Saturday, August 30, 2014

DIVA NA AUNT KIMENUKA MBAYA; CHANZO CHADAIWA UJAUZITO WA AUNT!

JAMBO limezua jambo! Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson amemvaa prizenta wa Kipindi cha Ala za Roho cha Redio Clouds FM, Lovennes Malinzi ‘Diva’ kwa madai kwamba amemtangaza mitandaoni kuwa amepachikwa ujauzito na mume wa mtu ambaye ni densa wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Moses Peter ‘Moze Iyobo’, jambo ambalo ni uongo.

Prizenta wa Kipindi cha Ala za Roho cha Redio Clouds FM, Lovennes Malinzi ‘Diva’

Akizungumza kwa masikitiko ya hali ya juu, Aunt alisema kuwa hakutegemea mtu kama Diva angetumia nafasi yake ya utangazaji kumchafua akimsingizia kuwa ni mjamzito, jambo ambalo limemsababishia matatizo kwenye ndoa yake na mumewe Sunday Demonte.
“Mwanamke kuwa mjamzito si jambo baya lakini kunichafua mbele ya jamii eti nina mimba ya Moze Iyobo, imeniuma sana.

“Hebu vuta picha wakwe, mawifi na mashemeji ambao tayari wameshasikia na kusoma kwenye ukurasa wa Diva, akisema mimi nina mimba ya yule mtoto, dah! Nimeumia sana, kwa kweli siwezi kuliacha lipite hivihivi.

Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson

“Huyo Diva lazima nitasimama naye mahakamani,” alisema Aunt.
Hivi karibuni, kwenye ukurasa wake wa Instagram, Diva aliandika: “Wakati sakata la mtoto mzuri Aunt Ezekiel ana mimba ya Moze Iyobo likipamba moto, mimba ambayo ni tangu Mwezi wa Ramadhan, sasa hesabuni miezi, hapa ni miezi miwili au mitatu.”



HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top