Tuesday, September 2, 2014

MARTIN KADINDA: WEMA SEPETU HANA PESA YA KUNILIPA, NAHANGAIKA ILI TUSILALE NJAA.

Martin Kadinda

Kadina amesema kuwa yeye na Wema hawana mkataba wa kulipana bali wapo kishkaji zaidi.

Martin Kadinda ambaye ni meneja wa Wema Sepetu ameibuka na kusema kuwa Wema Sepetu ambaye ni meneja wa Wema Sepetu ameibuka na kusema kuwa Wema Sepetu aliyekuwa akimwaga pesa vilivyo kwasasa hana pesa ya kumlipa bali yeye Martin anahangaika kwa issue zake binafsi ili wasilale njaa

"Wema hana pesa ya kunilipa mimi, ninachokifanya ni  kuhangaika kutafuta deals ili mimi na yeye  maishani tusilale njaa, maisha ni kutegemeana.

"Kikubwa ninachofanya ni kutafuta dili za kazi nyingi ili tuweze kupeana pasu kwa pasu lakini si mshahara, nafanya kazi na bosi wangu Wema kishikaji na kwa kweli nafurahia sana utaratibu huu"

Martin alisema kuwa kama angekuwa na mkataba na Wema kumlipa kila mwezi asingemudu na kusema yupo na Wema kwasababu anajua ni mtu wa aina gani na anafanya kazi zake kwa uhuru bila kubanwa.

Wakati Wema yupo kimapenzi na yule kigogo aliyejulikana kwa jina la Clement(CK),  Wema alidaiwa kumwaga pesa kila kona na wapambe kibao wa kula bata nao huku akiwa na magari kadhaa lakini kwasasa anadaiwa kushuka kiuchumi na kubaki na gari moja pekee huku wapambe aliokuwa nao wakitimua na waliobaki kulalamika hawali bata kama zamani.

Je umeipata hii ya KAJALA KUMWAJIRI WEMA?? Hii Hapa.

Hivi karibuni tena Diamond Platnumz aliye mpenzi wa Wema alisema kuwa Wema ni mtu wa starehe na kuendekeza mashoga wapenda anasa badala ya kutumia fursa na umaarufu mkubwa alionao sasa kufanya kazi zake kwa bidii hususani filamu.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top