Friday, January 31, 2014

Chezea CCM wewe: Kinana na Mangula wawasili Mbeya Kwa Maadhimisho ya miaka 37 ya CCM.

 
Mangula (katikati) akiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (kulia) pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Godfrey Zambi.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangula akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum, Dk. Mary Mwanjelwa baada ya kuwasili leo asubuhi kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya , tayari akwa maadhimisho ya miaka 37 ya CCM yatakayofanyika kitaifa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya Jumapili Februari 2. Kushoto ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati) akizungumza na Nape (kulia) pamoja na Zambi kwenye chumba cha watu mashuhuri (VIP) alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, Mbeya leo mchana, ttayari kwa maadhimidho hayo

 
Dk. Mary Mwanjelwa (kushoto) akijadiliana jambo na Makmu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Dogo Idd Mabrouk wakati wa mapokezi hayo   

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

"NAHISI NIMEAMBUKIZWA H.I.V"..NAHITAJI USHAURI TAFADHALI


Mimi ni kijana, umri wangu ni kati ya 25-30. Ni mhitimu wa chuo kikuu. Ni msaarabu, najiheshimu na napenda maendeleo.
 
Nipo kwnye mahusiano imara, japo tupo mikoa tofauti na tupendana sana na girlfriend wangu & recently tumeanza taratibu za utambulisho nyumban japo si rasmi.
 
Hivi karibuni nimepatwa na tukio la ajabu, kuna rafiki yangu wa kike way back toka primary scul tulikuwa tunawasiliana kawaida as normal friends lakin kumbe mwenzangu alikuwa na hisia za mapenz kwngu,,alipoona simtamkii akaamua avunje ukimya, nikamwambia haiwezekan na sabab nikampa..alilia sana akaomba 2fanye kwa siri coz hata yeye ana boyfrnd bt yupo mbal bt nikabak na msimamo wngu.
 
akaomba tuonane japo tuongee, nikakataa lakin akaforce kuja home (nlikuwa peke yang) coz alikuwa anapajua,,kafika home hana jipya, alipoona nmegoma kabsa akaanza kunfanyia fujo(sexual harassment) akavua nguo zote tufanye ngono, nikajikaza kiume nikamvalisha nguo & nikamtoa nje, too bad nlisahau funguo za gate ikabidi nirud ndan kumbe mwenzang ananfata nyuma pasi na kujua,,akaanza fujo tena & this time nlizidiwa nguvu & we had sex, unprotected sex..i was raped na mwanamke.
 
Nlilia sana that day nikapanga safar kwnda kumwambia my girl coz hatufichan ki2 (kwnye sim nilishindwa),ucku huo yule mwanamke akantext kuwa nikijaribu kumwacha atamwambia girlfriend wngu, cjui alichukua phone no. mda gani,,ikabid niwe mpole..then akanambia "too late" kuulza ana maana gan akawa anacheka.
 
Nilimwambia my friend lawyer akacma kesi ngumu coz tukio lilitokea hme so ngumu kuprove a rape..after 1 month nikaanza kupata symptoms za ajab, nikaenda kuchek STI (ckupima HIV) nikawa sina bt nlipata UTI, nkafuatilia zile dalili na kugundua ni related na Acute HIV, nkaogopa sana, nikaanza kumkwepa girlfriend wang kila akipanga safar natfta excuse, nia yangu itimie 3 months...i 

knw knowldge z power & najua kila kitu kuhusu HIV japo si dokta, najua i can live 30 years, najua the cure is near or imepatikana bt held in disguise,berlin patient,missisipi baby(cured of HIV) bt God AM FREAKED OUT, juz imetimia 3 months naogopa kwenda kupima, ntamwambia nin girlfrnd wng kama nmeathirika, ataniacha,,i'l be alone...am not too weak to kil myself or kill anyone..nmeamua kumsameh aliyenfanyia huu uchaf nmemwachia Mung,,all my life nimeishi vizur(mbal na vishawish) only God knows haya majaribu yana maana gani,,
Nimechanganykiwa naombeni msaada wa mawazo, nmejiunga huku walau niitoe moyoni nipate relief coz naogopa kuambia watu...I've got no one to talk to
habari kamili :: read more...

Loo! Kumbe lile zee lilolobabwa LIVE gesti likinanilii na binti limefanikiwa kuwakimbia na kutokomea mitini.


AIBU YA MWAKA: Babu akifunga shati baada ya kunaswa live kumbe kichani anampango ulikamili wa kutoroka.
Mzee huyo alinaswa laivu akiwa gesti na denti wa shule moja ya sekondari jijini Dar (jina la denti na shule vinahifadhiwa kimaadili). 

Tukio hilo la aibu lilijiri juzikati kwenye gesti moja iliyopo maeneo ya Kawe, Dar na kusababisha timbwili zito.


TAARIFA MEZANI KWA OFM
Hivi karibuni, kikosi maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) chini ya Global Publishers, kilipokea lalamiko kutoka kwa mzazi wa denti huyo ambaye alieleza juu ya mabadiliko ya mwanaye kitabia na kushuka kitaaluma kutokana na kusumbuliwa na ‘mbaba’ huyo.

Mzazi huyo aliiambia OFM kuwa amekuwa akifuma mawasiliano ya kwenye simu ya mkononi ya mwanaye na mwanaume huyo ambaye alikuwa hamfahamu.
 


 
FUNDISHO KWA WAZEE: Babu akijiandaa kuvaa nguo yake ya ndani baada ya kunaswa gesti.
CHANZO
Mama huyo alisema kuwa kutokana na maendeleo ya mwanaye kuzidi kudorora shuleni, aliamua kumfuatilia kwa karibu kwa kuwa hakutaka apotee.
Mama huyo alitiririka kuwa, siku ya tukio, alimsikia mwanaye huyo akiwekeana miadi kwenye simu na mwanaume huyo ndipo akaamua kumuwekea mtego.

Alisema wakati mwanaye huyo akilonga kwenye simu, yeye alibana sehemu na kuyasikia yote ambayo alikuwa akiyaongea na kwamba walipanga kukutana baa.
“Nilichokifanya nilimpigia simu mjomba wake na kumweleza kila kitu, nikamwelekeza namna ya kumfuatilia. Alichukua bodaboda na kuanza kumfuatilia. Mimi na timu yangu tulifuata nyuma,” alisema mama huyo kwa uchungu.
Alisema mzee huyo alikubaliana na mwanaye wakutane kwenye baa hiyo ambapo ndani yake kuna nyumba ya kulala wageni a.k.a gesti.

OFM YAITWA
Baada ya mpango wa mtego kukamilika ndipo mama huyo akawaita OFM ambao huwa hawalazi damu hivyo walifika mara moja.

TAARIFA POLISI
Kabla ya kuchukua hatua yoyote, walishauriana kutoa taarifa kituo cha polisi, jambo ambalo lilifanyika na kupatiwa msaada wa kiusalama.

NI SAWA NA BABU YAKE

Walipofika kwenye baa hiyo mama mtu alipigwa na butwaa kumuona mtu aliyekuwa akiwasiliana na mwanaye ni mzee sawa na babu yake.


“Yaani jamani kweli dunia imekwisha, mwanangu ni sawa na mjukuu wa huyu mzee, ama kweli tamaa mbaya sana,” alisema mama huyo kwa uchungu.
Huku wakifuatiliwa kwa karibu, mzee huyo na denti walipiga madikodiko na vinywaji ndipo wakatimba kwenye gesti hiyo.

Kilichofanyika ni kwamba polisi na mama wa denti walizama gesti hiyo na kuomba kumsaka mwanafunzi huyo, jambo ambalo halikupingwa.
FUMANIZI LAIVU

Baada ya kuzama ndani ndipo mtego ukafyatuka ambapo mzee Omari alibambwa katika moja ya vyumba vya gesti hiyo huku akiwa amejifunga taulo tu.


Mzee huyo alipatwa na taharuki kubwa asijue la kufanya kufuatia timbwili zito alilozua mama wa denti huyo.
“Kha! Kazi kuharibu watoto wa wenzenu, hivi angekuwa wa kwako ukakuta akifanyiwa hivi ungejisikiaje? Nasomesha kwa gharama kubwa wewe unataka kuniharibia. Hivi hujui mtoto anauma?” alihoji mama huyo kwa hasira huku akimtandika mwanaye vibao.
OMBI


Mara baada ya mzee huyo kunaswa, aliomba chondechonde kukaa na familia ya mwanafunzi huyo ili kuyamaliza yasifike mbali.


Hata hivyo, baada ya maombi ya muda mrefu walikubaliana kuandikishiana ambapo mzee huyo alitakiwa kulipa faini.
“Sisi hatuna maneno mengi, hatutaki kesi ila atulipe fidia ya kumsababishia mtoto wetu asiwe na mahudhurio mazuri shuleni kutokana na ulaghai wake,” alisema mzazi huyo.

MZEE AINGIA MITINI


Habari zilieleza kuwa mzee huyo alishindwa kulipa mara moja badala yake aliingia mitini kwa kigezo kuwa anakwenda kutafuta faini hiyo.


Hadi OFM inaondoka eneo la tukio mzee huyo alikuwa hajawasilisha faini waliyokubaliana hivyo tunafuatilia na tutakachobaini tutaandika katika matoleo yajayo
.
FUNDISHO
Hivi sasa kumeshamiri tabia ya wazee kupenda kuharibu mabinti wadogo hivyo kunaswa kwa mzee huyo litakuwa fundisho kwa wengine kwani OFM ambao huwa haikosei, imeamua kulivalia njuga suala hilo. Subirini muone!

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

ZITTO KURUKA KAMA CHADEMA


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
USHINDANI wa kisiasa kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umefikia hatua mpya baada ya CCM kuibuka na mkakati wa kumtumia Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kupambana na CHADEMA waziwazi.
Katika mkakati huo CCM imepanga kukodisha helikopta ya kumpeleka Zitto katika mikoa minne kwa gharama ya sh milioni 50 mara tu baada ya CHADEMA kuhitimisha Operesheni yao ya M4C Pamoja Daima.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vilivyo karibu na Zitto na CCM, yeye na chama hicho sasa wana adui mmoja – CHADEMA; na wameamua kujibu mapigo baada ya kuridhika kwamba kwa vyovyote Zitto amekwisha kupoteza uanachama wake katika CHADEMA.
Nia yao ni kumtumia Zitto kuleta mpasuko katika CHADEMA, na kufunika mjadala wa mgogoro wa CCM, kero za wananchi na mchakato wa Katiba mpya.
Zitto ambaye alivuliwa nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA – Naibu Katibu Mkuu Bara, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mjumbe wa Baraza Kuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni – anatarajia kutumia helikopta yenye uwezo wa kubeba watu wanne, ambayo inadaiwa kukodishwa na wapinzani wa CHADEMA.
Kwa mujibu wa habari hizo, lengo la ziara ya Zitto ni kujibu mapigo ya CHADEMA, hasa katika maeneo ambayo baadhi ya makada na viongozi wa chama hicho wamepita na kuzungumzia hatima yake kisiasa, hasa walipojibu maswali ya wananchi kuhusu sakata lake kuvuliwa uongozi kwa tuhuma za usaliti, na hatimaye Zitto kwenda mahakamani kuzuia chama kujadili uanachama wake.
Katika kesi ya msingi, Zitto aliyewahi kuwa maarufu akiwa kiongozi wa CHADEMA, anaomba arudishiwe nyadhifa zake zote, na apatiwe nakala za uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ili aweze kukata rufaa Baraza Kuu.
Taarifa zinasema tayari chama kimempatia nyaraka hizo, lakini kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA, Zitto amekwisha kujiondoa kwenye chama hicho kwa kupeleka shauri mahakamani.

Taarifa za Zitto kuanza ziara mikoani zilianza kusikika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mikoa iliyotajwa ni Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Morogoro na Dar es Salaam, ingawa maandalizi yanaendelea na kuna uwezekano wa kubadili baadhi ya mikoa kulingana na mkakati wao.

Kwa hadhi yake ya sasa, CHADEMA imeshasema haitahusika na mikutano yake, na wanachama wake hawatajihusisha nayo. Uratibu wa mikutano yake unafanywa na viongozi waandamizi wa CCM.

Baadhi yao walizungumza na gazeti hili kwa kujitapa kwamba hii ndiyo njia ya kuimaliza CHADEMA, lakini hawakutaka kutajwa majina gazetini.

Iwapo Zitto atakubali ufadhili huo wa CCM na kuendelea na mikutano yake, ni wazi atakuwa amekamilisha ushahidi wa kinachodaiwa na chama chake kwamba amekuwa akikisaliti kwa masilahi ya CCM.

Hata hivyo, baadhi ya viongozi wa CCM walipoombwa maelezo juu ya urafiki wao na Zitto kiasi cha kumkosanisha na chama kilichomlea kisiasa, CHADEMA, walisema kwamba urafiki uliopo si wa Zitto na CCM, bali Zitto na Rais Jakaya Kikwete.

Gazeti hili linafahamu kwamba wakati fulani mwaka juzi Zitto alipobanwa na wabunge wenzake kuhusu tabia zake za kuwasaliti kwa Rais Kikwete, alisisitiza kuwa Rais Kikwete ni rafiki yake binafsi, kwa hiyo wamwelewe.

Vilevile, wapo wanaohoji nia ya ziara hii wakati kwa muda mrefu amekuwa akikwepa kuambatana na viongozi wenzake katika ziara na operesheni nyingi za kichama.

Wanasema kwa kuwa operesheni ya sasa ya CHADEMA imepewa jina la M4C Pamoja Daima, kitendo cha CCM kuandaa ziara ya Zitto na kumkodishia helikopta, ni uthibitisho kuwa Zitto hayuko pamoja na CHADEMA tena.

Wameongeza pia kuwa kama hilo litafanyika, litakuwa limemwingiza Zitto katika orodha ya makada kadhaa wa upinzani waliotumikia CCM baada ya kufukuzwa au kunyimwa fursa za uongozi katika CHADEMA, kama Tambwe Hiza, Dk. Aman Walid Kabourou na Dk. Masumbuko Lamwai.

Alipotafutwa athibitishe kuhusu ziara hii na kama ni kweli inafadhiliwa na CCM, Zitto hakuweza kupatikana.

Mbowe kuwania tena uenyekiti

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema kuwa kamwe hatakiacha chama hicho katika uchanga wa harakati za kulikomboa taifa kama kiongozi wake wa juu.

Akihutubia katika mikutano ya Operesheni M4C Pamoja Daima katika sehemu mbalimbali mkoani Morogoro jana, mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa, bado atagombea nafasi ya uenyekiti kwa lengo la kuendeleza harakati za ukombozi wa pili wa taifa hili.

Bila kutaja jina, Mbowe alionya kuwa wenye fikra za kuachiwa chama hicho kikiwa katikati ya ukombozi huo hawatapata nafasi, kwa sababu hawana nia thabiti ya kukiendeleza, bali wana nia ya kukibomoa kwa kutumiwa na wapinzani wa CHADEMA.

“Makamanda, kumbukeni kuwa chama hiki na sisi viongozi wake tumepita katika majaribu makubwa na hata kukoswakoswa kuuawa. Mimi nimekoswakoswa kuuawa kwa bomu huko Arusha, lakini pia kuna watu wamepoteza maisha, wamefungwa jela, wengine wamekuwa vilema, halafu watu wengine wanatusaliti kwa kupewa visenti ili wakivuruge chama na wanataka tuwape chama. Huu ni uendawazimu,” alisema.

Mwenyekiti huyo alisema CCM imekuwa ikifanya jitihada za kuihujumu CHADEMA kwa mbinu mbalimbali, zikiwemo za kupandikiza migogoro, jambo ambalo limeshindwa kufanikiwa kwani Mungu ameweka mkono wake ili kisisambaratike.

“Harakati hizi tunazofanya za kuwakomboa Watanzania mjue tunahatarisha maisha yetu, tumejaribiwa kushawishiwa ndani na nje ya Bunge ili tuwe kondoo, tumekataa. CCM wamekuja na mbinu za kupandikiza migogoro wameshindwa na sasa wanaomba nife wakifikiri nikifa na CHADEMA itakufa. Nawaambia CHADEMA haifi kwa kuwa tumezalisha makamanda wengi, watakiendeleza,” aliongeza Mbowe.

Akielezea kwa mara ya kwanza kwa undani zaidi kuhusu mauaji ya Arusha, mwenyekiti huyo alisema wana ushahidi wa kutosha kwamba polisi walihusika na mauaji hayo na kuongeza kuwa waliohusika ni polisi wa kutoka mkoani Morogoro.

“Kwa mara ya kwanza niliseme hili, mauaji ya Arusha yaliyofanyika kwa kurusha bomu katika mkutano wa kampeni za CHADEMA, yalifanywa na polisi ambao walitoka mkoani Morogoro. Ndiyo maana tunaendelea kumwambia Rais Jakaya Kikwete aunde tume ya kimahakama ili kupata ukweli wa jambo hili,” alisema.

Kuhusu Katiba
Akizungumzia msimamo wa CHADEMA kuhusu muungano, Mbowe alisema chama hicho kinaunga mkono maoni yaliyokusanywa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba, ya serikali tatu.

Alisema hata tafiti mbalimbali zilizofanyika, zikiwemo za wanasheria na wachumi zinaonyesha kuwa Muungano utaimalika zaidi chini ya muundo wa serikali tatu.

“Nawaonya Wana CCM wasijaribu kuingilia mjadala wa Bunge la Katiba na kama wanataka nchi ichimbike, basi walazimishe serikali mbili,” alisema Mbowe.

“Zipo tetesi za CCM kutaka kupitisha hoja zao kwa nguvu kutokana na idadi yao ndani ya wabunge zaidi ya 600, wakiwemo 356 wa Bunge la Tanzania Bara, 84 kutoka Zanzibar na 201 kutoka makundi mbalimbali watakaokwenda kwenye bunge hilo. Wasidanganyike kwamba wanaweza kutumia wingi wao kubadilisha maoni ya Watanzania kuhusu serikali tatu,” alisisitiza Mbowe.

Halima Mdee anguruma

Naye Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, ambaye yuko katika msafara wa mwenyekiti huyo, alisema vijana wengi wanaochipukia katika siasa kupitia chama hicho, wamelelewa na Mbowe, ambao leo wamekuwa chachu ya mabadiliko nchini.

“Ukweli ni kwamba kamanda huyu wa anga (Mbowe), ndiye ametulea vijana wengi nikiwemo mimi, tena wengine hatukuwa na ujasiri tulionao sasa, asiwadanganye mtu, hasa sisi vijana kwamba tuliingia CHADEMA na umaarufu, hawapo hao, tumelelewa na huyo kamanda,” alisisitiza huku akipigiwa makofi.
CHANZO NI TANZANIA DAIMA

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

A-Z ya MSANII BONGO MOVIES ALIVYOJINYONGA

SAKATA la kujinyonga kwa msanii wa filamu Bongo, Victor Peter limegubikwa na matukio tofauti ya kustaajabisha ambayo marehemu aliyafanya siku kadhaa kabla hajapatwa na umauti, Ijumaa limefukunyua kila kitu.

Mwili wa marehemu Victor Peter ukipelekwa mochwari.
Kwa mujibu wa rafiki wa marehemu, Hamisi Koba, msanii huyo alijinyonga usiku wa Februari 27, mwaka huu mkoani Tanga ambapo marehemu alifika jijini humo kuigiza filamu yake iitwayo Our Family.
Hamisi alisema Victor aliwasili jijini humo akiwa na timu ya wasanii sita na kufikia kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Safari Junior iliyopo maeneo ya Kisosora ambapo punde walianza kushuti filamu hiyo ambayo yeye na Mzee Jengua ndiyo walikuwa wahusika wakuu.
 
Marehemu Victor Peter enzi za uhai wake.
“Mimi ndiye nilikuwa kama mwenyeji wake mkubwa hapa Tanga, alikuwa ni mpole na siku zote tulipokuwa kazini kwa ajili ya kushuti filamu hiyo aliniambia mambo mengi kuonesha amejipanga kuhakikisha anaifikisha mbali.
“Victor alitokea Mwanza, akaenda Dar ambapo alifika na kuandaa filamu yake ya kwanza aliyoiita Chozi ambayo tayari ilikuwa imekamilika na kuiuza kwenye Kampuni ya Kapiko ya jijini humo,” alisema Koba na kuongeza:
“Filamu hiyo ilikuwa bado haijatoka, akaamua kuja Tanga kuandaa filamu hiyo ya pili ambayo nayo ilikamilika juzi. Naumia sana ninapokumbuka mipango yake maana alikuwa ana ndoto za kufanya makubwa.

“Siku ya Januari 27 tulipokuwa tunakamilisha filamu, kuna muda alikuwa anaonekana kama ana wenge hivi... alipomaliza kushuti sehemu yake tulienda benki, akachukua fedha na kuwalipa wasanii wote.”
Akiendelea kutiririka juu ya tukio hilo, Koba alisema marehemu alionesha kama alikiona kifo chake kabla kwani aliuliza mara mbilimbili kama kuna mtu anamdai ili amlipe.
“Wakati anatupatia fedha kila mara alikuwa anauliza kama kuna mtu anamdai hadi tuliingiwa wasiwasi na ingawa wengine walisema atakuwa amefurahia labda kumaliza muvi yake,” alisema.
Koba alizidi kueleza kuwa, marehemu akiwa na furaha ya kumaliza muvi hiyo, alikwenda chumbani kwake na kujifungia lakini alfajiri (Januari 28) walipomgongea mlango waligundua amejinyonga.


Baadhi ya mashuhuda wakiwa eneo la tukio.
“Tulichungulia kupitia tundu la funguo tukaona kama ananing’inia ndipo tukaenda kwenye kituo cha Polisi cha Chumbageni na kuchukua askari ambao walishirikiana na mwenye gesti hiyo kuvunja
mlango na kumkuta kajinyonga, tukachukua mwili na kuupeleka kwenye Hospitali ya Bombo, mipango ya kuusafi risha mwili kwenda Kahama nyumbani kwao imeanza,” alisema Koba na kuongeza:
“Kwenye hiyo filamu yake, stori ilikuwa mzee Jengua kama baba wa Victor ambapo Mzee Jengua alikufa na baadaye Victor anakufa kiajabu, kifo kimempata kweli.”
Kuhusiana na kifo hicho, Koba alisema kilimuuma kwani alikilinganisha na kile kilichomtokea marehemu Steven Kanumba ambaye pia aliigiza filamu ya Power of Love ikionesha anakufa, akafa kikwelikweli.
Mwili wa marehemu uliokuwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Bombo ulitarajiwa kusafi rishwa juzi kwenda nyumbani kwao Kahama kuzikwa.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

WASTARA: NIKIKUMBATIWA NAKUWA HOI: wewe ukikumbatiwa unakuaje???

 Wastara Juma.
MSANII wa filamu, Wastara Juma amefunguka kuwa starehe yake kubwa duniani ni kukumbatiwa na anapofanyiwa kitendo hicho na mtu wa jinsia yoyote huwa hoi.



Akistorisha na paparazi wetu, Wastara alisema: “Mimi napenda sana kukumbatiwa au kukumbatia, awe ni mwanaume au mwanamke, ndugu yangu au hata kama siyo ndugu yangu, tukikumbatiana tu najisikia raha sana.


“Unajua kila mtu anakuwa na kitu anachokipenda duniani sasa mimi starehe yangu ndiyo hiyo hata marafiki zangu wanajua kwamba mimi napenda kukumbatiwa.”

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Baada ya Pombe kumkolea Mke wa mtu apiga Picha za UCHI GESTI; wajanja wa baa wamla uroda.

Wanasema Pombe sio Chai Mke wa mtu aamua kupiga picha za uchi na kufanya mapenzi kwenye Gesti maarufu Jijini Mwanza.

Inshu kamili ilikuwa hivi baada ya kuonekana mwanamke huyo ambaye kwa haraka hakufahamika jina lake aliingia kwenye gesti hiyo ambayo inatoa huduma ya vinywaji na kuanza kupata moja moto moja baridi.

Baadaye kidogo aliingia mwanaume wa makamo.ndipo walipojumuika pamoja na kendelea kugonga glass.

Mnamo majira ya saa mbili usiku alionekana mwanaume akiingia ndani ya gesti hiyo na mwanamke kumfuata kilichoendelea tazama picha hizo chini.









habari kamili :: read more...

Thursday, January 30, 2014

Mzee Malecela amuunga mkono Paul Makonda Adai Edward Lowassa anakivuruga chama.

Mzee Malecela atoa tamko: Amuunga mkono Paul Makonda. Adai Edward Lowassa anakivuruga chama kwa tamaa ya urais

TAARIFA YAKE HII:
Ndugu zangu waandishi wa habari, awali ya yote naomba niwasalimie na niwapongeze kwa kufika -mwaka mpya 2014, pia naomba niwapongeze kwa kazi kubwa ambayo mmekuwa mkiifanya hasa kuhakikisha watanzania wanapata habari kwa kila jambo linaloendelea kila kona ya taifa letu la Tanzania.

Ndugu waandishi wa habari nimewaita hapa ili kuzungumza nanyi na mnisaidie kufikisha ujumbe kwa watanzania hasa kuhusu jambo hili ambalo limekuwa gumzo kwa watanzania wengi la mbio za urais 2015 kwa baadhi ya watu ndani ya chama changu cha mapinduzi (CCM), kilichonisukuma zaidi na kupata hamu ya kuongea nanyi ni baada ya kumsikia -na kumuona kijana wetu ndani ya chama cha mapinduzi bwana Paul Makonda akiwa na ujasiri wa kukemea vitendo mambo haya yanayofanywa na baadhio ya viongozi bila uwoga wowote naomba tuchukue fursa hii kumpongeza sana kijana huyu.

Nadiriki kusema nampongeza kijana huyu hasa kwa kauli zake nzito na za kijasiri kwa maslahi ya chama changu cha CCM ili chama kiendelee kupendwa na kuchaguliwa na watanzania.

Pia itakuwa si busara kama sitawapongeza vijana wangu katibu mkuu wa chama ndugu ABDULRAHMAN KINANA na NAPE NNAUYE kwa juhudi zao za dhati za kujenga chama na kuendelea kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya chama cha mapinduzi (CCM) kwa kuwakemea viongozi wasiofaa bila kujali cheo na umaarufu wao ndani ya chama na serikali, nawaomba waendelee -na juhudi zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watru wanaowabeza naomba wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ndani ya chama na serikali ni msingi wa chama chochote kilichounda serikali.

Aidha nawaomba watanzania wenzangu wazalendo wasikubali kukatishwa tama na kikundi cha watu wachache wasio na mapenzi mema na taifa letu ambalo limekuwa mfano wa kuigwa kwa amani, upendo, utulivu na mshikamano urithi tulioachiwa na baba yetu wa taifa mwalimu julias kambarage nyerere ndani na nje ya mipaka ya bara letu la afrika.

Ndugu zangu waandishi wa habari naomba niwaambie kuwa msemaji wa UVCCM kijana wetu Paul Makonda namuunga mkono kwa -kitendo chake cha ujasiri cha kumkemea ndugu EDWARD NGOYAI LOWASSA bila uwoga kwa jinsi anavyokivuruga chama chetu kwa lengo la kutaka urais 2015 huku secretariet ya chama ikiwa imekaa kimya wakati inajua kuwa muda wa kuanza mbio hizi bado na kufanya hivi kwa sasa ni kukiuka misingi na katiba -ya chama. Hapa najiuliza kuwa ile misingi imara ya uongozi ndani ya chama chetu cha mapinduzi iko wapi? Mpaka tumuachie mototo ndio akemee haya? Je, hapa chama kiko wapi?

Ukweli ni kwamba wanachama wetu na vijana wamekuwa njia panda huku wakitamani kusikia tamko au karipio la chama juu ya suala hili la harakati za urais 2015 bila mafanikio.

Naomba niseme kuwa bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia pesa zao hadharani kwa lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa vijana ili kupata madaraka wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya chama.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuona juhudu za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni pamoja na sekretarieti inayoongozwa na katibu mkuu ABDULRAHMANI KINANA na katibu mwenezi NAPE NNAUYE za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga.

Ninaomba juhudi hizi zisibezwe na watu wenye nia njema na chama. Ukweli ni kwamba vijana hawa wamekuwa na juhudi kubwa sana ya kujenga na kuimarisha chama chetu -kwa wananchi kila pembe ya taifa letu kwa kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. Swali: Je! Chama hakioni haya mpaka vijana ndio waone?

Kwa hili ni lazima tubadilike ili kujenga chama chetu na naishauri -secretariet ya chama lazima ichukue hatua mara moja, kijana huyu paul makonda asingesema haya yote kama hana uhakika wa ushahidi wa wa haya aliyoyasema na nampongeza sana.

Vijana na wanachama wengi wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka kujua msimamo wa chama chao bila mafanikio na ndio sababu ya baadhi ya-wengine kupoteza mwelekeo.

Sisi tulikijenga chama hiki kwa taabu sana hapakuwa hata mtu mmoja aliyediriki kutumia fedha zake kutaka madaraka. Nidhamu, busara na uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa maslahi ya wananchi ndio vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi ndani ya chama na serikali, ndio maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka kutekwa na wenye fedha kwa uchu wa madaraka, mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi pesa wanatoa wapi? Na haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa maslahi ya nani? Huku watanzania wakiendelea kuwa maskini.

Mfano hivi karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana kwenye vyombo vya habari,vitendo hivi havina tija kwa chama na wala havileti umoja na mshikamano ambao umedumu ndani chama kwa muda mrefu.

Mwisho Ninaomba sekretarieti ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu makonda na kweli kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi kwamba utaleta kutokuelewana ndani ya chama kusiko kuwa na lazima.


JOHN SAMWELI MALECELA

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

SOURCE: JAMII FORUM:

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Kazi imeaanza: Naibu waziri wa fedha atembelea ofisi ndogo ya Hazina Njombe.

 
Naibu Katibu Mkuu CCM Bara,Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Njombe wakati alipotembelea Ofisi Mpya ya Hazina Ndogo Mkoa wa Njombe mapema leo Asubuhi ya Tar.30/01/2014

 
 
Naibu Katibu Mkuu CCM Tanzania Bara Mh;Mwigulu Lameck Nchemba akibadilisha mawazo na Mkuu wa Wilaya wa Wanging'ombe Wakati wakitoka Kutembelea Ofisi Ndogo Mkoa wa Njombe.
Mh;Mwigulu Nchemba akioneshwa moja ya Chumba cha Mapokezi ya Wageni kwenye Ofisi za Hazina Ndogo.


Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Mwizi achomwa moto LIVE Mchana wa leo HUKO KAGONGWA KAHAMA


WANANCHI WA KATA YA KAGONGWA WAKISHUHUDIA JINSI MWIZI ALIVYOCHOMWA MCHANA HUU
Tutakujulisha zaidi baada ya kuchanganua vizuri habari hii usifunge page hii
habari kamili :: read more...

Hawa jamaa sasa wanazingua;Eti Helikopta yao ilipotea juzi.Wanaleta siasa hadi angani?

HELIKOPTA ya Chadema maarufu kama Chopa, juzi ilipotea angani na kusababisha viongozi wa chama hicho kushindwa kufanya mkutano katika Kijiji cha Mpwayungu wilayani Chamwino, kama ilivyokuwa imepangwa kwenye ratiba.

Kwa mujibu wa ratiba iliyokuwa imepangwa, viongozi wa kitaifa ambao ni Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (BAVICHA), walikuwa wafanye mkutano katika kijiji hicho saa 4 asubuhi.

Akizungumza na MTANZANIA, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Dodoma, Steven Massawe alikiri kupotea kwa helikopta hiyo na kukanusha kwamba hakuna njama zozote zilizofanywa na CCM kutokana na kupotea kwa helikopta hiyo.
 Kijiji cha Mpwayungu kipo katika Kata ya Mpwayungu, ambayo nafasi ya udiwani ipo wazi na vyama vya Chadema na CCM vyote vimesimamisha wagombea.

“Sababu kubwa ya kupotea kwa helikopta ni tatizo la mawasiliano kama mnavyojua Kijiji cha Mpwayungu hakina mawasiliano. Helikopta ilikuwa ifike katika Kijiji cha Mpwayungu saa nne asubuhi, lakini Kapteni alipotea na kusababisha kukaa angani kwa saa moja na dakika arobaini na akatua Kijiji cha Chipogolo.

“Alipofika Chipogolo akaambiwa sio kijiji hicho chenye mkutano na akatakiwa kurudi nyuma kwa upande wa magharibi kwa kilometa 40, hata hivyo hakufanikiwa ikabidi arudi mjini kujaza mafuta,” alisema Massawe.

Alisema baada ya kujaza mafuta, viongozi hao hawakwenda tena kufanya mkutano Mpwayungu badala yake wakaenda Mpwapwa ambapo kulikuwa na mkutano mwingine saa 7 mchana kwa mujibu wa ratiba.

“Leo (jana) hii viongozi hao kwa kutumia helikopta wamekwenda tena Mpwayungu na kufanikiwa kufanya mkutano majira ya saa nne asubuni na baada ya hapo waliekea Kijiji cha Segala Wilaya ya Chamwino, baadaye wataenda Kiteto na Moshi,” alisema.

Alisema sio kweli kwamba CCM walifanya njama helikopta ya Chadema ipotee ili isifanye mkutano katika kijiji hicho na kwamba Chadema na CCM vyote vilishafanya uzinduzi wa kapteni katika kata hiyo.

“Chadema ilifanya uzinduzi wake wa kampeni katika Kata ya Mwayungu, Januari 26 mwaka huu na CCM walifanya uzinduzi wao Januari 20,” alisema Massawe.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, amesema iwapo Serikali ya CCM haitaweka mazingira ya haki kwa makundi mbalimbali ndani ya jamii kwa ajili ya amani ya kudumu, migogoro ya ardhi italitumbukiza taifa katika sintofahamu na hatari kubwa nchini.

Dk. Slaa aliyasema hayo kwenye mikutano ya M4C Pamoja Daima, jana alipokuwa akiwahutubia wananchi wa maeneo ya Iselamagazi, Kishapu, Mhunze, Itilima, Lugulu na Bariadi.

Alisema ni haki kwa wananchi kuwa na matumaini, kwani ndiyo misingi wa amani ya kweli ambayo haihitaji kuhubiriwa jukwaani.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Chezea White man wewe!!!! Shilole anasa kwa Mzungu.



Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na mchumba wake.
KWA mara ya kwanza msanii wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amenaswa akiwa na mwanaume wa Kizungu anayedaiwa kuwa ndiye mchumba wake.
 
Chanzo makini kimepenyeza habari kuwa, safari za mara kwa mara za Shilole nchini Uingereza zimekuwa zikisababishwa na mchumba huyo wa Kizungu ambaye huwa anamuita kufurahia penzi lao pamoja na kumtafutia shoo mbalimbali.

“Ukweli ni kwamba Shilole ana mchumba wa Kizungu na walikutana kwenye shoo ya mara ya kwanza aliyoenda kufanya nchini Uingereza na hivi karibuni ataenda tena na amealikwa na huyo mchumba wake,” kilisema chanzo hicho.

Gazeti hili limekuwa la kwanza kunasa picha kadhaa za Shilole akiwa katika mapozi tofauti ya kimahaba na Mzungu huyo.

Baada ya chanzo hicho kumwaga ‘upupu’ huo, mapaparazi wetu walimtafuta Shilole ili aweze kufunguka ambapo bila kuumauma maneno, alikiri kuwa amepata mchumba huyo aliyemtambulisha kwa jina la Ankar.

Akizidi kumwaga data za boifrendi wake huyo, Shilole alisema awali walikutana kwenye moja ya shoo zake nchini humo ndipo urafiki ulipoota mizizi na kufikia hatua ya kuwa wapenzi.

“Kweli nina mchumba Mzungu ambaye ni raia wa Uingereza, nilipokuwa napataka nimefika, sipindui tena. Unajua muziki wangu na mauno yangu yanawavutia sana watu, siku ya kwanza aliniona kwenye shoo akanipenda ndipo tukaanzisha urafiki.

“Hivi karibuni nina safari ya kwenda nchini humo kwa mwaliko maalum alionipa, nitaenda peke yangu kwani safari nyingine zote zilizopita nilikuwa naenda na watu,” alisema Shilole.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Haaaaa!! Hii sikuipata hii: kitovu cha uchafu wa ngono katika Garden Murilo.<..Reposted..>


Hakika  huu ndo mwisho wa dunia........Huu  ni  uchafu  ambao hufanyika  katika  Garden moja ijulikano kwa  jina  la  Murilo.......

Ni  kitovu  cha uchafu,  laana, maasi  na  dhambi  zooooooote   unazozijua  hapa duniani........

 










Hiyo ni  kambi ya Vigogo,wanasiasa  na  wasanii  mbali mbali  toka  Tanzania, Kenya na Uganda.......
Kahaba  ni kahaba tu......Malaya  ni  malaya tu.  Hakika  wanadamu tumeasi.Iko haja  ya  kumrudia  mwenyezi mungu........
 Kitovu  cha uchafu huo kipo Kenya

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Faraja Kota: Siwezi kumshauri mume wangu katika kazi yake.


MISS Tanzania 2004, Faraja Kota amefunguka kuwa kamwe hawezi kuingilia kazi za mumewe ambaye ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kwani anaamini mumewe ana akili nyingi kuliko yeye.

Akizungumza na paparazi wetu, Faraja alisema siyo rahisi kuingilia kazi za mume wake zaidi ya kuzungumza naye kidogo sana kama kuna kitu amekiona anaweza kumshauri kwa sehemu fulani lakini siyo kwa kiasi kikubwa sana.

Lakini alisema mume wangu anaporudi nyumbani anakuwa ni baba zaidi na sio waziri hivyo masuala ya kifamilia namshauri kidogo.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Vijana changamkia hi:Billionea atangaza dau la paundi 40million kwa atayemuoa bintiyake msagaji.

 
Na Mwandishi Wetu, Kwa Msaada wa Mtandao
KATIKA
 Hali ya isiyo kuwa ya kawaida, Bilionea wa Hong Kong ametangaza dau la zaidi ya Paundi 40 milioni kwa mwanaume yeyote anayeweza kumuoa binti yake msagaji.

Mfanyabiashara huyo wa meli za biashara na mizigo na muendelezaji majengo Cecil Chao Sze –Tsung anaonekana kuchoshwa na mahusiano yabinti yake Kiki kwa binti mwingine wa kike kwa karibu miaka tisa.
Mfanyabiashara huyo wa Hong kong alikuwa na nia ya kumrithisha himaya yake binti yake huyo lakini kwa masharti ya kuolewa katika desturi za kistaarabu na siyo kuwa na mahusiano na mwanamke mwenzake.


Taarifa zinasema kwamba kwa kuangalia ukubwa biashara yake na amewapa baadhi ya makampuni zake wanawe wengine wawili na fedha za kutosha, lakini tajiri huyo Chao anataka wanawe wawe na maadili mema katika jamii na sitabia za ovyo.
Chao mwenye umri wa miaka 77 aliliambia gazeti la Malaysia Nanyang Siang Pau kwamba angeweza kutoa fedha mara mbili ya hizo katika kuvutia wanaume wengi kujitokeza kwa ajili ya kumuoa mwanae.
Binti huyo anaonekana kama amechanganyikiwa kwa uamuzi wa baba yake kumpa masharti ya kuolewa kabla ya kurithi mali na fedha taslimu za baba yake.
Amesema kwamba fedha si kitu cha kumvutia mwanaume au yeye kumpenda mwanaume kwa sababu ya kupenda ni utashi wa mtu binafsi.


“Napenda kuwa na furaha kufanya urafiki na mtu yeyote tayari kuchangia kiasi kikubwa cha fedha kwa jamii na upendo wangu ni kwa watu wote na si kwa sababu ya fedha za baba yangu,” amesema.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya maendeleo ya Cheuk Nang, ambaye pia ni mwanaharakati wa LGBT anasema kwamba kwa kipindi kirefu watu wamekuwa wakikiuka haki za mashoga na ndiyo sababu ya kushirikiana karibu na Big Love Alliance ambacho ni kikundi cha kutetea haki za mashoga Hong Kong na kutaka haki za mashoga kuwa sheria na kupitishwa na serikali.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Wednesday, January 29, 2014

Matokeo ya Vodacom premier League ya leo haya hapa:Yanga washushwa kileleni.


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC wameshushwa kileleni mwa ligi hiyo leo kufuatia kulazimishwa sare ya bila kufungana na Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. 
Matokeo hayo yanaifanya Yanga itimize pointi 32 baada ya kucheza mechi 15 na kuipisha Azam FC kileleni, ambayo imetimiza pointi 33 baada ya kuifunga Rhino Rangers bao 1-0 leo.   Mchezo ulisimama mara mbili kwa dakika moja na ushei ili kupisha zoezi la uokotaji wa chupa za maji zilizojazwa mikojo na tupu zilizorushwa uwanjani na mashabiki wa timu hizo.
Kwanza ilikuwa dakika ya 29, mashabiki wa Yanga waliporusha chupa baada ya kukerwa na kitendo cha mshika kibendera nambari moja kumezea kitendo cha beki wa Coastal Union Juma Nyosso kuunawa mpira uliopigwa na Didier Kavumbangu katika eneo la hatari.

Dakika tisa baadaye, mashabiki wa Coastal nao walirusha chupa langoni mwa Yanga kufutia timu yao kushambuliwa na Wana Jangwani. 

Yanga SC ilitawala mchezo kipindi cha kwanza na Coastal walitawala kipindi cha pili.
Huo unakuwa mchezo wa nne Yanga SC kucheza chini ya kocha wake mpya, Mholanzi Hans van der Pluijm ikishinda mechi mmoja tu.

Awali Mholanzi huyo aliyefukuzwa fukuzwa timu kibao Ghana na St George ya Ethiopia kwa matokeo mabaya kabla ya kutua Jangwani, alitoa sare mbili katika ziara ya Uturuki na akashinda dhidi ya Ashanti United kwa taabu 2-1 Jumamosi katika Ligi Kuu.

Katika mchezo wa leo uliotawaliwa na vurugu za mashabiki, kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Frank Domayo, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbangu, Mrisho Ngassa/Nizar Khalfan dk83 na David Luhende/Jerry Tegete dk66.

Coastal Union; Shaaban Kado, Hamad Juma, Abdi Banda, Juma Nyosso, Mbwana Bakari, Jerry Santo, David Lyanga, Crispian Odula, Lutimba Yayo/Mohammed Miraj dk88, Haruna Moshi na Kenneth Masumbuko/Mohamed Soud dk78.


Mbeya City 1-1 Ruvu Shooting
 Nayo Mbeya City ilipunguzwa kasi na Ruvu Shooting baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi ikiwa ni pointi ya kwanza kwa kocha Tom Olaba tangu aanze kuinoa Ruvu.
Ruvu walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Jerome Lembeni kabla ya Jeremia John kusawazisha. Mabao yote yakifungwa katika dakika 15 za awali za kipindi cha kwanza.


AZAM FC 1-0 Rhino Rangers
  AZAM FC imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia ushindi wa bao 1-0 jioni hii dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Bao pekee la Azam limefungwa na mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche dakika ya 26 kwa shuti kali baada ya kuukuta mpira uliozuiwa na mabeki wa Rhino, kufuatia shuti la ndugu yake kutoka nchi moja, Ismael Kone.

Azam sasa inafikisha pointi 33 na kupanda kileleni, ikiiteremsha Yanga iliyolazimishwa sare ya bila kufungana na Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga leo ambyo sasa inakuwa na pointi 32.    

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...

Picha za Jengo la JMC lilivyonusurika kuungua na moto leo:





 Wafanyakazi kutoka Kampuni ya Ultimate Security wakiwa eneo hilo kuongeza nguvu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick (kulia) akipata maelezo ya awali kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa Jeshi la Polisi.


Maofisa mbalimbali wa Jeshi la Polisi wakiwa eneo la tukio.
JENGO la JMC linalomilikiwa na Zhihir Shivji lililopo eneo la Kamata mtaa wa Kasanga, Kiriakoo jijini Dar es Salaam leo majira ya saa nane mchana lilinusurika kuteketea kwa moto ulioanzia ghorofa ya saba.
Chanzo cha moto huo na mali zilizoteketea mpaka sasa bado havijafahamika.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick alifika eneo la tukio na kuagiza wamiliki wa majengo kuweka vyombo vya kutambua hitilafu mbalimbali kwenye majengo yao.
Katika tukio hilo hakuna majeruhi yeyote aliyeripotiwa.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

habari kamili :: read more...
 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top