Tuesday, December 16, 2014

UPDATES ZA MATOKEO MIKOA MBALIMBALI YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA YALIYOKWISHA TANGAZWA HADI SASA.

 Mbozi; Mtaa Masaki: CHADEMA 99, CCM 44

Kigoma Mjini; Mtaa wa Gezaulole: CHADEMA 240, CCM 198

Ukonga- Mtaa wa Kivule Majohe: CHADEMA 231, CCM 77

Musoma Vijijini- Kijiji cha Muhoji: CHADEMA 197, CCM 464

Ubungo- Mtaa wa Msewe: CHADEMA 683, CCM 356

Kinondoni- Mwenge Nzasa: CHADEMA 344, CCM 318

Tarime Forodhani boda (kitongoji): CHADEMA 289, CCM 90

Tarime Forodhani Kijiji: CHADEMA 312, CCM 99

Monduli Mto wa Mbu Kijiji Jangwani: CHADEMA 147, CCM 124

Mwanga Kitongoji Mgagao: CHADEMA 56, CCM 32

Rorya- Mtaa Ngasaro: CHADEMA 480, CCM 360

Arumeru Mash. Mtaa wa Manyata: CHADEMA 168, CCM 91

Ubungo- Mbezi Yusuph: CHADEMA 190, CCM 163

Mwanga- Mtaa Mtahang’a: CHADEMA 116, CCM 73

Ilemela- Mtaa wa Pasiansi: CHADEMA 689, CCM 247

Karatu- Mtaa Mazingira: CHADEMA 290, CCM 130

Karatu Mtaa wa Maliasili: CHADEMA 240, CCM 77

Karatu- Mtaa wa Manyara: CHADEMA 220, CCM 170

Tarime Mtaa wa Bugosi: CHADEMA 438, CCM 138

Tarime Mtaa wa Regoryo: CHADEMA 191, CCM 75

Segerea Mtaa wa Migombani: CHADEMA 547, CCM 225

Mamlaka ya Mji mdogo Shirati-Rorya ina mitaa 9: CHADEMA mitaa 7, CCM mitaa 2

Mererani mitaa 8: CHADEMA mitaa 7, CCM mtaa 1

Magu Mjini: CHADEMA mitaa 10, CCM mitaa 7

Manispaa ya Bukoba: Mitaa 66 ndani ya Manispaa ya Bukoba, CCM wamepata mitaa 35 huku upinzani ukijinyakulia mitaa 31.

Jumla ya Wajumbe 330 walitakiwa ambapo wapinzani wamepata WAJUMBE 205 dhidi ya CCM waliopata WAJUMBE 125.

Wilayani Karagwe: Wilaya ina jumla ya mitaa/vijiji 18, Upinzani wamejinyakulia vijiji/mitaa 12 huku CCM wakipata vijiji/mitaa 6

Wilaya ya Nachingwea: Kitongoji cha Raha Leo, CCM 60 na Chadema 59.
Kitongoji cha Amani: CCM 35 na CDM 9.

Kijiji cha Mnyune: CCM 207 na CDM 20.

Monduli Magharibi: CDM 76, CCM 199.

Monduli Mjini Mashariki: CDM 57, CCM 88 na Mtaa wa Sabasaba CDM 84, CCM 172.

Kitongoji cha Mandela, Kata ya Mkalama: CCM imeshinda kwa kura 240 na CDM 196.

Kitongoji cha Kichangani Kata ya Gairo Mjini: CCM 260, CDM 115 zilozoharibika 2.

Wilaya ya Kyela: Orodha ya Vitongoji na chama kilichoshinda
Butiama- CHADEMA
Kyela kati -CHADEMA
Roma -CHADEMA
Mikoroshoni -CCM
Mbugani -CHADEMA
Nazareti -CHADEMA
Unyakyusa -CCM
Kapwil- CCM
Itunge mashariki -CCM
KEIFO -CCM
OROFEA -CHADEMA
SAMA B -CCM
Mikumi -CHADEMA
Mwaikambo -CHADEMA
Kilasil- CCM
Mkombozi -CHADEMA
Bondeni A-CCM
Bondeni B-CHADEMA
Itunge-Mundekesye CHADEMA

Tarime; Mtaa wa Bhughucha: CHADEMA 135, CCM 123

Tarime; Mtaa wa Buhemba: CHADEMA 104, CCM 50

Tarime; Nyarusahi: CHADEMA 197, CCM 54

Tarime; National: CHADEMA 170, CCM 130

Tarime; Kijiji Nyabitocho: CHADEMA 899, CCM 315

Segerea; Migombani: CHADEMA 547, CCM 225

Huko Mvomero hadi sasa kati ya Vijiji 20 vya awali

CHADEMA Vijiji 15
CCM Vijiji 5

Vijiji hivyo 15 ni; Sarawe, Lungo, Kidudwe (nyumbani kwao mbunge wa Mvomero), Mndelwa, Masili, Ndugutu, Lukunguni, Mwalavi, Mvomero, Bumu, Madizini, Doma, Mlali, Tchenzema na Nanyinga (nyumbani kwa Mwenyekiti wa Halmashauri- CCM).

VURUGU SIMIYU: Watu 600 wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chadema wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Simiyu wakihusishwa na vurugu za uchaguzi wa serikali za mitaa jana.

Kabla ya kukamatwa hapo jana kati ya saa 2 – 3 asubuhi, polisi walilazimika kuwatawanya wafuasi hao wa Chadema kwa mabomu ya machozi walipokuwa wakipinga uchaguzi kufanyika leo badala ya kufanyika jana kama ilivyopangwa.

Kutokana na kulipuliwa mabomu ya machozi, huduma za usafiri wa mabasi kutoka na kuelekea Mwanza, Musoma, Bunda, Tarime, Simiyu zilisimama.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Charles Mkumbo alipopigiwa simu kutoa kauli kuhusu sakata hilo, hakupokea simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu hakujibu.

Takwimu uchaguzi: Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa taarifa ya Takwimu ya mambo yaliyotokea wakati wa kampeni za Uchaguzi Serilali za Mitaa.

Takwimu hizo zinaonyesha kuwa Mkoa wa Tabora unaongoza kwa ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi ukifuatiwa na Kagera wakati Shinyanga na Mbeya wakifanya vizuri.

Kwa upande mwingine takwimu zinaonyesha kuwa kukosekana kwa mwamko wa kisiasa 19%, kampeni kuisha baada ya muda 18%, ratiba za kampeni kuwa wazi 12%, rushwa kwa wapiga kura10%, huku kampeni kuzuiwa na mamlaka 1% na vitisho kutoka kwa watu wasio vyombo vya dola 1%.

Mgombea Chadema atumbukia shimoni, afariki: Aliyekuwa mgombea ujumbe katika Kituo cha Msalala Road, Geita kupitia Chadema, Bethar Nchimani Ngosha amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye shimo la choo lililokuwa limejaa maji.

Baada ya kutangaziwa kuwa ameshinda, marehemu alikuwa anaelekea uani, karibu na choo kulikuwa na shimo la choo lililokuwa wazi ndipo alipodumbukia na mauti kumpata.

Akataa kusaini: Mtaa wa Katoma Geita Mjini wananchi wamekesha kusubiri matokeo.Mgombea wa CCM ameshindwa na amekataa kusaini matokeo.

Mabomu yatumika: Jeshi la Polisi limeamua kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi mkoani Mwanza katika maeneo ya Pasians, Mji Mwema, Kirumba, Ibungiro na Kitangiri baada ya vurugu wakati wa kusubiri kutangazwa matokeo.

Kijiji cha Muungano Kata ya Chahwa mkoani Dodoma: CHADEMA 196, ADC 38

Mbozi; Mtaa wa Masaki: CHADEMA 99, CCM 44

Kigoma Mjini; Mtaa wa Gezaulole: CHADEMA 240, CCM 198

Ukonga; Mtaa wa Kivule Majohe: CHADEMA 231, CCM 77

Musoma Vijijini; Kijiji cha Muhoji: CHADEMA 197, CCM 464

Ubungo; Mtaa wa Msewe: CHADEMA 683, CCM 356

Kinondoni; Mwenge Nzasa: CHADEMA 344, CCM 318

Mwanga Mtaa wa Lwami: CHADEMA 55, CCM 35

Mererani: CHADEMA imeshinda mitaa 7 kati ya 8

Kitongoji cha Endulele: CHADEMA 170, CCM 130

Monduli; Kitongoji Kambi ya Mkaa: CHADEMA 27, CCM 13

Mwanga Mtaa wa Lwami: CHADEMA 55, CCM 35

Arumeru Magharibi, Kitongoji Endulele: CHADEMA 170, CCM 130

Ushirombo Mjini: CHADEMA inaongoza vitongoji 10, CCM inaongoza vitongoji 4

Moshi Manispaa, Kitongoji Longuo A: CHADEMA 206, CCM 66

Mbozi Mtaa wa Mbugani: CHADEMA 227, CCM 160

Kata ya Mji Mpya, Morogoro yenye mitaa 12, CCM imeshinda mitaa 9, CHADEMA wakishinda mtaa 1 huku mitaa miwili mpaka sasa bado vurugu zimetanda baada ya kura kudaiwa kuzidi huku watu kadhaa wakituhumiwa kupiga kura mara mbili.

Kagondo, Kata ya Muhutwe, Kagera: CHADEMA imeshinda mitaa 4 kati ya 5

Kufungwa Vituo: Katika maeneo mengi vituo vya upigaji kura tayari vimefungwa huku wananchi wakisubiri kwa hamu kujua matokeo.

Uchaguzi Migombani: Uchaguzi wa Serikali za Mitaa eneo la Migombani, Segerea jijini Dar umeingia dosari baada ya Afisa Mtendaji Kata ya Segerea kutangaza kusitisha uchaguzi huo kimyakimya bila sababu za msingi ambapo wananchi waliamua kumweka mtu kati mpaka akaruhusu uchaguzi huo kuendelea kwa maandishi. Akijitetea afisa huyo alidai kuwa ameagizwa na Mkurungenzi wa Uchaguzi wa Manispaa ya Ilala kufanya hivyo.

Mazimbu, Morogoro: Eneo la Mazimbu, Moro kimenuka mpaka wanajeshi wamelazimika kuingilia kati kutuliza ghasia wakati wa zoezi la upigaji kura.

Kawe, Dar: Uchaguzi wadaiwa kuingia dosari baada ya mgombea wa CCM kutoa amri ya vitabu kufungwa kabla ya muda ulipangwa.

Kigogo, Dar: Mgogoro umezuka katika Kituo cha uchaguzi Kigogo jijini Dar baada ya wananchi kudai kuwa baadhi ya watu wamepelekwa kama mamluki eneo hilo kwa ajili ya kugipa kura.

Sokoine-Kibaoni, Morogoro: Wananchi eneo la Sokoine-Kibaoni, Wilaya ya Mvomero, Morogoro mpaka sasa bado hawajaanza kupiga kura mbali na wengi wao kujitokeza huku wengine wakiwa wamekodi magari kutoka Bwawa la Kihonda umbali wa kilomita 20 kwenda kupiga kura lakini mpaka sasa bado hawajapiga kura.

Amana, Ilala: Baadhi ya wananchi wameamua kususia zoezi la upigaji kura katika Kituo cha Amana, Ilala jijini Dar baada ya mgombea Uenyekiti wa Mtaa wa Amama aitwaye Mathias Ijumba kuondolewa katika uchaguzi dakika za mwisho kwa kile kinachodaiwa kuwa si mkazi wa eneo hilo lakini jambo la ajabu jina like liko katika orodha ya watu waliojiandikisha kupiga kura na mgombea huyo ameruhusiwa kupiga kura yake.

Baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamedai jamaa huyo anakubalika sana na huenda ndiyo chanzo cha jina lake kuondolewa.

Dar es Salaam: Wananchi katika vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam wanalalamikia utaratibu wa majina unaotumika katika zoezi la upigaji kura linaloendelea, wengi wadai kupata tabu kuona majina yao huku wengine majina yao yakiwa hayapo kabisa katika vituo.

Shariff Shamba, Ilala: Eneo la Shariff Shamba, Ilala jijini Dar uchaguzi umeahirishwa mpaka Jumapili ijayo baada ya vifaa kutopatikana ndani ya muda muafaka. Vyama vyote vinavyoshiriki vimeafikiana.

Kagunga, Kigoma Kaskazini: Uchaguzi katika Vijiji vya Zashe na Kagunga, Kata ya Kagunga, Jimbo la Kigoma Kaskazini umefutwa hadi itakapotajwa tena baada ya Mtendaji wa Kata kuwaengua ACT katika uchaguzi huo baada ya kudaiwa kuwa wagombea wawili wa vijiji hivyo kutoka ACT walitumia anuani ya shule kama anuani yao. Hata hivyo Msimamizi Mkuu amesema anafuta uchaguzi hadi watakapotangaza tena.

MCHINA AMLA MATE DADA WA KIBONGO MBELE ZA WATU.



UNGANA NAMI KATIKA FACEBOOK KWA KUBOFYA Like HAPO JUU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top