Monday, February 17, 2014

Picha na matukio ya Mgombea ubunge jimbo la Kalenga kupitia CHADEMA alipochukua fomu.

 Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kalenga Bi Pudensiana Kisaka akimkabidhi fomu ya kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Kalenga Bi. Grace Tendega anayeiwakilisha CHADEMA katika ukumbi wa sayansi na kilimo cha wilaya ya Iringa vijijini leo hii.

kiongozi huyo wa CHADEMA alipokuwa anawasili katika eneo la ukumbi huo kwenda kuchukua fomu hiyo ambayo kwa mujibu ya sheria za uchaguzi huo inatakiwa kurudishwa tarehe 18/02/2014 (kesho, Jumanne)


msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo la Kalenga; Bi. Pudensiana Kisaka alipokuwa anamkaribisha kiongozi huyo wa CHADEMA, Bi. Grace Tendega kuchukua fomu hiyo katika ukumbi huo.

Bi. Grace Tendega alipokuwa anakaribia kukabidhiwa fomu hiyo ya ugombea wa nafasi ya ubunge katika jimbo hilo la Kalenga kupitia CHADEMA

Kiongozi huyo (Grace Tendega) alipokuwa katika ofisi ya  CHADEMA wilaya ya Iringa katika eneo la Mshindo; alipokuwa akijibu maswali waandishi wa habari.
Na Riziki Mashaka.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top