Thursday, February 12, 2015

MHE. WASIRA AAMUA KUMWONA NGOWI ILI AMTENGENEZEE SUTI ZAKE.



Mhe. Stephen Wasira akichukuliwa vipmo vya suti na mbunifu wa mavazi, Sheria Ngowi.

BAADA ya kuandamwa sana katika mitandao ya kijamii kuhusu kutofunga vizuri vifungo vya suti yake,
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Stephen Wasira ameamua kumuona mbunifu wa mavazi wa kimataifa, Sheria Ngowi ili aanze kumtengenezea suti zake.

Waziri Wasira akijaribu kurekebisha suti yake iliyokosewa kufungwa vifungo na kuzua mjadala mitandaoni.

Mhe. Wasira ameamua kukutana na mbunifu huyo aliyeanza mara moja kumchukua vipimo vyake ili amtengenezee mavazi yake ambayo atakuwa akiyatumia katika shughuli zake mbalimbali za kiserikali.

Picha za Waziri Wasira zilienea mitandaoni alipopiga picha ya pamoja akiwa na Viongozi wa Kanisa la Kisabato kwenye Uwanja wa Taifa, Dar huku koti la suti yake likiwa limekosewa kufungwa vifungo.
Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walirusha picha mbalimbali zikimuonesha Mhe. Wasira huku mmoja wa watangazaji akisema kuwa iwapo akikubaliwa, atajitolea kuwa wabunifu wa suti zake za mitoko ili jambo hilo lisijitokeze tena.

Mhe. Wasiara akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kanisa la Kisabato kwenye Uwanja wa Taifa, Dar huku koti la suti yake likiwa limekosewa kufungwa vifungo.

Kwa kuamua kumuona Sheria Ngowi, Mhe. Wasira atakuwa amepata mti shamba wa tatizo hilo lililotawala mitandao ya kijamii hivi karibuni.

U.S. Leads 12 Air Strikes Against Islamic State – U.S. Military.

UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Wednesday, February 11, 2015

U.S. Leads 12 Air Strikes Against Islamic State – U.S. Military.

The United States and its coalition partners has struck four units of Islamic State militants amid 11 air strikes in Iraq since early Monday, the U.S. military said in a statement while speaking with journalists, Reuters inclusive.

The strikes, near seven Iraqi cities including Tal Afar, Kirkuk and Bayji, also hit an Islamic State bunker, fighting positions, a checkpoint and other targets, said the statement released on Tuesday.

sponsored post

The U.S.-led coalition also conducted one air strike in Dayr az Zawr, Syria, hitting an Islamic State vehicle, the statement said.

EXCLUSIVE: TEVEZ AFUNGUKA ALIVYOTESWA.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Chibok girls have not yet released – Defence HQ.

Abuja (NAN) – The Defence Headquarters (DHQ) has said that “the story circulating in respect of the release of the Chibok girls is not true.”

The clarification is contained in a statement posted on the DHQ website on Tuesday.

According to the statement, the buses that drove into the barracks in Maiduguri purportedly carrying the girls were conveying other individuals.

The News Agency of Nigeria (NAN), however, learnt that the DHQ would soon address newsmen on some of the recent developments in the counter-insurgency campaign. Many terrorists were said to have died in the campaign, while many were captured by troops and some others willingly surrendered themselves.

EXCLUSIVE: TEVEZ AFUNGUKA ALIVYOTESWA.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Tanzania Yasikitishwa na Uamuzi wa Kenya wa kuzuia magari ya kitalii ya Tanzania.

Serikali imeelezea kusikitishwa na uamuzi wa Kenya wa kuzuia magari ya kitalii ya Tanzania kwenda kuchukua na kushusha watalii wanaotumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, kwa kusema kuwa hatua hiyo haijengi wala kuendana na dhamira njema ya mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe alisema jana kuwa,  dhamira ya kuanzishwa upya kwa jumuiya hiyo haiendani  na tukio la aina hiyo.

Hata hivyo alisema kwamba Serikali ya Tanzania itaendelea kuheshimu na kuzingatia amri iliyotolewa na Kenya ili kulinda undugu na urafiki uliopo kati ya nchi hizo huku wakitafakari hatua za kuchukua kuondoa bughudha iliyotokea kwa watalii na wasafiri wanaopitia uwanja huo.

Waziri Mwakyembe alieleza kwamba Serikali ya Tanzania itaendelea na mchakato ulioanzishwa wa kuhusisha wadau wote wanaoguswa na tatizo hilo hadi kufikia  uamuzi ambao utauwasilisha kwa Serikali ya Kenya kupitia vikao rasmi vya Jumuiya.
Hata hivyo, alisema pamoja na kwamba amri hiyo ya Serikali ya Kenya inakwenda nje ya mkataba wa 1985 kwa kuvihusisha hata viwanja vya ndege kuwa sehemu ya vivutio vya utalii, Serikali ya Tanzania itaheshimu na kuzingatia amri hiyo ili kulinda undugu na urafiki uliopo kati ya nchi hizo mbili.
Alisema pia kwamba Serikali itatafakari hatua za kuchukua ili kuondoa bughudha kubwa itakayotokea kwa watalii na wasafiri wanaokuja nchini wanaopitia uwanja huo wa Jomo Kenyatta.
Alizitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kuwafahamisha watalii na wageni wote wenye nia ya kutembelea vivutio vya kitalii vya Tanzania kutumia viwanja vingine vya ndege ili kuepuka kadhia na gharama zisizo za lazima.

Waziri huyo alisisitiza kuwa viwanja vya ndege hasa vile vya kimataifa vitaendelea kuwa sehemu ya milango ya kuingilia na kutokea kwenda kokote ndani ya Jumuiya au nje ya Jumuiya na havitachukuliwa kama vivutio vya utalii.

"Tanzania haitazuia magari ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki au nchi nyingine yoyote kuingia katika viwanja vyake vya ndege kuleta au kuchukua watalii wanaopitia katika viwanja hivyo na kwenda katika nchi zao," alisema.

Dk Mwakyembe ambaye ni Waziri mpya kwenye wizara hiyo alisema mkataba wa mwaka 1985 kati ya Tanzania na Kenya ulilenga kutoa mwongozo wa ushirikiano katika Sekta ya Utalii kati ya nchi hizo mbili.

Aliongeza kuwa makubaliano hayo yalielekeza maeneo muafaka kwa ajili ya kubadilishana watalii huku ikizingatiwa kuondoa bughudha kwa watalii.

Maeneo hayo ni pamoja na miji ya mipakani na miji rasmi iliyopendekezwa na kukubalika na pande zote mbili ikiwemo Nairobi ambako Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Jomo Kenyatta kipo.

EXCLUSIVE: TEVEZ AFUNGUKA ALIVYOTESWA.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Thursday, February 5, 2015

EXCLUSIVE: TEVEZ AFUNGUKA ALIVYOTESWA.

EXCLUSIVE! Kile kisa cha mtalaka wa mwimba taarab mahiri Bongo, Aisha Ramadhani Nkongo ‘Isha Mashauzi’, Jumanne Hassan ‘Tevez’ kuteswa na kudhalilishwa nchini Afrika Kusini kisa kikidaiwa ni kudhulumu mzigo wa wafanyabiashara wenzake kimeingia awamu nyingine!
Kwa mara ya kwanza Gazeti Pendwa la Amani Tanzania limeweza kuzungumza na Tevez kwa dakika arobaini na tano kutokea nchini humo ambako anauguza majeraha.

Majeraha ya mgongoni aliyopata, Jumanne Hassan ‘Tevez’ wakati wa kuteswa.

KWANZA SIKU YA TUKIO
Kabla Tevez hajasimulia kilichompata na hali yake kwa sasa, ni muhimu kukumbuka kuwa, tukio hilo ambalo lilikuwa habari ya Jiji la Dar es Salaam, lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo picha zake zilizagaa zikimuonesha akiwa amefungwa kamba huku mwili wake ukiwa umetapakaa damu na majeraha kadhaa.

AMANI LAMSAKA
Kwa vile habari za tukio hilo ziliandikwa na baadhi ya vyombo vya habari bila kupata balansi (uwiano) na Tevez mwenyewe, Amani liliingia kazini kumsaka mhanga huyo usiku na mchana.

MSIKIE SASA
Akizungumza kwa hisia kali na gazeti hili juzi, Februari 3, mwaka huu kutoka Mji wa Durban, Afrika Kusini, Tevez alisema:
“Kusema ukweli tukio lililonikuta watu huko nyumbani (Bongo) wanalitafsiri tofauti sana. Nimesikia kwamba wanasema eti nilidhulumu mzigo wa mtu, ndiyo maana niliteswa! Si kweli.”

‘Tevez’ akiwa salama nyumbani kwake.

UKWELI NI UPI?
“Ishu iko hivi, mwenyeji wangu hapa Durban, anaitwa Ibra, ndiye ambaye alinipokea siku nilipotua hapa.
“Huyu bwana inaonekana  ni tamaa. Aliniundia njama, aliita wenzake na kuniteka kisha kunitesa sana wakidhani nina pesa nyingi.
“Niliteswa sana kwa kweli. Kama mlivyoona picha. Nilidhalilishwa sana, lakini katika yote ukweli sijadhulumu mzigo wa mtu.”

ULICHOPOTEZA KATIKA UTESWAJI
 “Katika mateso yangu, walifanikiwa kunipora Dola za Marekani elfu 14 (kama shilingi milioni 22) na Landi za Afrika Kusini elfu 3 (shilingi 480,000) zikiwemo simu zangu mbili aina ya Sumsung na Nokia ambayo nilikuwa naitumia sana kuwasiliana na watu wangu muhimu.”

HAIKUWA KAZI RAHISI
Tevez akazungumzia jinsi jamaa walivyomkamata: “Jamaa siku wananiteka usiku kiukweli nilipambana nao sana hadi wanafikia hatua ya kunizidi nguvu na kunifunga kamba. Nilikuwa nimewachapa kwelikweli ila kwa vile walikuwa wengi na walikuwa wakitumia silaha nilijikuta nikiishiwa nguvu baada ya kunipiga na kitu kizito kichwani nikapoteza fahamu, nilipojitambua ndiyo nikakuta wamenifunga kamba.”

KINACHOKUUMA NINI?
“Tukio linaloniuma zaidi ni yule jamaa ambaye anaonekana katika picha amekaa jirani na mimi, hana shati. Alinichoma pasi mgongoni, namchukia sana lakini nimemwachia Mungu.”

‘Tevez’akiwa na mwanaye.

KUHUSU KUKATWA NYETI, KUFANYIWA KITU MBAYA
Tevez: “Nasikia watu huko Tanzania wanazusha eti nimekatwa nyeti, si kweli kabisa. Mimi nimepigwa na kuchomwa pasi wala hakuna kitu kama hicho zaidi ya kunichoma na pasi.
“Nimesikia wengine wanasema nimetobolewa macho, huo ni uzushi wa watu tu! Mimi niko safi na hali yangu ya kiafya inaendelea vizuri.”

SABA WAMEKAMATWA
Tevez tena: “Nashukuru sana serikali ya huku wameweza kunisaidia kwani mpaka sasa ninapoongea na wewe Musa Mateja hawa jamaa wamekamatwa saba.
“Jana (Jumatatu) walifikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka ya kunishambulia na kupora fedha. Wanatarajiwa kurejea tena mahakamani baada ya siku 7, ingawa nimeambiwa kesho (jana Jumatano) wataletwa Polisi Central ya huku kwa ajili ya mimi kuwatambua zaidi.”

BONGO LINI TEVEZ?
“Bongo natarajia kurudi Alhamisi (leo) au Ijumaa (kesho) kama mambo yangu yatakuwa kwenye mstari ila pia sasa hivi natarajia kuwasiliana na balozi wetu ili nijue kama ana taarifa zangu na namna ambavyo ataweza kunisaidia kama kiongozi wangu.”

HALI YAKO KWA SASA
“Kusema ukweli naendelea vizuri ni majeraha tu ambayo hata hivyo yanakauka. Ila hili la pasi mgongoni ndiyo  linasumbua kwa mbali, lakini naamini litakaa sawasawa.”

This Woman has refused to Smile for 40 years to avoid wrinkles.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

AUNTY: WANAOSEMA NIMEJIFUNGUA NI MAPEPO.

STAA wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel amewabwatukia watu waliomzushia kuwa amejifungua na kusema kuwa anawaona kama wametumwa na mapepo wabaya.

Staa wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel.

Akizungumza na Centre Spread, Aunty alisema anawashangaa wanaokurupuka na kuzungumza kitu ambacho si cha kweli kabisa na kwamba hakuna mtu ambaye alikuwepo siku aliyopata ujauzito huo.

“ Nafikiri watakuwa na mapepo wabaya hao wanaozungumza kitu ambacho si cha kweli.  Hakuna mtu ambaye anajua nilipata ujauzito lini na nitajifungua lini, waniache kabisa,” alisema Aunty.

This Woman has refused to Smile for 40 years to avoid wrinkles.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Muendesha pikipiki apigwa rirasi shingoni na kuporwa pikipiki mkoani Morogoro.

Mtu mmoja mikocheni wilayani mvomero mkoani Morogoro ameuwawa kwa kupigwa risasi shingoni na kisha kuporwa pikipiki aina Boxer ambapo jeshi la polisi linawashikilia watu watatu waliohusika na tukio hilo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amesema jeshi la polisi lilifika katika eneo la tukio nakufanikiwa kuwakamata watu watatu wanasadikiwa kujihusisha na tukio hilo na linaendelea kuwahoji kisha watafikishwa mahakamani.

Aidha kamanda Paulo amesema jeshi la polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa aliye kimbia ambapo katika hatua nyingine wamefanikiwa kumkamata hawara wa mtu huyo aliyejulikana kwa majina ya Husuna Isimaeli mkazi wa mkindo ambaye alikuwa akimhifadhi mtuhumiwa  na jeshi la polisi litaendelea kumshikilia kwa mahojiano ilikumpata mtuhumiwa aliye kimbia.

This Woman has refused to Smile for 40 years to avoid wrinkles.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Tuesday, February 3, 2015

This Woman has refused to Smile for 40 years to avoid wrinkles.

It's 40 years now and this woman has neither smiled nor laughed. At nights out with friends she has made a conscious effort not to laugh or smile. Even with champagne flowing and their conversation gets more raucous and peals of laughter hang over their table.

There’s always an odd one out in the happy scene. Tess, 50 sits stony-faced while her friends giggle around her. Not even a flicker of smile, let alone a laugh, escapes her lips.



She has made a conscious decision for the past 40 years not to smile or laugh even at the birth of her only daughter. For her, it’s a way to keep her admittedly, impressive youthful looks.

‘I don’t have wrinkles because I have trained myself to control my facial muscles. I haven’t laughed or smiled since I was a teenager. My dedication has paid off. I don’t have a single line on my face’ says Tess.

Celebrities such as Kim Kardasihan 34 have also admitted to not smiling or laughing because it causes wrinkles.

MBUNGE WA MBEYA MJINI APATA AJARI MILIMA KITONGA IRINGA.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

Afisa Elimu Mbinga avuliwa madaraka.

BARAZA la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma limemvua madaraka afisa elimu msingi wa wilaya hiyo Daniel Mkali baada ya kufanyiwa uchunguzi kwa muda kwa tuhuma mbalimbali zilizotajwa na baadhi ya madiwani pamoja na viongozi wa idara hiyo ya elimu msingi na kuelekea kutishia kuibuka kwa mgogoro wilayani humo.
 
Akitangaza uamuzi huo wa kumvua wadhifa huo pamoja na kumshusha cheo na kutakiwa kupangiwa shule ya kufundisha mwenyekiti wa halmashauri hiyo ya Mbinga Alanus Ngahi, mbele ya madiwani pamoja na watumishi wengine wa halmashauri hiyo amesema uamuzi huo umefikiwa na kamati ya maadili iliyokutana kujadili suala hilo la kinidhamu na kiutumishi na baraza hilo kuridhia hatua zichukuliwe dhidi ya afisa elimu huyo.
 
Akizitaja tuhuma nne zilizokuwa zikimkabili afisa elimu huyo, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga Hussein Isa amesema ni pamoja na kusajili asasi isiyokuwa ya kiserikali iliyojulikana kwa jina la (UWEKAMBI) umoja wa waratibu elimu kata ya Mbinga na kuwaagiza walimu wakuu wa shule za msingi wilayani humo kuhamishia fedha zote za capitation na michango ya Umitashumta jumla ya shilingi milioni 232 ambapo katika fedha hizo shilingi milioni 60 ni michango ya Umitashumta, milioni 10 ni michango ya wazazi na shilingi milioni 61 ni fedha kwa ajili ya capitation na mitihani zilipelekwa kwenye akaunti yenye namba 61714000405 iliyopo katika benki ya NMB tawi la Mbinga.
 
Ameitaja tuhuma nyingine kuwa ni kughushi nyaraka kwa lengo la kutoa fedha kupitia ununuzi wa mafuta ya diesel lita 5500 na petrol lita 5500 na kuwaagiza walimu wakuu wachangie fedha za kupiga picha wanafunzi wa darasa la saba pamoja na fedha kwa ajili ya TSM 9 kwa maelekezo hayo ni kosa kwa sababu alikuwa akijua kuwa gharama za TSM 9 hugharamiwa na serikali kwa asilimia mia moja.
 
Amesema kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi milioni 12.47 zilipelekwa kwenye akaunti hiyo ya UWEKAMBI na ameitaja tuhuma nyingine kuwa ni kumdanganya mwajiri kuwa hakujakusanywa fedha yoyote kutoka kwa wazazi na hakuna fedha ya capitation iliyopelekwa kwenye akaunti hiyo ya UWEKAMBI.
 
Aidha mkurugenzi mtendaji amesema baada ya maamuzi hayo yaliyotolewa na baraza la madiwani hatua nyingine zinazohusishwa na mamlaka nyingine zikiwemo za kinidhamu zitafuata ingawa kwa sasa anapaswa kuyatumikia maamuzi yaliyotolewa na baraza hilo la madiwani.

HATIMAYE JOTI WA ORIGINAL COMEDY AMVISHA PETE MCHUMBA WAAKE WA SIKU NYINGI.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...

HATIMAYE JOTI WA ORIGINAL COMEDY AMVISHA PETE MCHUMBA WAAKE WA SIKU NYINGI.


 Kwa mujibu wa mtandao wa JF, Mwigizaji wa vichekesho Lucas Mhuvile, almaarufu kama Joti, anayepiga kazi kwenye kampuni ya Orijino Komedi, amemvisha pete mpenzi wake wa siku nyingi, ikiwa ni ishara na dalili njema kwamba safari ya kuelekea kwenye taasisi muhimu zaidi duniani ya NDOA imewadia.

Akiwa na swahiba wake wa siku nyingi, Mr. Mjuni Sylvatory a.k.a Mpoki, Joti alionekana mwenye furaha muda wote kwa kutimiza tendo hilo huku akiwa amealika watu wachache sana kuhudhuria tukio hilo.
 Kama ni kweli, tunampongeza sana na kumtakia kila la kheri yeye pamoja na mwenza wake.

Masogange Drops Five New K!lling Photos….Lazima uzione.


UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

habari kamili :: read more...
 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top