Wafanyakazi kutoka Kampuni ya Ultimate Security wakiwa eneo hilo kuongeza nguvu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick (kulia) akipata maelezo ya awali kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa Jeshi la Polisi.
Maofisa mbalimbali wa Jeshi la Polisi wakiwa eneo la tukio.
JENGO la JMC linalomilikiwa na Zhihir Shivji lililopo eneo la Kamata mtaa wa Kasanga, Kiriakoo jijini Dar es Salaam leo majira ya saa nane mchana lilinusurika kuteketea kwa moto ulioanzia ghorofa ya saba.
Chanzo cha moto huo na mali zilizoteketea mpaka sasa bado havijafahamika.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick alifika eneo la tukio na kuagiza wamiliki wa majengo kuweka vyombo vya kutambua hitilafu mbalimbali kwenye majengo yao.
Katika tukio hilo hakuna majeruhi yeyote aliyeripotiwa.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment