“Unajua mimi ni mtu ninayejitambua na ninayejali maisha yangu hivyo ninapobaini mwanaume f’lani anaonesha kunijali na kunipa mapenzi ninayoyahitaji, kwa nini nisikubali kuingia naye kwenye maisha ya ndoa…?
“Kwa kifupi nampenda Diamond na yeye ananipenda, that’s it,” alisema Wema.
MKWARA WA MAMA YAKE
Kuhusu mama yake kuchimba ‘biti’ kuwa hamtaki Diamond na kamwe hawezi kukubali mwanaye aolewe na mwanaume huyo, Wema alisema:
“Unajua yule ni mzazi, wakati mwingine si mbaya kuonesha hisia zake lakini nitamseti na naamini kwa kuwa ananipenda atakubaliana na mawazo yangu.”
NDOA LINI?
Alipobanwa kuhusu lini watafunga ndoa kwani wamekaa kwenye uhusiano kwa muda mrefu huku wakiachana na kurudiana, Wema alionekana kutokuwa na jibu la moja kwa moja ila akaishia kusema kuwa, siku ikifika kila kitu kitakuwa wazi.

NUKUU YA MAMA WEMA!
Katika sakata hilo, kwa upande wake mama Wema alikuwa na haya ya kusema: “Ndoa yao watafungia chumbani, si hadharani, tena wakiwa na ndugu wa upande mmoja tu wa Diamond.
“Sisi hatuwezi kushiriki ng’oo, ndugu zangu wakijitokeza tu nitakuwa na panga mkononi, watakiona cha moto.”
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment