Saturday, February 15, 2014

Dayna na Cindy wa Uganda wababwiwa mbaya na mashabiki usiku wa Valentine kwenye shoo.

 

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Dayna Nyange akikamua vilivyo usiku huu wa Valentine Day katika Ukumbi wa JB Belmonte Hotel katika jiji la Rocky City (Mwanza) ambapo katika ukumbi huo huo alikuwepo na mkali  wa muziki Cindy Sanyu kutoka Nchini Uganda pamoja na wasanii wengine wa hapa jijini Mwanza.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Dayna Nyange akifanya mambo yake jukwaani usiku huu.

Dayna akiimba kwa hisia moja ya wimbo wake mbele ya mashabiki wake
Nivute kwako!!! ni wimbo wake msanii Dayna akiuimba vyema Jukwaani leo kwenye Ukumbi wa JB Belmonte Hotel katika jiji la Rocky City (Mwanza) leo Valentine Day.

Dayna Nyange amekamua nyimbo zake kadhaa huku wadau wakimkubali zaidi katika ukumbi huu. Cha zaidi kwa Dayna hakuweza kuficha tabasamu lake huku akijua ni sikukuu ya Wapendanao hivyo amekamua kisawasawa!!!


Cindy Sanyu kutoka Nchini Uganda(katikati) akicheza kwa pamoja na wanamuziki wake kuwapa kile Wabongo walichomwitia katika ukumbi huu wa JB Belmonte Hotel.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top