Saturday, May 31, 2014

ROSE NDAUKA AJIBU TUHUMA ZA KUPORA WAUME ZA WATU!



Wiki iliyopita katika Exclusive Interview tuliona sehemu ya kwanza ya Rose Ndauka alivyoeleza kuwa aliwamwaga wanaume na kutulia na Maliki. Wawili hao kwa sasa wanaogelea katika penzi zito na mikakati thabiti ya ndoa imeshaanza, wanatarajia kuoana baadaye mwaka huu.

Msanii wa Bongo Muvi, Rose Ndauka.

Leo tunaendelea, atafungukia skendo za kupora waume za watu.
Risasi: Kuna taarifa zilienea kuwa uliwahi kutoka na baba mtoto wa Snura Mushi (mama Majanga), kuna ukweli wowote?

Rose: Nilishawahi kusikia skendo hiyo lakini aliyekuwa anadhania hivyo ni Snura, hakujua tu kama yule alikuwa ni mshkaji wangu na mimi nilimjua Snura walipokuwa kwenye uhusiano.
Risasi: Mbali na huyo, mbona inatajwa kuwa uliwahi kumnyang’anya mwigizaji mwenzio, Yvone Cherry ‘Monalisa’ mpenzi wake? Tena inasemekana mlikuwa marafiki!

Rose Ndauka akiwa na mume wake Maliki.

Rose: Sijawahi kuwa na urafiki na Mona (Monalisa) na huyo aliyezua hayo maneno ni Richard, siyo kweli kwani tuliwasiliana kawaida yeye akapindisha maelezo, shahidi ni baba mtoto wangu aliyeunganishwa na baba mtoto wangu pamoja na marehemu Kanumba (Steven).

Risasi: Umekuwa ukihusishwa na uvutaji wa bangi mara kwa mara, unalizungumziaje hilo?
Rose: Sijawahi kuvuta bangi ila nimewahi kunywa pombe sana hasa nilipokuwa na ‘stress’ na yote niliyokuwa nayafanya mwisho wa siku nilikuwa nikiyajutia.

Risasi: Ni kitu gani kilikufanya ujutie hasa katika suala zima la kugida ulabu?
Rose: Kuna habari imewahi kutoka gazetini nikiwa nabusiana na Maya, iliniumiza sana kwani tulitafsiriwa vibaya kwenye jamii na haitakuja kufutika kwani nilifanya matendo yale kwa sababu ya pombe na toka siku hiyo kiukweli niliacha unywaji wa pombe za vile, nilijuta.

Risasi: Ukipata nafasi ya kuongea na wasichana wasagaji utawaambia nini?
Rose Ndauka: Nitawashauri kuacha kabisa mambo hayo kwani ni ya kuiga tu, wajisomee vitabu vya kila aina ili kujinusuru kwenye tatizo hilo hasa vyenye mafunzo na kuonesha madhara ya usagaji.
Risasi: Tunafahamu kwamba mumeo mtarajiwa umemkuta na mtoto, unamleaje na hujawahi kupata malalamiko kama mama wa kambo?

Rose: Mimi ni kipenzi cha watoto, nampenda na yeye ananipenda, ninapomuona ana kosa namuadhibu kama mwanangu na sitarajii mtu kunisema vibaya kwani malezi ninayompa ni mazuri kama ambavyo namlea wa kwangu.
habari kamili :: read more...

JOHARI AMTUPIA CHUCHU VIJEMBE MSIBANI.


STAA wa Bongowood, Blandina Chagula ‘Johari’ anadaiwa kumtupia vijembe kiaina msanii mwenzake, Chuchu Hans ambaye ‘anabanjuka kimalovee’ na mkurugenzi mwenza wa Kampuni ya RJ, Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’.

Staa wa Bongowood, Blandina Chagula ‘Johari’.

Tukio hilo lilichukua nafasi kwenye msiba wa mwigizaji Sheila Haule ‘Recho’ Sinza-Palestina, Dar, hivi karibuni ambapo vijembe viliibuka baada Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ kumuuliza kwa lugha ya utani Chuchu kuwa RJ itachangia nini msibani hapo, Johari akadakia:

“Kampuni yangu si ya uchochoroni au ya chumbani, nina TIN namba kabisa siyo kama hiyo nyingine, iweje umuulize asiyehusika...”

Baada ya Johari kutamka maneno hayo, waombolezaji waliokuwepo msibani hapo walipigwa na butwaa na kuhoji kulikoni?

Johari amekuwa akidaiwa kuwa na uhusiano na Ray kipindi cha nyuma huku kukiwa na taarifa kuwa Chuchu ana kampuni iitwayo Chura ikimaanisha Chuchu na Ray hivyo ilitafsiriwa kuwa alikuwa akiipiga kijembe kwa madai kuwa haiwezi kufikia levo za RJ.

Alipofuatwa na mwanahabari wetu ili kupata ufafanuzi juu ya ishu hiyo, Johari hakuwa tayari kwani alisema ana majonzi ya kuondokewa na kipenzi chake Recho hivyo hakutaka malumbano na watu katika kipindi hiki kigumu.
habari kamili :: read more...

Kijana anayedaiwa kuwa Msukule aonekana nje ya nyumba ya Kikongwe aliyeuawa kwa imani hizo.

Kijana Ndaki Samola akiwa amepandishwa ndani ya gari la polisi kwa ajili ya kupelekwa kwa wataalamu ili kufanyiwa uchunguzi kama ana matatizo ya akili.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mamia ya wananchi wa kijiji cha Ilebelebe kata ya Itilima wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wamefurika kushuhudia tukio la kijana mmoja anayesadikiwa kuwa ni msukule aliyeibuka siku moja baada ya kikongwe kuuawa kwa kucharangwa mapanga kwa imani za kishrikina kijijini hapo.

Kijana huyo aliyedai kuwa anaitwa Ndaki Samola alionekana jirani na nyumba ya mwanamke Nyanzala Basu (65-70) aliyeuawa Mei 26 mwaka huu,saa moja na nusu usiku baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana kisha kumcharanga mapanga akiwa nyumbani kwake kisha kutokomea kusikojulikana.
Imeelezwa kuwa siku ya mazishi ya Kikongwe huyo Mei 27 mwaka huu ndipo kijana huyo anayedaiwa kuhifadhiwa na kikongwe huyo alikutwa na wananchi nyuma ya nyumba ya kikongwe huyo saa tatu usiku akizunguka na kusikika akisema kaamua kutoka nje baada ya kukosa chakula.
Walioshuhudia tukio hilo walisema Kijana Ndaki Samola anayedaiwa kuwa ni msukule akizungumza kwa shida alisema anatoka kijiji cha Bubale kata ya Samuye wilaya ya Shinyanga na alifika kijijini hapo kwa ajili ya kuoa.
Kijana huyo akizungumza bila ya kufafanua ni kipindi gani amekaa katika kijiji hicho alidai alikuwa akiishi kwenye nyumba ya bati ya kikongwe huyo na wenzake wawili na kwamba kutokana na njaa yake ndiyo kaamua kutoka.

Mwenyekitiwa kijiji cha Ilebelebe Thomas Nkindo alisema tukio hilo limewashangaza kwani kijana huyo hajawahi kuonekana kijijini hapo hata siku moja ,hali ambayo imewapa wasiwasi wananchi kutokana na maneno aliyoeleza kwamba alikuwa kwenye nyumba ya kikongwe huyo ambayo ilikuwa imefungwa kwa muda mrefu na haitumiki.

“Baada ya kuhojiwa na jeshi la jadi sungusungu kijana, alidai kilichomtoa ndani ni njaa na kawaacha wenzake wawili mmoja akiwa ni mwanamke,na alikuja kwa ajili ya kuoa na kufikishiwa kwenye nyumba hiyo ya tope ambayo imeezekwa kwa bati iliyokuwa ikimilikiwa na marehemu”,alieeleza Nkindo.
Akifafanua zaidi kuhusu tukio hilo afisa mtendaji wa kijiji cha Ilebelebe Emmanuel Asili alisema marehemu Nyanzala Basu kabla ya kufikwa na mauti siku hiyo ya tukio asubuhi alikuwa amealika wanawake, ambao walifanya kazi ya kumsaidia kukata viazi maarufu kama michembe ndipo usiku huo huo alivamiwa na kuuawa majira ya saa 1.30 wakati akimpatia mbwa wake chakula.

“Kilichotushtua zaidi huyo kijana Ndaki alikuwa ananukia harufu ya nyama wakati tunamuona na ukizingatia mchana kwenye mji huo ulipokuwa msiba walikuwa wamechinja mbuzi,moja kwa moja wananchi walimtilia mashaka inawezekana akawa ni msukule kwa kulinganisha na maelezo yake “alisema Asili.

“Kutokana na mashaka hayo tulitoa taarifa kwa jeshi la polisi huku tukimhifadhi kijana kwa muda katika ofisi yangu uangalizi zaidi na polisi walipofika walizungumza na wananchi na kuamuru mlango wa nyumba hiyo uvunjwe ili kuona kilichomo ndani wakakuta beseni,ndoo na bati lililochakaa”,alieeleza afisa mtendaji wa kijiji.

Akizungumza na wananchi mkuu wa kituo cha polisi wilaya ya Kishapu ASP Samwel Kijenga aliwataka kutoa ushirikiano ili kuwabaini watu waliosababisha mauaji hayo ya kinyama huku akiwataka kuondoa wasiwasi kuhusu nyumba waliyokuwa wakihofia kwani wameangalia hawajaona kitu hivyo waendelee na shughuli za maendeleo.

Hata hivyo wakati kijana huyo akiwa tayari amepandishwa ndani ya gari la polisi kwa ajili ya kupelekwa kufanyiwa uchunguzi kama ana matatizo ya akili,alitokea mwanamme aliyejitambulisha kwa jina la Nyalali Chaba mkazi wa kijiji cha Ikoma wilayani Kishapu na kudai kuwa anamfahamu ni mdogo wake anasumbuliwa na tatizo la akili ndipo polisi wakamkabidhi kwa maandishi.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga SACP Evarist Mangalla amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la mauaji ya kikongwe na tayari watu wanne wanashikiliwa kwa ajili ya mahojiano zaidi wakati wakiendelea na upelelezi
habari kamili :: read more...

Breaking!! GEORGE TYSON WA BONGO MOVIE AFARIKI DUNIA.

 George Tyson enzi za uhai wake.

George Tyson akimlisha keki Yvonney Chery ‘Monalisa’ wakati mtoto wao Sonia alipopata kipaimara.

Marehemu Tyson akiwa na Monalisa (kushoto), kulia ni Tyson na mwanae Sonia.

NI pigo tena kwa tasnia ya Bongo Muvi, mwongozi filamu Bongo na aliyekuwa mume wa staa wa filamu Bongo, Yvonny Cherry 'Monalisa', George Tyson amefariki dunia baada ya kupata ajali mbaya ya gari eneo la Morogoro akitokea mkoani Dodoma. Tyson alikuwa ameambatana na watu kadhaa katika safari hiyo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Monalisa amemlilia Tyson kwa kuandika yafuatayo:


MUNGU AIPUMZISHE ROHO YA MPENDWA WETU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!
habari kamili :: read more...

Friday, May 30, 2014

Habari ya kusikitisha; Mwanafunzi wa Chuo kikuu UDSM akutwa Hosteli kitandani amekufa.



TUTAKUPA TAARIFA KAMILI NA ZAIDI HIVI PUNDE.
habari kamili :: read more...

Arsene Wenger ametia saini mkataba wa kuendelea kuinoa Arsenal hadi mwaka 2017.

Arsene Wenger ametia saini mkataba wa miaka miwili kama meneja wa klabu hiyo hadi mwaka 2017.

Wenger, 64, ameongoza Arsenal na kufanikisha ushindi wa mataji 8 tangu kujiunga na klabu hiyo Septemba mwaka 1996.Msimu huu aliweza kuongoza timu hiyo hadi kufuzu kwa mara ya 17 kwa kombe la klabu bingwa ulaya na kupata ushindi aliosubiri kwa hamu kwa miaka tisa dhidi ya Hull City katika fainali ya kombe la FA Cup.

Wenger alikuwa anafika ukingoni mwa mkataba wake mwaka huu

Arsenal ilikuwa haijawahi kushinda taji la nyumbani tangu mwaka 2005 ingawa walifika fainali ya kombe la mabingwa wa Ulaya mwaka 2006.Wenger, ambaye sasa ni meneja mkongwe zaidi katika ligi ya Ulaya baada ya Sir Alex Ferguson kustaafu, mwezi Mei mwaka 2013, anasifika kwa kuleta mawazo mapya kuhusu michezo na lishe bora katika soka Uingereza.

''Huyu ndiye mtu anayefanya kazi mwa saa 24 kila siku,'' alisema mlinda lango wa zamani wa Arsenal Bob Wilson.

"anachukia sana kushindwa. Alileta mageuzi makubwa, katika kila sekta ya mchezo huo nchini Uingereza. Watu wanadhani kuwa ana mamlaka sana lakini mtu ambaye anajitolea sana kwa mchezo huu ni mtu anayethaminiwa sana.''

Ushindi mkubwa wa Wenger ulikuwa wakati ambapo alishinda kombe la ligi ya Premier kati ya mwaka 2003-04 alipokuwa na wachezaji kama vile Thierry Henry na Patrick Vieira.

Wenger alimsajili Mesut Ozil kwa kima cha dola milioni 42.4 kwa msimu ambao umekamilika.

Lakini licha ya hali ya suitofahamu kuhusu mustakabali wa Wenger mwezi Januari, mkurugenzi mkuu wa Arsenal, Ivan Gazidis, alitabiri kuwa Wenger huenda akaongezewa muda Arsenal.
habari kamili :: read more...

AGNES MASOGANGE AVISHWA PETE YA UCHUMBA YA MIL.16 BAADA YA KUDUNGWA MIMBA AFRIKA KUSINI.


Habari mpya ni kuwa Agnes Masogange ambaye ni video queen maarufu nchini amevishwa pete ya uchumba yenye thamani ya shilingi mil.16 za kitanzania. 

Habari zaidi zinadai kuwa Masogange kwasasa ni mjamzito na alipoenda Afrka  Kusini hivi juzi kati kumuambia jamaa aliyempa mimba kuwa ana ujauzito wake Jamaa huyo alifurahi sana na kumvisha Masongange pete inayoonekana pichani ambayo Agnes mwenyewe aliweka picha hiyo katika mtandao mmoja wa kijamii na kuandika maneno yasemayo "mama kijacho".
habari kamili :: read more...

Mchawi mtanzania jela miaka 3 nchinin Kenya.

Mchawi kutoka Tanzania amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu nchini Kenya kwa kumlaghai mwanamke mfanyabiashara mkenya na kumuibia shilingi milioni tisa.

Mchawi huyo alimhadaa mama huyo kuwa kwa kupitia njia za kichawi angeweza kuzifanya pesa hizo kuwa maradufu yaani milioni 18. Bwana Amos Chipeta pia ataongezwa kifungo cha miezi tatu kwa kupatikana na vifaa vinavyoumiwa kufanya uchawi kama vile chupa, visu na ngozi ya Paka.

Kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation, Chipeta alihukumiwa pamoja na mwenzake bwana Peter Christopher aliyepatikana na hirizi zinazotumika kufanyia uchawi.

Bwana Chipeta alimlaghai Bi Catherine Njeri hela zake tarehe tofauti tofauti kati ya mwezi wa Agosti na Decemba 2012 baada ya mwanamke huyo kuwaendea na kumwomba wazifanye pesa hizo ziwe maradufu

Walijitetea kwa kusema kuwa mwanamke huyo aliwaendea ili wampe nguvu za kichawi aweze kuwashinda wapinzani wake wa kisiasa

Maafisa wa polisi walipata hirizi hizo na vifaa walivyotumia kwa uchawi mwezi Februari 1, 2014 katika nyumba ya kukodisha iliyo kando ya barabara ya Juja viungani mwa mji mkuu Nairobi.

Hakimu aliyesikiliza kesi hiyo alisema kuwa wanaume hao waliona mwanamke huyo kuwa mjinga na basi kumnafiki kwa urahisi na kuwa hawana majuto au toba.
habari kamili :: read more...

Italy yathibitisha kuwa umri wa Minala ni miaka 17 sio 42.

 
Uchunguzi wa shirikisho la soka la Italia umebaini kuwa mchezaji tineja wa Cameroun Joseph Minala ana umri wa miaka 17 wala sio 42 kama ilivyodhaniwa na kuripotiwa katika vyombo vya habari.
Mnamo mwezi Februari mtandao mmoja wa michezo barani Afrika ulichapisha habari ambayo ilizua dukuduku iwapo kiungo huyo alikuwa amedanganya umri wake .
Mtandao huo ulichapisha habari za kuashiria kuwa hakuwa tineja bali mtu mwenye umri wa miaka 42.
Uchunguzi uliofwatia ulimlazimu kukatiza kwa muda mipango yake ya kucheza soka ya kulipwa hadi pale matokeo ya uchunguzi yangewekwa wazi na maafisa wa shirikisho la soka la Italia.
Minala alijiunga na klabu hiyo yenye makao yake mjini Rome na hata alishiriki mchuano wa vijana wasiozidi umri wa miaka 23 wa Viareggio mnamo mwezi wa Februari.
habari kamili :: read more...

Mume amshtaki mkewe kwa kumnyima ngono.

Majaji waliamua kuwa mkewe Mason hakufanya kosa lolote
Kuna kisa kimeibuka nchini Uingereza ambapo mwanamume mmoja kwa jina David Mason, mwenye umri wa miaka 30, alimshitaki mkewe Brenda kwa kumnyima haki yake ya kingono au kukataa kushiriki tendo la ndoa.

Mwanamke huyo alimfanyia mgao wa wiki moja kila mwezi wa kitendo cha ndoa mumewe kwa hofu ya kushika mimba kwa mara ya tatu.

Kwa mujibu wa jarida la mtandao la Mirror, la Uingereza, Bwana Mason, ambaye kazi yake ni fundi mitambo alishinda kesi hiyo mwaka 1980.

Lakini mkewe alikataa rufaa ambapo Mason alipoteza kesi hiyo baada ya majaji kusema kuwa mahakama isingeweza kuamua kuwa mkewe Mason alimkosea.

Nini maoni yako kuhusu tukio hili?

Chanzo: http://www.bbc.co.uk/swahili
habari kamili :: read more...

Majibu ya Zitto Kabwe juu ya madai ya kambi ya upinzani kuhusu Lekadutigite na Gombe Advisors haya hapa.

Kwenye Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ya Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo aliyoiwasilisha Bungeni leo hii muda mfupi uliopita. Waziri Kivuli Joseph Mbilinyi  ‘Sugu’ alimtaja Zitto Z. Kabwe kama Mmiliki wa Kampuni ya Leka Dutigite aliyofanya biashara isivyo halali na Mashirika ya Umma ya NSSF na TANAPA.

Hivi ndivyo ilivyokuwa sehemu ya hotuba hiyo.

Mheshimiwa Spika, Tarehe 13 Agosti, 2012, Msajili Msaidizi wa Makampuni katika Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) alitoa Hati ya Usajili (Certificate iof Incorporation) kwa kampuni inayoitwa Leka Dutigite Limited. Kwa mujibu wa nyaraka za BRELA, Leka Dutigite Ltd. ina ofisi zake katika ghorofa ya kwanza ya jengo la City House lililoko katika Mtaa wa Mkwepu, Dar es SalaaM.

Mheshimiwa Spika,Katiba yaani Memorandum and Articles of Association, ya kampuni ya Leka Dutigite Ltd. iliyosajiliwa BRELA tarehe 13 Agosti, 2012 inaonyesha kwamba mwenye hisa nyingi katika kampuni hiyo ni kampuni nyingine inayoitwa Gombe Advisors Ltd. ya Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za kibenki ambazo Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu imezipata, mnamo tarehe 10 Desemba, 2012, Hifadhi ya Taifa ya Saadani ilihamisha jumla ya shilingi 12,200,000 kwenda kwenye akaunti na. 0150357447800 iliyoko CRDB Bank tawi la Pugu Road, Dar es Salaam, inayomilikiwa na Leka Dutigite Ltd. Hifadhi ya Taifa ya Saadani inamilikiwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), ambayo ni shirika la umma. Siku moja baadae, fedha hizo zilitolewa kwa pesa taslimu kutoka kwenye akaunti hiyo.

Baada ya hapo, kati ya tarehe 14 Januari na 7 Februari, 2013, akaunti ya Leka Dutigite Ltd. iliingiziwa jumla ya shilingi 28,600,000. Fedha hizi zote ziliingizwa kama fedha taslimu na mtu aitwaye Mchange (shilingi 3,600,000 tarehe 14 Januari, 2013) na Leka Dutigite (shilingi 25,000,000 tarehe 23 Januari na 7 Februari, 2013). Kufikia tarehe 7 Februari, 2013, fedha hizo zote zilikwishatolewa benki.

Mheshimiwa Spika, Tarehe 28 Februari, 2013, akaunti ya Leka Dutigite Ltd. iliingiziwa shilingi 32,367,000 na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Kwa mujibu wa taarifa za kibenki, siku hiyo hiyo, fedha hizo zilitolewa kwenye akaunti hiyo. Siku nne baadae, yaani tarehe 4 Machi, 2013, NSSF ilifanya malipo mengine kwenye akaunti ya Leka Dutigite Ltd., kwa mikupuo miwili, ya jumla ya shilingi 46,663,000. Siku hiyo hiyo, fedha hizo nazo zilitolewa kutoka kwenye akaunti hiyo kwa mikupuo miwili. Kwa hiyo, katika kipindi cha miezi mitatu katika ya tarehe 10 Desemba, 2012 na 4 Machi, 2013, Leka Dutigite Ltd. ililipwa shilingi 119,930,000 kwa utaratibu huo huo wa ingiza na toa fasta. Kati ya fedha hizo, shilingi 12,200,000 zililipwa na TANAPA na shilingi 79,027,000 zililipwa na NSSF.

Mheshimiwa Spika, Katika mazingira ya kawaida, sio kitu cha ajabu kwa mashirika ya umma kama NSSF na TANAPA kufanya biashara na watu au taasisi mbali mbali kama makampuni binafsi. Ukweli ni kwamba, kwa upande wa malipo yaliyofanywa na TANAPA, Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu imeweza kupata nakala ya mkataba unaohusu Maandalizi ya Filamu (Documentary) kwa Ajili ya Kuhamasisha Shughuli za Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Saadani kwa Kutumia Wasanii Kutoka Kigoma. Mkataba huo umesainiwa tarehe 5 Desemba, 2012, kati ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani na Leka Dutigite Ltd. na una thamani ya shilingi 12,200,000, kiasi kile kile kilicholipwa na Hifadhi hiyo.

Hata hivyo, Mheshimiwa Spika, mazingira ya malipo haya sio ya kawaida. Hii ni kwa sababu ya uwepo wa kampuni ya Gombe Advisors Ltd. Kwa mujibu wa nyaraka za BRELA, kampuni hii ilisajiliwa tarehe 24 Novemba, 2011. Kwa mujibu wa nyaraka hizo, ofisi za Gombe Advisors Ltd. ziko kwenye jengo la City House, Mtaa wa Mkwepu, Dar es Salaam, ziliko ofisi za Leka Dutigite Ltd. Kwa mujibu wa nyaraka hizo, wakurugenzi wa Gombe Advisors Ltd. ni Zitto Zuberi Kabwe ambaye kazi yake inatajwa kuwa ‘mchumi’, na Raphael Ongangi ambaye anatajwa kuwa ‘mchambuzi wa fedha na vitega uchumi’ (Financial and Investment Analyst). Bwana Ongangi aliwahi kutajwa na gazeti la kila wiki la —– la tarehe 26 Desemba 2013 kuwa ni mmoja wa washauri wa Zitto Zuberi Kabwe na anasemekana kuwa msaidizi wake.

Mheshimiwa Spika, Zitto Zuberi Kabwe sio ‘mchumi’ anayetajwa katika nyaraka za BRELA zinazoihusu kampuni ya Gombe Advisors Ltd. pekee, bali pia ni Mbunge, tangu mwaka 2005, wa Bunge lako tukufu. Kama Mbunge, Mheshimiwa Zitto Kabwe ni ‘kiongozi wa umma’ kwa mujibu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, 1995. Sheria hii inawalazimu viongozi wa umma, wanapokuwa madarakani, kuwa “waadilifu, wenye huruma, utulivu, umakini na watakaoendeleza viwango vya juu vya maadili ili kujenga na kuendeleza imani ya umma kwa uadilifu wa Serikali.”

Aidha, viongozi wa umma “… watawajibika kutekeleza wajibu wao kwa umma na kuendesha shughuli zao binafsi kwa namna ambayo itaonekana na kuthibitika kuwa ni wazi kwa umma na haitatosheleza kwao kutekeleza wajibu wao kwa kufuata sheria tu.” Vile vile, kuhusiana na maslahi binafsi, Sheria hii inaelekeza kwamba “… viongozi wa umma hawatakuwa na maslahi binafsi ambayo yanaweza kuathiriwa na maamuzi ya serikali wanayoshiriki katika kuyafanya.

Mwisho,kuhusiana na maslahi ya umma, viongozi wa umma wanatakiwa, pale wanapochaguliwa au kuteuliwa, kupanga masuala yao “kwa namna itakayozuia migongano ya maslahi ya wazi, iliyojificha au inayoonekana kuwepo na pale ambapo migongano hiyo inatokea kati ya maslahi binafsi na maslahi ya umma basi itatatuliwa kwa kuangalia zaidi maslahi ya umma.” Kwa kadri ya ufahamu wa Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu, Mheshimiwa Zitto Kabwe hajawahi kutangaza maslahi aliyonayo kwenye mikataba ya Gombe Advisors Ltd. na Leka Dutigite Ltd. na NSSF na TANAPA.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe sio tu ni Mbunge anayebanwa na masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, bali pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha za Serikali (PAC). Kwa mujibu wa kipengele cha 12 cha Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Kudumu za Bunge lako tukufu, mojawapo ya majukumu ya PAC ni kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za umma katika Wizara na Mashirika ya Umma yaliyoainishwa katika taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. NSSF na TANAPA ni baadhi tu ya Mashirika ya Umma yaliyo chini ya usimamizi wa kibunge wa PAC.

Kwa maana hiyo, Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Zitto Kabwe, kwa kutumia makampuni yake ya Leka Dutigite Ltd. na Gombe Advisors Ltd., amefanya biashara na TANAPA, shirika la umma analolisimamia kama Mbunge na Mwenyekiti wa PAC. Mheshimiwa Zitto Kabwe na wanamuziki washirika wake, kwa kutumia makampuni ya Gombe Advisors Ltd. na Leka Dutigite Ltd., wamelipwa fedha za umma za TANAPA na NSSF.

Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kutoa maelezo juu ya madai ya ukiukwaji wa Sheria uliofanywa na viongozi wa umma na mashirika ya umma katika kashfa hii. Pamoja na maelezo yatayotolewa , Kambi Rasmi ya Upinzani inataka Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalum juu ya matumizi ya fedha zilizotolewa na TANAPA na NSSF; msukumo uliofanya fedha hizo zitolewe na matumizi ya fedha hizo kwa kuzingatia masharti yanayosimamia fedha za umma na utawala bora katika usimamizi wa fedha za umma. Aidha, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ifanye uchunguzi juu ya malipo na matumizi husika kwa kurejea masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Sheria nyingine zinazohusika. Kwa upande mwingine, kwa kuwa suala hili linahusu mbunge na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayohusika na usimamizi wa fedha za umma, Kamati ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge nayo ifanye uchunguzi wake juu ya madai ya masharti ya Katiba ya Nchi, Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na Kanuni za Bunge juu ya maadili ya kiongozi wa umma ikiwemo yahusuyo utangazaji wa maslahi.

Mheshimiwa Spika; Mwisho, Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu inatoa rai kwa wanamuziki na wasanii wengine wote nchini kuwa waangalifu na watu wanaotaka kutumia umaarufu wao kama wanamuziki na wasanii kwa lengo la kufanikisha dili za kifisadi. Bila kuchukua tahadhari ya kutosha, wasanii hao wanaweza kujikuta wakipoteza sifa na umaarufu wao ambao wameujenga kwa jitihada zao wenyewe.

Zitto Kabwe kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii amepost ujumbe huu usiku wa Mei 29 ambao unaonyesha kuwa na majibu juu ya maswali yaliyoulizwa na kambi ya upinzani juu ya umiliki wa Lekadutigite na Gombe Advisors,Hii ndiyo status yake.

Maelezo yangu kuhusu kazi za Kigoma AllStars/LEKADUTIGITE kwa NSSF na TANAPA.

Leo tarehe 29 Mei, 2014 Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Habari, Michezo, Vijana na Utamaduni amenituhumu kuhusika na kinachoitwa ufisadi katika Shirika la TANAPA na NSSF.

Nasikitika kwamba katika hali niliyonayo ya kumwuguza mama yangu naingizwa kwenye siasa za majitaka. Kwa sasa nitatoa maelezo kwa ufupi ili kuondoa upotoshaji.

Kampuni ya LekaDutigite inamilikiwa na wasanii 15 ambapo kila mmoja ana hisa 5% ambazo niliwalipia ili waweze kushirikiana katika kazi zao. Hisa 25% zilizobakia zinamilikiwa na kampuni ya Gombe Advisors ambayo ni kampuni isiyofanya faida (Company limited by guarantee) na haina maslahi yeyote ya kibiashara (not for profit company). Hivyo Mimi binafsi sina maslahi yeyote ya kifedha zaidi ya kuwasaidia wasanii hawa katika kazi zao mbalimbali.

Wasanii wa Kigoma AllStars wamefanya kazi na TANAPA na NSSF, kazi ambazo zinajulikana na zipo. Kwa upande wa TANAPA wasanii hawa waliandaa kazi ya kuitangaza Hifadhi ya Saadani na walilipwa. Kwa upande wa NSSF wasanii hao walitunga wimbo na video yake na wimbo huo unatumika katika Shirika hilo.
Vile vile walifanya matamasha mbalimbali ya kuhamasisha watu kujiunga na NSSF. Wasanii wa Kigoma All Stars wote ni wanachama wa Mfuko huo.

Katika kazi zote hizi Mimi binafsi sijafaidika kwa namna yeyote ile kifedha. Kauli yeyote ya kujaribu kuonyesha kazi hizi za wasanii ni ufisadi ni kauli za kusikitisha na kukatisha tamaa kwa mtu ambaye anajaribu kusaidia wasanii kufaidika na kazi zao za sanaa.

Katika kazi zote hizi Mimi binafsi sijafaidika kwa namna yeyote ile kifedha. Kauli yeyote ya kujaribu kuonyesha kazi hizi za wasanii ni ufisadi ni kauli za kusikitisha na kukatisha tamaa kwa mtu ambaye anajaribu kusaidia wasanii kufaidika na kazi zao za sanaa.

Toka mwaka 2012 nilipoanza kujitokeza kusemea wasanii watu kadhaa wenye maslahi na tasnia hii wamekuwa wakinikatisha tamaa na hata wengine kuona nimewaingilia kazi zao.
Hivi sasa wasanii wa Kigoma AllStars ni wanahisa katika kampuni ya PERA Africa limited ili kufaidika na biashara ya miito ya simu. Yote haya nilifanya kwa uchungu nilionao kwa vijana wetu na sio kwa kutaka kufaidika kifedha. Nimeumizwa sana na tuhuma hizi za kuokoteza okoteza.

Inaniumiza zaidi kutokana na ukweli kwamba ninamwuguza mama yangu mzazi, kipindi ninachohitaji kutiwa moyo na kuombewa hata na maadui zangu kisiasa. Kipindi ambacho mama yangu yupo mahututi, tena mjumbe wa kamati kuu ya chama ambacho watoa tuhuma wanatoka, pole ninayopewa ndio hiyo. Hakuna namna ya kukosa ubinaadamu zaidi ya hivi.

Najua wajibu wangu ni kusimamia Mashirika ya Umma na nikiwa mpigania uwajibikaji nipo makini sana kuhakikisha sina mgongano wa maslahi katika mambo yangu. Ndio maana sina biashara yeyote ile ili kuhakikisha natimiza wajibu wangu kwa uadilifu mkubwa. Napata ‘moral authority’ ya kutaka uwajibikaji kwa sababu nafanya kazi zangu kwa misingi hiyo ‘at arms length’.

Hivyo ninataka mara moja CAG afanye ukaguzi wa kazi za wasanii hao kwenye NSSF na TANAPA. Pia achunguze kama Gombe Advisors ( company limited by guarantee) ina maslahi yeyote ya kifedha katika kazi hizo za wasanii. Nataka pia Shirika la NSSF na TANAPA waweke wazi mchakato wa kazi zao na wasanii hawa kupitia LEKADUTIGITE Limited.

Zitto Kabwe
Mei 29, 2014
Dar Es Salaam.
habari kamili :: read more...

Wasichana watatu wabakwa na kuning'inizwa kwenye mt huko India.

Takribani wanaume watatu akiwemo afisa mmoja wa polisi tayari wamekamatwa kuhusiana na tukio la kubakwa kwa wasichana wawili wadogo na kundi la watu na kuning’inizwa juu ya mti huko nchini India.

Mamlaka katika Jimbo la Utter Pradesh limesema kuwa bado linamsaka mtu mmoja ambaye anatuhumiwa kuwepo katika kundi hilo lililohusika kufanya tukio hilo la kusikitisha.

Familia za wahanga wa tukio hilo zimesema kuwa mara ya kwanza polisi walikataa kuwasaidia katika kuwatafuta watoto hao baada ya kupotea ambapo matukio ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake nchini India bado yameendelea kuwa tatizo kubwa.

Wanakijiji walikuta miili ya wasichaa hao wenye umri wa miaka 14 na 15 ikiwa inaning’inia juu ya mti wa maembe saa chache baada ya kupotea nyumbani katika kijiji cha Katra kilichopo kwenye jimbo la Utter Pradesh.
Wasichana hao walikuwa wamekwenda vichakani kuoga kutokana na kutokuwa na vyoo nyumbani kwao ambapo mamia ya wanakijiji wenye hasira walikusanyika katika eneo hilo la mti kwa siku nzima wakiandamana kushinikiza polisi kukabiliana na vitendo hivyo.
habari kamili :: read more...

Vazi la lulu akitembea huku akiwa ameachia mtindi out hizi hapa.

 MSANII wa filamu Bongo, Elizaberth Michael ‘Lulu’ hivi karibuni aliwashangaza watu baada ya kuvukwa na gauni alilokuwa amevaa na kulazimika kutembea huku sehemu kubwa ya kifua chake ikiwa wazi.

Msanii wa filamu Bongo, Elizaberth Michael ‘Lulu’.

Tukio hilo lilitokea hivi karibuni katika kiwanja kimoja kichopo mjini Arusha ambapo mmoja wa watu aliyemtia machoni Lulu aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema:

“Yaani nilimuona Arusha akiwa amevaa gauni lililoacha wazi matiti yake, kaficha chuchu tu na inavyoonekana gauni lilimvuka, akaonekana akihangaika kulirudishia bila mafanikio.”

Ijumaa lilimtafuta Lulu kupitia simu yake ya mkononi bila mafanikio ila juzikati akatundika picha kwenye mtandao wa instagram akiwa amevaa gauni kama lile aliloonekana nalo Arusha.
habari kamili :: read more...

Thursday, May 29, 2014

HUYU NDIE MREMBO ALIYENASWA AMETINGA NGUO ZA MAREHEMU KUAMBIANA.

Takribani siku kumi tangu alipofariki dunia aliyekuwa ‘kichwa’ kwenye filamu za Kibongo, Adam Phillip Kuambiana (38), mrembo aliyejitambulisha kwa jina Mary Njombe amenaswa na nguo za staa huyo wakati mali za marehemu hazijagawanywa.Mary Njombe aliyenaswa akiwa amevaa nguo za marehemu Adam Phillip Kuambiana.
 Kwa mujibu wa vyanzo vyetu makini, Mary ambaye ni mkazi wa Magomeni Hospitali, Dar amekuwa akipigilia pamba za marehemu hasa baada ya jamaa huyo kutangulia mbele ya haki.“Jamani njooni huku Magomeni Hospitali hapa mtaa wa pili kuna mwanamke anatinga nguo za marehemu Kuambiana,” kilisema chanzo chetu.

Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu walifanya msako eneo hilo hadi wakamnasa Mary.

Katika mahojiano na gazeti hili, Mary alisema kuwa alikuwa mchumba wa Kuambiana na alichobahatika kubaki nacho ni nguo ambazo alimpatia mara ya mwisho amfulie (zinaonekana pichani).Mary alisema kuwa yeye na Kuambiana walifahamiana tangu mwaka 2006 ambapo alikuwa akimbembeleza kuwa naye.“Mwaka 2008 ndiyo tulianza rasmi uhusiano kwani mimi nilikuwa sina mwanaume na yeye hakuwa na mtu hivyo tulikubaliana na alikuwa akijulikana nyumbani kwetu,” alifunguka Mary.

Mwanadada huyo alisema kuwa yeye na Kuambiana walikuwa wakikutana kwenye Hoteli ya Grand iliyopo Magomeni, Dar na mara nyingi alikuwa akimpikia chakula na kumpelekea ‘lokesheni’.

“Nimeumia sana na sijielewi, Kuambiana ameniachia donda kubwa, nakumbuka neno la mwisho aliniambia nimpende sana kwani ipo siku nitamkubuka,” alisema Mary huku akiangua kilio.


Alipoulizwa kama kweli nguo hizo ni za marehemu Kuambiana, alizama ndani akatoka akiwa amevaa pensi na shati la ‘drafti’ alilokuwa anapendelea kulivaa staa huyo ambalo ni maarufu sana.
Kuambiana alifariki dunia usiku wa kuamkia Mei 17, mwaka huu baada ya kuanguka chooni kutokana na kusumbuliwa vidinda vya tumbo.

Adam Phillip Kuambiana enzi za uhai wake akiwa amevaa shati alilonaswa nalo mrembo.
habari kamili :: read more...

AIBU YA MWAKA, ANGALIA ALICHOKIFANYA BWANA HARUSI HUYU BAADA YA KUINGIA UKUMBINI.

Kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firahuni ndo kama hiiiii.
habari kamili :: read more...

Huyu ndie jamaa aliyekodi Ngoma wakati wa TUKIO la KUMFUMANIA MKE wake!

AMA kweli dunia ina mambo na mambo yenyewe ndiyo haya! Katika hali ya kushangaza, mwanaume aliyefahamika kwa jina la Ramadhan Ally, mkazi wa Kata ya Mbuyuni Manispaa ya Morogoro amewashangaza wengi kufuatia uamuzi wake wa kukodi ngoma ya asili kwa lengo la kwenda kumfumania mkewe aliyejulikana kwa jina moja la Asha.

Mwanadada aliyetambulika kwa jina la Asha baada ya kufumaniwa akisindikizwa na ngoma.

Tukio hilo lililofunga mtaa lilijiri asubuhi ya saa 3:14  Jumatatu iliyopita eneo maarufu kwa jina la Sultani baada ya mwanaume huyo kutonywa kuwa, mke wake alikuwa amelala kwa rafiki yake kipenzi, Abdallah Elias.

Baadhi ya wananchi waliobahatika kuwasili katika eneo la tukio walishuhudia mwenye mali akiwashushia kichapo kikali ‘wasaliti’ hao ambapo vurugu zikapamba moto.

Kufuatia hali hiyo, viongozi wa serikali ya mtaa huo waliamua kutoa taarifa kwa Kamanda Mkuu wa Ulinzi wa Jadi Kata ya Mbuyuni, Aidan Mtimbo ambaye alifika eneo la tukio na vijana wake na kuwasomba watuhumiwa hao msobemsobe huku wakisindikizwa na ngoma hiyo hadi Kituo cha Polisi Kata ya Mbuyuni.

Vijana wakipiga ngoma wakati wa fumanizi la Asha.

Katika hali ya kushangza, nje ya kituo hicho cha polisi baadhi ya wananchi waliokuwa na hasira walishinikiza watuhumiwa watolewe nje wawafanyie kitumbaya huku baadhi yao wakikipopoa mawe kituo hicho kilichokuwa na askari mmoja aliyevaa nguo za kiraia.

Baada ya vurugu hizo, afande huyo alipiga simu kituo kikuu cha polisi kuomba msaada ambapo askari wa pikipiki walifika na kuwakodia teksi watuhumiwa hadi kituoni.

Mwandishi wetu alifanikiwa kuwahoji wahusika wote watatu ambapo mume wa mwanamke huyo ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzungumza kama ifuatavyo:

“Huyu mwanamke ni malaya sana, kwanza  nimemtoa kwao Matombo (Morogoro) akiwa na watoto wawili na kila mmoja na baba yake.

“Mimi sikujali hilo, ukipenda bonga penda na ua lake. Miezi mitatu iliyopita aliniambia ana ujauzito wangu, taarifa hizo zilinifurahisha sana. Cha ajabu juzi akaniambia ametoa mimba yangu, nilipomuuliza kwa nini, akasema kwa ujeuri eti hayupo tayari kuzaa na mimi kwa sasa.

“Nilichukua uamuzi wa kumrudisha kwao, jana usiku napokea taarifa kuwa yuko nyumbani kwa rafiki yangu kipenzi, Abdallah Elias.

Polisi baada ya kutinga eneo la tukio kuwanusuru watuhumiwa.

“Ndiyo asubuhi nikakodi ngoma na kwenda, niliwakuta wamelala kitandani.”
Kwa upande wake Elias alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo, alisema:
“Huyu mwanamke ni mbaya sana, ametuchanganya mimi na rafiki yangu Dullah, yeye kaja kwangu jana Jumapili akaniambia  amefukuzwa na mumewe hivyo anaomba alale kwangu kesho  yaani leo aende kwao Matombo kumbe alisharudishwa kwao toka juzi.”

Naye mwanamke huyo alipohojiwa na paparazi wetu alikuwa na haya ya kusema:
“Huyu mwanaume (Ramadhan) hajanioa, kila siku nikimwambia twende kwa wazazi wangu ananipiga danadana. Ni kweli nimetoa mimba yake, siko tayari kuzaa naye mtoto nje ya ndoa. Huyu Elias, yeye alionesha nia ya kunioa.”

Mume wa Asha, Ramadhan Ally.

Diwani wa Kata ya Mbuyuni, Samuel Msuya amethibitisha kutokea kwa fumanizi hilo kwenye mtaa wake lakini aliwatupia lawama polisi wa pikipiki kwa kupuuza uongozi wa juu wa kata hiyo ambao kwa kushirikiana na walinzi wa jadi walifanikiwa kuwalinda watuhumiwa wao na kufika salama kwenye kituo cha polisi.
habari kamili :: read more...

Wednesday, May 28, 2014

Mkuu wa jeshi aponea chupu chupu ya kifo huko Somalia.

Mkuu wa jeshi la Somalia ameponea chupuchupu kuuawa mjini Mogadishu.

Hili ndilo shambulio la punde zaidi katika msururu wa mashambulio dhidi ya viongozi wa serikali na rasilimali za serikali nchini humo.Gari lake Jenerali Dahir Aden Elmim lilirushiwa bomu katika barabara kuu karibu na afisi za wizara ya ulinzi mjini Mogadishu.

Aliponea kwa sababu yeye huendesha mojawepo ya magari machache yaliyo na uwezo wa kudhibiti shambulio la risasi, ambayo yametengewa viongozi wakuu wa serikali hiyo.

Hakuna yeyote aliyedai kuhusika na shambulio hilo kufikia sasa japo inafahamika kuwa kundi la Al shabaab limekuwa likifanya mashambulio ya mara kwa mara mjini Mogadishu.

Mwishoni mwa juma, watu 15 waliuawa katika shambulio lililolenga jengo la bunge la Somalia. Wengine wengi walijeruhiwa wakiwemo wabunge 3.
habari kamili :: read more...

INASEMEKANA MUME WA FLORA MBASHA AMEMBAKA SHEMEJI YAKE MWENYEWE UMRI WA MIAKA 17.

Dar es Salaam.

Mume wa mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili,  anatuhumiwa kumbaka shemeji yake mdogo 17.
Taarifa za tukio hilo ziliripotiwa juzi saa 12 jioni katika Kituo cha Polisi Tabata (Tabata Shule), zikimtuhumu mwanamume huyo kwamba alimbaka binti huyo mara tatu na kumsababishia maumivu makali.

Binti huyo alifika katika kituo hicho cha polisi akiwa na ndugu zake wawili ambao walilalamika kwamba kulikuwa na jitihada kubwa kutoka upande wa mtuhumiwa wa kuzima kesi hiyo.
Akizungumza na blog hili nje ya kituo hicho, binti huyo alisema shemejiye alimbaka mara ya kwanza, Ijumaa iliyopita na Jumapili alipombaka mara mbili ndani ya gari.

Alisema mara ya kwanza alikaa kimya baada ya mtuhumiwa kumtishia kwamba angemdhuru kama angetoa taarifa ya tukio hilo alilofanyiwa wakiwa sebuleni nyumbani kwako Tabata Kimanga, lakini aliamua kutoa taarifa kwa ndugu zake baada ya kubakwa mara ya pili.

Polisi katika kituo hicho walithibitisha kupokea taarifa za tukio hilo lakini walishindwa kwenda kumkamata mtuhumiwa kwa maelezo kwamba hawakuwa na askari wa kutosha na kuahidi kwamba angekamatwa jana. Hata hivyo, hadi jana mtuhumiwa huyo alikuwa hajakamatwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi kutwa nzima ya jana hakupatikana kuzungumzia tukio hilo na kila simu yake ilipopigwa (kati ya saa nane mchana na saa mbili usiku), ilipokewa na msaidizi wake akisema bosi wake ana kazi nyingine.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema hakuwa amepokea taarifa yoyote ya aina hiyo.

Mwimbaji anena
Alipoulizwa jana, mwimbaji huyo alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia kwa undani tuhuma zinazomkabili mumewe na kwamba alikuwa anajisikia vibaya kutokana na tukio hilo kuhusisha watu wake wa karibu.

“Of course (bila shaka), hili sio tukio zuri. Kwa sasa sina uwezo wa kuzungumza kwa sababu hili suala lipo Polisi. I am confused (nimechanganyikiwa), ukizingatia kwamba linasemekana kutokea wakati sikuwepo nyumbani, naomba tuzungumze baada ya akili kutulia,” alisema.

Kadhalika, jana saa 6:20 mchana, gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza na mtuhumiwa ambaye baada ya kupewa maelezo kuhusu tuhuma zinazomkabili alisema: “Samahani sana ujue sikusikii kabisa,” kisha alikata simu.
habari kamili :: read more...

MSANII WA BONGO MOVIE RECHO ATAZIKWA KESHO DAR.

Marehemu Rachel Haule 'Recho' enzi za uhai wake.
MSANII wa filamu Rachel Haule 'Recho'  aliyefariki dunia siku ya jana atazikwa jijini Dar es Salamm siku ya kesho badala ya  Songea kama ilivyopangwa hapo awali.
Ratiba ya kuuaga mwili wa marehemu inabaki pale pale siku ya kesho Leaders Club na baadae kwenda kuzikwa katika makaburi ya Kinonondoni.
habari kamili :: read more...

Baada ya Ndikumana kutoeleweka haya Ndio ayafanyayo Irene Uwoya na mijanaume.

Siku kadhaa zilizopita kuliwahi kulipotiwa na kuonesha picha Irene Uwoya akimtomasa sehemu nyeti Msanii mwenzake wa maigizo Haji Adam na kuzua mambo mengi hasa katika mitandao ya kijamii, lakini haikuishia hapo wawili hawa wamekuwa wakionekana pamoja mara kwa mara tena nyakati za usiku na pozi zao zinaonyesha ishara ya mahaba,ndipo swahilitz iliamua kumtafuta Haji Adam lakini hatukuweza kumpata vilevile ilitokea kwa irene uwoya kwani namba yake ilikuwa haipatikani ndipo tulibahatika kupata mawasiliano ya rafiki wa karibu na Irene ndipo akafunguka "Mbona hao wapenzi kitambo sema nyiye mmechelewa kufahamu ukweli tu" alimaliza rafiki huyo
Chanzo:williammalecela.com 

Msami ambae ni staa wa single ya ‘sound track’ amehusishwa na uhusiano wa kimapenzi na Irene Uwoya.

uuuHaya ni majibu ya Msami alipoulizwa juu ya uhusiano na Irene Uwoya>>’Nipo na uwoya kivipi? hizi stori sijui nani kakupa bwana’

Majibu ya mpenzi wa Msami anaitwa Rehema>>’Maswali gani hayo mpigie mwenyewe muulize kifupi yeye ana mambo yake mwenyewe hamna lolote tamaa za vijana wanapotoka wanashawishika na tamaa ya hela, sijui wanajifanya wao meneja,yule mimi kuniacha ni ngumu sana yaani hata apite nani na nani kuniacha mimi hawezi yaani nina uhakika huo na najua mpaka jana nawasiliana nae yaani yule chapa ilale sisikii wivu’

‘Mimi najiamini na najikubali kwamba hata nikitokea hawezi kuongea chochote Msami, hata Uwoya simuogopi kwa sababu staa? maana hata mie staa, hawezi kuwa anammiliki maana kama angekua anammiliki asingekua na ruksa Msami akamwambia nina mwanamke wangu ana hivi na hivi maana hata uwoya mwenyewe ananijua’

‘Yeye mwenyewe anatakiwa kujiheshimu kwanza ajitazame yeye mkubwa halafu lazima ajihesabie katembea na watu wangapi na nasikia taarifa yake kuwa yeye kawaida yake yaani kila mtu mtaani analalamika, anajishusha sana tofauti na wenzake wanaojiheshimu, kwa sababu sio rika lake kwa mtu anayejiheshimu hawezi kufanya hivyo’.

picha: www.makorokocho.co
habari kamili :: read more...

Hii ndo video ya House Girl aliyelazimishwa kufanya mapenzi na Mbwa na Bosi wake Mzungu.

habari kamili :: read more...

Tuesday, May 27, 2014

Majina ya walioitwa katika usaili UHAMIAJI NAFASI ZA KONSTEBO WA UHAMIAJI NA KOPLO haya hapa katika pdf.

Kuona majina hayo bofya hapa
habari kamili :: read more...

Mamen igeni staili Hii kuwafikisha kileleni haraka mashii zenu.

Mimi sio mwigizaji, zaidi ya hapo nilikuwa mtu wa mwisho kwenye maigizo kipindi cha shule ya msingi, ila nina uwezo mkubwa wa kusema "Oooh, hapo hapo.. unanifikishaaa!", mpaka mwanaume akahisi kweli amenifikisha, hata hivyo siko peke yangu wanawake wengi tu wanaigiza wakati wapo wanafanya mapenzi.
Utafiti wa kitaifa wa ngono uliofanywa na chuo cha indiana, ulionyesha asilimia 85% ya wanaume wakisema mara ya mwisho kufanya ngono waliwafikisha kileleni wenza wao, hata hivyo asilimia 64% tu ya wanawake walisema walifika kileleni mara ya mwisho walipofanya ngono, hii inamaanisha ni hesabu ya ajabu hata mtoto wa darasa la pili anajua imekosewa, na inamaanisha asilimia 21% ya wanaume walidanganywa na milio ya kimahaba ya wenza wao na wakaamini kuwa waliwafikisha.
Iwapo tukichukulia na wewe utaki kuwa mmoja wa hao waliodanganywa na mbaya zaidi hawakua na ufahamu wowote kuwa wamedanganywa, waulize wanaume wamekuandalia dalili zinazoonyesha na zitakazokuwa zinakuonyesha iwapo unadanganywa.

        #1; Unamwelewa

Tuweke hivi, "Ooooh, hapo hapo usiitoe... ooh, naisikia mpaka kichwani!", mwanamke huwa anasema hivi akiwa anakandwa miguu yake na maji ya moto baada ya safari ya miguu ya mwendo mrefu, "OH... USI...., JAMA... UNA.... NDIO...., HAPO HA...", hivi ndomwanamke anavyosema ukiwa unashughurika vizuri kitandani, akiweza kuunganisha sentensi nzima na ikaeleweka ujue anakuzuga, maana akifikia mshindo akili yote inakua kama haifanyi kazi vizuri na ikitokea akiwa analia kama kwenye video za ngono wanavyolia, ujue anakusubiri umalize mambo yako aanze kukuelezea shida zake alizonazo, wale wa kwenye video za ngono huwa wana igiza, mwanamke wa kihalisia wa kawaida huwa hawafiki kileleni iwapo mwanaume anatumia nguvu ovyo ovyo bila ya mpangilio na msuguano wowote unaohusisha kinembe.

         #2; Anakubusu bila kuacha

Kwa mwanamke ili afike mshindo, inabidi awe na umakini mkubwa na kuweka hisia zake zote kwenye msuguano na msisimko anaoupata mwilini mwake ili afike mshindo, kubusu na kutekenya hawezi kuvifanya kwa wakati huo ambao anaweka mawazo yote mahala hapo, ukiona unataka kumpiga denda akageukia pembeni ujue mambo ndoyamemkolea vizuri na sio vinginevyo.

        #3; Uso wake unakuwa mzuri

Ulishawahi kujiangalia kwenye kioo wakati uume wako unagombana na mikono yako, najua ulishawahi kujisugua, nani ambae hajawai..., hakuna!, na unaelekea yale mambo kumwagika, unajua usowako unakuwaje?, uso wako unakuwa kama vile unataka kutolewa maisha au kama unataka kulia vile, binadamu wote wako sawa upande wa kihisia, hata wanawake pia!, akiwa na sura nzuri wakati ndo anafika mshindo ujue hapo hakuna!, anatakiwa kuwa na sura ambayo haina mvuto kama anataka kulia na sio awe bado anapendeza kama ndo anaingia harusini.

      #4; Unafanya mapenzi na mpenzi wako kwa stairi ya kimbwa mbwa

Mwanamke kufika kileleni kwa stairi ya kutoka kwa nyuma ni sawa na wewe kufika mshindo huku mwanamke akiwa anakuchzea kwa mikono.
Sijasema haiwezekani, ila inahitaji ufundi mkubwa na dereva inabidi awe anaijua kwa umakini mkubwa njia yake anayopita, ili manbo hayo yaweze kutokea, kwa hio nitakua na wasiwasi kama mwanamke akisema kafika kileleni kwa kutumia hio stairi, mwanamke anauwezo mkubwa wa kufika kileleni iwapo anafanya mapenzi ila yeye ndo yuko juu ya mwanaume kashika msukani, au kwa stairi ya missionary inayoitwa Coital Alignment Technique kwa kifupi The Cat, najua huijui... i gugo(google) na utaiona.

     #5; Ngozi yake inakuwa nyororo na kavu

Mwanamke akiwa amefika kileleni, moyo, presha ya damu na mdundo vyote vinakuja juu ambavyo inamaanisha lazima jasho limtoke kwa aina yeyote ile na mwili unakua na majimaji kwenye ngozi, hii ni moja ya dalili amekwea mlima na kufika kileleni kwa furaha.
habari kamili :: read more...

Jeshi la nchini Nigeria limesema linajua mahali walikofichwa zaidi ya wasichana 200 waliotekwa.

Jeshi la nchini Nigeria limesema linajua mahali walikofichwa zaidi ya wasichana 200 waliotekwa wakiwa shuleni lakini hawawezi kuitaja sehemu hiyo hadharani.

Wasichana hao walitekwa na kundi la kigaidi la Boko Haram ambalo linadai haliwezi kuwaachia hadi watakapobadilishana wafungwa wao na serikali ya nchi hiyo.
Kwenye kituo cha TV cha Nigeria, imetangazwa kwamba japo imefahamika walipo Wasichana hao ambao bado wanashikiliwa mateka….. majeshi ya Nigeria na mengine yanayoendesha opareshen hiyo hayatotumia nguvu za kijeshi kwenye uokoaji wa wasichana hawa.

Kitendo cha kutekwa kwa wasichana hao kimeibua majonzi makubwa miongoni mwa wazazi na kufanya kuibuka kwa kampeni iliyosambaa katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari yenye jina la Bring Back Our Girls ikimaanisha “Rudisheni wasichana wetu”

habari kamili :: read more...

BREAKING NEWS!! MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Rachel Haule ‘Recho,’ amefariki dunia asubuhi hii.

Rachel Haule ‘Recho' enzi za uhai wake.
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Rachel Haule ‘Recho,’ amefariki dunia asubuhi hii. Marehemu amepoteza maisha mara baada ya kujifungua. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!
habari kamili :: read more...

Picha chafu za Mke wa kigogo Dodoma hizi hapa.

Picha zake zasambaza baada ya kuchepuka na dent wa udom


habari kamili :: read more...

BINTI ALIYEZIKWA AIBUKIA NYUMBANI KWAO AKIWA MZIMA.


 HOFU ya ushirikina imetikisa Mkoa wa Arusha kufuatia tukio la hivi karibuni ambapo mwanafunzi wa Chuo cha Kompyuta jiji hapa, Witness Obed (21) aliyefariki dunia Aprili 12, mwaka huu na kuzikwa kwenye makaburi ya nyumbani kwao Kijiji cha Nanja, Kata ya Moshono wilayani Arumeru, Arusha kuibuka akiwa hai.

Witness Obed (21) aliyefariki dunia Aprili 12 mwaka huu na kuzikwa kwenye makaburi ya nyumbani kwao Kijiji cha Nanja, mkoani Arusha na kuibuka akiwa hai tena.

Binti huyo aliibuka kwao hivi karibuni akiwa mpole na kuwafanya baadhi ya watu, wakiwemo wazazi wake kutimua mbio kwa hofu.
Watu kutoka maeneo

mbalimbali jijini hapa  wamekuwa wakimiminika nyumbani kwa wazazi wa binti huyo kwa lengo la kumshuhudia kwa vile ndugu walishaamini kuwa, mpendwa wao huyo alishakufa na alizikwa.

Umati wa watu ukiwa katika hali ya mshangao kutokana na tukio hilo.

UWAZI LATIA TIMU NYUMBANI
Baada ya kusikia taarifa hizo, Uwazi lilifunga safari mpaka eneo la tukio na kumshuhudia binti huyo kisha likaenda kwenye kaburi alilozikwa.

Kwenye kaburi hilo, msalaba wenye kuonesha siku yake ya kuzaliwa (1992) na kufa (12, Aprili, 2014) ulikuwa bado umesimama imara huku kaburi lenyewe likionesha dalili ya kutitia kidogo.

BABA MZAZI ASIMULIA
Akisimulia mkasa huo kwa mshangao mkubwa, baba mzazi wa binti huyo, Obed Leiyo alisema:
“Ilikuwa Aprili mwanzoni, binti yangu alitoweka nyumbani  baada ya kurudi kutoka chuoni majira ya saa 2 usiku akiwa amechelewa.

Hili ni kaburi alipozikwa Witness Obeid Leiyo.

Mimi kama mzazi nilimfokea kwa kuchelewa kwake kurudi nyumbani.
“Yeye kwa hasira zake alizunguka nyumba akaondoka muda huohuo na hakurudi kabisa hapa nyumbani.

“Siku iliyofuata tulianza kumtafuta maeneo mbalimbali bila mafanikio, tukatoa matangazo kwenye vyombo vya habari lakini binti yangu hakuonekana.”

TAARIFA ZAFIKA, KAFA
Mzazi huyo aliendelea kusema: “Siku moja tulipata taarifa kwamba kuna mwili wa msichana umeonekana  katika Kijiji cha Bwawani hapahapa Arumeru.
“Mimi pamoja na ndugu wengine tuliamua kwenda katika kile kijiji. Tulipofika tuliambiwa ni kweli mwili wa msichana uliokotwa lakini wananchi wakauzika.”

WAFUKUA KABURI
Baba huyo anaendelea: “Niliamua kwenda Kituo cha Polisi cha Usa River ambako niliomba kibali kwa ajili ya kufukua kaburi na kuutoa mwili ili kuutambua kama ni binti yangu au la!

“Nilipewa kibali, tukafukua kaburi na kutoa mwili. Nilimtambua kuwa ni binti yangu kutokana na alama mbalimbali alizokuwa nazo, ikiwemo rangi kwenye kucha na sehemu ya kushoto ya uso ilikuwa nyeusi kwa sababu aliwahi kupooza.

Witness akiwa na baba yake mzazi, Bw. Obeid Leiyo Mara baada ya kurudi nyumbani akiwa hai.

MWILI WASAFIRISHWA, WAZIKWA
Baba huyo wa Witness alizidi kueleza kuwa waliusafirisha mwili huo hadi nyumbani kwake Moshono na kuandaa taratibu za mazishi ambapo Aprili 23, mwaka huu mwili ulizikwa.

AIBUKA GHAFLA
Hata hivyo, Obed anasema alishangaa siku ya tukio kumwona binti yake huyo akiibuka nyumbani hapo akiwa hai jambo ambalo lilimshangaza na kumfanya akimbie kwanza na baadaye kufanya mawasiliano naye.

BINTI ASIMULIA
Akizungumza na Uwazi, binti huyo alikiri kutoweka nyumbani kwao Aprili 15, mwaka huu na kwenda kusikojulikana.

Alisema hakujua kilichoendelea baada ya kuondoka nyumbani lakini baadaye alibaini kuwa alikuwa katika Kijiji cha Olkokola wilayani Arumeru na alikwenda kwenye nyumba ya mwanamke mmoja asiyefahamiana naye akamuomba maji ya kunywa.

“Nilifika kwenye nyumba moja nikamkuta mama mmoja, nikamwomba maji ya kunywa akaenda kuniletea. Nilikunywa huku amenisimamia, lakini maji yalikuwa machungu sana, nikamrudishia, akanilazimisha ninywe kwa kunisukumia kikombe kinywani. Nilipomaliza nilipoteza fahamu.

“Baadaye nilizinduka, nikaendelea kuishi palepale nyumbani kwa yule mama  lakini sifahamu nilikuwa nafanya nini.

“Juzi ndiyo nikashangaa
kujikuta nimerudi nyumbani, mimi sijui nini kilikuwa kikiendelea,” alisema binti huyo.

MAJIRANI NAO
Majirani kadhaa waliokuwepo nyumbani kwa Obed walilielezea tukio hilo kwamba ni la ushirikina huku wakisema ni jambo la kuogofya ambalo halikuwahi kutokea kijijini hapo kabla.

Wengine walisema kuwa binti huyo alifufuka na wengine walisema alichukuliwa msukule.
“Hili si suala la kawaida lazima kuna ushirikina kwani huyu binti tulishamzika na wazazi wake walimtambua kabisa kuwa ni yeye baada ya

kuambiwa alikutwa amekufa, sasa hebu fikiria tangu tumezika mbona hakuna mtu aliyekuja na kusema na yeye alipotelewa na binti yake halafu cha ajabu hilo kaburi mbona limebonyea? Atakuwa amefufuka,’ alisema mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Amina Liwa.

Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Usa River, Benedict Mpujila amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema uchunguzi unafanyika.

KUMBUKUMBU
Mapema mwaka jana tukio la kishirikina liliibuka katika wilayani Arumeru eneo la Kwa Mrefu ambapo mtu mmoja alidaiwa kudondoka na ungo, muda mfupi baadaye alitoweka na kwenye ungo kubaki mayai na kuku mweupe.
habari kamili :: read more...
 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top