Sunday, July 12, 2015

MATOKEO YA UCHAGUZI NI John Pombe Magufuli 87%, Balozi Amina Ali 10% na Asha-Rose Migiro 3%.

July 12 2015 Tanzania ilikuwa inasubiri kwa hamu kujua Mgombea yupi anasimamishwa na CCM kwenye nafasi ya Urais 2015, ninayo Ripoti nyingine kutoka Dodoma sasahivi!!
Kura zimepigwa na Wajumbe wa Halmashauri Kuu CCM na matokeo yako hivi
 John Pombe Magufuli 87%, Balozi Amina Ali 10% na Asha-Rose Migiro 3%.

Katika Mkutano Mkuu uliofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Dodoma, Dk. Magufuli amechaguliwa kwa kura 2104 sawa na asilimia 87.08, akifuatiwa na Balozi Amina Salum Ali aliyepata kura 253 sawa na asilimia 10.4 na Asha-Rose Migiro aliyepata kura 59 sawa na asilimia 2.44702.


Jumla ya kura zilizopigwa kwenye Mkutano Mkuu wa CCM kumchagua Mgombea atakayepeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi Mkuu wa 2015 ni kura 2422, kura zilizoharibika ni sita, kura halali walizopigiwa wagombea ni 2416.
habari kamili :: read more...

Tuesday, July 7, 2015

Ramadhani Singano "MESSI wa Bongo" huru kusajiliwa na Timu yoyote.

HATIMAYE Shirikisho la soka Tanzania limethibitisha kuwa mchezaji Ramadhani Singano ‘Messi’ kuwa yupo huru na anaweza kusajiliwa na timu yeyote itakayo muhitaji baada ya klabu yake aliyokuwa akiichezea siku za nyuma Simba kushindwa kutekeleza baadhi ya vipengele vilivyopo kwenye mkataba.

habari kamili :: read more...
 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top