Saturday, June 7, 2014

Mdogo ake Kim Kardashian, Khloe Kardashian atua South kwa ajili ya mapenzi.

Mitandao mingi ya udaku wamekuwa wakiripoti mapenzi mapya kati ya rapper wa Bad Boys record “French Montana” na “Khloe Kardashian” ambaye ni mdogo wake Kim Kardashian.

Khloe alikuwa ni mke wa mcheza kikapu Lamar Odom lakini wamepitia mambo mengi na jinsi ilivyo hivi sasa mahusiano yao hayapo vizuri kabisa.

Sasa kilichotokea hivi sasa ni kwamba Khloe Kardashian amesafiri hadi South Africa kuungana na French Montana ambaye anatarajiwa kufanya show kwenye tukio hilo.

Sifa moja wapo ya mtu yoyote anayekuwa na mahusiano na Kardashian sisters lazima ataandamwa na vyombo vya habari sana haswa mapaparazi. Kanye West alikuwa anasumbuliwa na mapaparazi lakini hali ilizidi baada ya kuanzisha mahusiano na Kim K.

Sasa French Montana na yeye ameshaanza kuandikwa na kupigwa picha na mitandao mingi sana.

Tafadhali bofya like hapo juu kama bado hujabofya upate habari mpya haraka

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top