Monday, November 24, 2014

Polisi amvua mwanamke nguo Kenya.

Afisa mmoja wa polisi wa utawala nchini Kenya ni miongoni mwa wanaume waliokamatwa kwa kujaribu kumvua nguo mwanamke katika mtaa wa Komarock viungani mwa mji mkuu Nairobi.
Polisi walisema watu wanne walimsingira mwanamke huyo alipokuwa anaenda nyumbani kutoka kanisani akiwa ameandamana na rafiki yake.

Wanaume hao walijaribu kumvua nguo mmoja wa wanawake hao ila waliokolewa na wananchi waliokuwa wakielekea makwao.

Wanaume wawili waliokuwa wanawaokoa wanawake hao walijeruhiwa.
Kwa mujibu wa taarifa za mtandao wa Daily Nation, Kioo cha basi iliyokuwa barabarani pia kilivunjika katika purukushanio hilo.

Polisi waliofika katika eneo la tukio waligundua kuwa mmoja wa waliowashambulia wanawake hao alikuwa afisa wa polisi.

Tukio hilo limefanyika siku chache tu baada ya mamia ya wanawake kuandamana mjini Nairobi kulaani kitendo cha kumvua mwanamke mmoja mavazi yake yakisemekana kutokuwa na heshima.

DIAMOND AKAMILISHA KUTEMBEA NA MADEMU WANAOJIITA WAKALI ‘TAKEU’.



HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top