
Chatu akiwa ametumbukia ndani ya nyumba hiyo kupitia tundu la ukutani
Hicho ni kitambaa ambacho alikuwa amefungwa chatu huyo mkiani.

Chatu akiwa amekatwa katwa na wananchi
Chatu wa ajabu ameuawa jijini Arusha na wananchi 'wenye hasira kali' leo jioni. Alionekana chatu maeneo ya Sakina akiingia kwenye nyumba ya mkazi mmoja wa eneo hilo. Wananchi walipomuona, waliogopa, wakampigia simu mwenye nyumba ambaye wakati huo hakuwepo nyumbani. Lakini cha kushangaza, mwenye nyumba akawaambia wasimuue kwani ni mwanae!

Cha kushangaza zaidi, chatu huyo alipoangaliwa vizuri alionekana anaburuza karatasi nyeupe aliyokuwa amefungwa mkiani ambayo ilikuwa imeandikwa maneno ya kiarabu ambayo hakuna aliyejua yana maana gani, hatimaye chatu huyo ameuawa!
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment