Gazeti la New Times la Rwanda limeandika kuwa Bi Shyrose aliporomosha matusi mazito na maneno ya kashfa dhidi ya wabunge wenzake na viongozi wa mataifa kadhaa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Hilo ndilo linalodaiwa kusababisha kuvunjika kwa vikao ambapo wabunge wenzio walimtaka Spika wa EALA, Bi Margret Nantongo Zziwa, amchukulie hatua Shyrose lakini hawakufanikiwa.
Kando na hilo kumekuwa na ujumbe unaosambazwa katika Whatsapp ukidai kwamba mbunge huyo alianzisha ugomvi ndani ya ndege wakati yeye na wabunge wenzake wakisafiri kwenda Ubelgiji hivi karibuni kwa shughuli za kikazi. Inaelezwa alikuwa kaambatana na wabunge wengine kutoka Tanzania, Adam Kimbisa na Angela Kizigha.
Hata hivyo Taarifa News haikufanikiwa kumpata Shyrose kujieleza kuhusu tuhuma hizo nzito na ambazo kama atapatikana na hatia kupitia taratibu za EALA anaweza kufukuzwa kutoka bunge hilo.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment