Monday, October 27, 2014

MWONE BOB JUNIOR LIVE NA ‘MCHEPUKO’.

Mchepuko? Baada ya kuachana na mkewe, Halima Ally, staa wa Nyota ya Chipsi Mayai na Prodyuza wa Sharobaro Records, Raheem Rummy Nanji ‘Bob Junior’ amenaswa live na mrembo anayejulikana kwa jina la Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ ambaye ni msanii wa filamu, wakiwa katika mahaba nipoteze kama ndege ya Malaysia.

Staa wa Nyota ya Chipsi Mayai , ‘Bob Junior’ akiangusha busu shavuni mwa mrembo anayejulikana kwa jina la Sabrina Omary ‘Sabby Angel’

Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Sabby ambaye ndiye aliyevujisha picha za tukio hilo, Sabby na Bob Junior kwa sasa wako katika mahaba mazito na ni watu wanaopendana kwa sababu kila unapomuona Sabby yupo karibu na mwanamuziki huyo.

Bebi huyo, ‘Sabby Angel’ akimkubatia 'Bob Junior' kimahaba.

“Sasa hivi Sabby na Raheem ndiyo habari ya mjini kwani kila sehemu wapo pamoja na wanapendana sana,” alidai rafiki huyo wa Sabby.Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba wawili hao wanaweza kuvalishana pete ya uchumba muda wowote kuanzia sasa.
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Bob Junior ambaye hakupatikana lakini alipotafutwa Sabby ili kusikia kauli yake kuhusu uhusiano wake na Bob Junior alikiri na kusema kuwa ni mtu ambaye anampenda na ndiye anamfanya awe na furaha.

Unaambiwa its Full Time Manchester United 1-1 Chelsea.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHIN

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top