Friday, June 6, 2014

Picha mbalimbali za mgomo wa chuo cha NIT.



 Wanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wanaolipiwa na Bodi ya Mikopo wakimsikiliza Makamu Mkuu wa Chuo hicho aliyekuwa akiongea nao.

Makamu Mkuu wa Chuo akijaribu kuwatuliza wanachuo hao kwa kuwaahidi kushughulikia suala lao.

Viti vikiwa vimetawanywa baada ya vurugu zilizosababishwa na mgomo huo.

WANAFUNZI wanaolipiwa na Bodi ya Mikopo katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kilichopo Mabibo Mwisho jijini Dar, leo wamegoma na kufanya vurugu wakidai kucheleweshewa fedha zao za mkopo. Mgomo huo umeanza majira ya saa 6 na nusu mchana ambapo polisi waliingilia kati kutuliza ghasia zilizokuwa zinaendelea chuoni hapo. Mpaka mtoa habari hii anaondoka eneo la tukio, bado wanachuo walikuwa wakisubiri majibu ya uongozi wa chuo hicho
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top