Monday, February 17, 2014

Kesi ya Elizabeth Michael LULU imehairishwa hadi mahakama itakapotoa taarifa tena.


Elizabeth Michael 'Lulu' (katikati) akiwa na mama yake mzazi, Lucresia Karugila (wa pili kushoto) na Dk. Cheni (kulia) ndani ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.

 Leo February 17 kutoka Mahakama kuu kanda ya Dar es salaam, msanii wa maigizo nchini Tanzania Elizabeth Michael maarufu kama Lulu alikuwa akisomewa shitaka lake la kuua bila kukusudia msanii mwenzake wa maigizo Marehemu Steven Kanumba April 07 2012  eneo la Vatican.

Akisoma maelezo ya awali wakili wa serikali Monica Mbogo mbele ya Jaji anayesikiliza kesi hiyo Rose Teemba amesema mshtakiwa siku ya tukio kulikuwa na ugomvi kati ya marehemu na mshtakiwa na baadaye mshtakiwa aliondoka usiku wa saa sita baada ya marehemu kuanguka chumbani ambapo alfajiri ya April 07  majira ya saa 11 alfajiri Lulu alikamatwa eneo la Bamaga.

  Kwa upande wake wakili  Peter Kibatala ambaye anamtetea Lulu amesema wameridhishwa na sehemu kubwa ya  maelezo ya awali ya mteja wao, ambapo kesi hiyo imeahirishwa mpaka itakapopangwa tena huku kila upande ukitarajia kuleta mashahidi watatu.

 Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie waliohudhuria leo mahakamani ni Dr.Cheni na Kajala.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top