, Ilala: Baadhi ya wananchi wameamua kususia zoezi la upigaji kura katika Kituo cha Amana, Ilala jijini Dar baada ya mgombea Uenyekiti wa Mtaa wa Amama aitwaye Mathias Ijumba kuondolewa katika uchaguzi dakika za mwisho kwa kile kinachodaiwa kuwa si mkazi wa eneo hilo lakini jambo la ajabu jina like liko katika orodha ya watu waliojiandikisha kupiga kura na mgombea huyo ameruhusiwa kupiga kura yake.

Baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamedai jamaa huyo anakubalika sana na huenda ndiyo chanzo cha jina lake kuondolewa.

Dar es Salaam: Wananchi katika vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam wanalalamikia utaratibu wa majina unaotumika katika zoezi la upigaji kura linaloendelea, wengi wadai kupata tabu kuona majina yao huku wengine majina yao yakiwa hayapo kabisa katika vituo.

Shariff Shamba, Ilala: Eneo la Shariff Shamba, Ilala jijini Dar uchaguzi umeahirishwa mpaka Jumapili ijayo baada ya vifaa kutopatikana ndani ya muda muafaka. Vyama vyote vinavyoshiriki vimeafikiana.

Kagunga, Kigoma Kaskazini: Uchaguzi katika Vijiji vya Zashe na Kagunga, Kata ya Kagunga, Jimbo la Kigoma Kaskazini umefutwa hadi itakapotajwa tena baada ya Mtendaji wa Kata kuwaengua ACT katika uchaguzi huo baada ya kudaiwa kuwa wagombea wawili wa vijiji hivyo kutoka ACT walitumia anuani ya shule kama anuani yao. Hata hivyo Msimamizi Mkuu amesema anafuta uchaguzi hadi watakapotangaza tena.

MCHINA AMLA MATE DADA WA KIBONGO MBELE ZA WATU.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...
 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top