Wednesday, June 4, 2014

Diamond Platnumz azidi kumburuza davido katika BET Awards.

fans’ wanaweza kufanya lolote kuhakikisha wanampa ushindi msanii wao katika shindano lolote linalohitaji ushiriki wao hasa kwa kupiga kura au maoni, kama kinachofanywa hivi sasa na mashabiki wa diamond platnumz katika tuzo za bet.

BET wanaendelea kuweka majina ya nominees katika page zao za mitandao ya kijamii ili kuwapa mashabiki nafasi ya kuwaongezea ushawishi wa kupewa ushindi wasanii wao. Kama ilivyokuwa jana picha ya Diamond imeendelea kupata likes na comments nyingi katika Facebook ya BET, mpaka sasa ina likes 2649 na comments 5471 huku Davido akiwa na likes 1465 na comments 619 tu.

Diamond-Davido-Number-One-Remix-4
Upande wa Instagram ya BET Awards picha ya Diamond iliyowekwa jana usiku na maelezo haya:
‘Dbl tap this pic if you want #DiamondPlatnumz to win #BestInternationalAct: Africa @ the #BETAwards this yr’,

Hadi sasa ina likes 3275 na comments 4354 huku picha ya Davido katika akaunti hiyo ya IG ya BET iliyowekwa siku mbili zilizopita ina likes 518 na comments 2.

Cha kushangaza mashabiki wa Diamond wameamua kutoka nje ya kile kinachotarajiwa baada ya kuamua ku-comment jina la Diamond katika picha hiyo ya Davido.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top