WanaCCM msiwe na shaka, tutavuka kwa nguvu zetu... wingi wenu huu unanipa faraja kuwa katika safari yetu na kwa kumte gemea Mungu tutashinda ...Tulifurahi pamoja, tulihuzunika pamoja na tutashinda pamoja.”
Nguvu ya makundi ya watu wanaotajwa kuwania urais kupitia Chama
Cha Mapinduzi (CCM) zinaendelea kukitikisa chama hicho huku makada wake
wakitoa angalizo wakiutaka uongozi wa juu wa kuchukua hatua haraka za
kinidhamu kwa wahusika.
Wiki iliyopita wanachama wa chama hicho wanaodaiwa
kutoka katika kambi tofauti zinazoisaka nafasi ya urais waliibuka na
kutoa kauli zinazoonekana wazi kupigana vijembe, kila upande ukiuponda
mwingine kuwa unavunja kanuni na katiba ya chama hicho.
Malumbano hayo ya makada wa CCM yanayoonekana
dhahiri kuchagizwa na makundi pamoja na wafuasi wa vigogo wanaousaka
urais kupitia chama hicho.
CREDIT:Mwananchi.
Ingawa makundi yanayosaka urais kupitia chama hicho ni mengi, ni
kundi moja tu linalomuunga mkono aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa
ndilo linaloonekana dhahiri kupigiwa kelele kwa kutajwa kwa majina bila
kificho, hasa baada ya kauli yake kuwa ameanza safari, aliyoitoa mbele
ya wageni wakati wa kuadhimisha mwaka mpya 2014.
Kutokana na kauli hiyo na mambo mengine, Katibu wa
Uhamasishaji na Chipukizi wa UV-CCM, Paul Makonda aliibuka na
kumshambulia Lowassa, suala ambalo limeyaibua makundi mengine, baadhi
yakiunga mkono kauli ya Makonda na mengine yakiibeza na kumshushia
tuhuma za kuvunja kanuni za chama.
Mmoja kati ya waliojitokeza ni Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM,
John Malecela ambaye ameonyesha waziwazi kutofautiana na mipango na
mikakati ya Lowassa.
Malecela anamuunga mkono Makonda, kwa kauli yake,
ikiwamo kwamba Lowassa anafadhili mikakati ya kupingana na juhudi za
sekretarieti ya CCM chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahaman Kinana na Katibu
wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Wakati Makonda na Mzee Malecela wakitoa tuhuma
hizo, makundi mbalimbali ya Jumuiya ya Vijana UVCCM nao wameibuka na
kumshutumu Makonda kuwa aliyoyasema ni maoni yake na siyo msimamo wa
Jumuiya hiyo.
Kauli hiyo ya Makonda imeibua malumbano baina ya
viongozi wa jumuiya hiyo, wengi wakimshutumu kwa “kutumiwa kumchafua
Lowassa” na kwamba kauli aliyoitoa ni ya kwake na idara yake, wala
isihusishwe na Umoja wa Vijana wa CCM.
Baadhi ya waliojibu ni pamoja na wajumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kupitia kundi la vijana, Jonas Nkya na
Ramadhani Kimwaga, pamoja na Mjumbe wa Baraza Kuu la jumuiya hiyo Mkoa
wa Mbeya, Adam Mwakalinga.
Vijana hao kwa nyakati tofauti wanasema
wamehuzunishwa na matamshi ya Makonda akimshutumu Lowassa na kutamka
kuwa umoja huo hautaki kuingizwa katika masuala binafsi ambayo yanaweza
kukigawa chama na jumuiya zake.
Mwakalinga anasema Makonda anapaswa kufanya kazi
ya idara yake ya watoto badala ya kukurupuka na kutaka kuwaaminisha
Watanzania kuwa Edward Lowassa si kiongozi mzuri huku akijua wananchi
wenyewe na hata wapinzani wanaona uthubutu wake katika maendeleo hasa
kwa vijana.
Kauli ya Sadifa
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis anasema kutangaza nia ya kugombea nafasi yoyote ndani ya chama si kosa mradi tu mhusika ataridhika kuwa na nia, sifa na uwezo wa kile anachokisema.
Kauli ya Sadifa
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis anasema kutangaza nia ya kugombea nafasi yoyote ndani ya chama si kosa mradi tu mhusika ataridhika kuwa na nia, sifa na uwezo wa kile anachokisema.
Anasema ingawa UVCCM haijakaa kujadili watu hao,
lakini haoni kosa lolote kwa mwanaCCM kujitokeza na kutangaza nia yake
hadharani.
“Nikuulize mwandishi, kutangaza nia ni kosa? Kama
mtu ameamua kueleza nia yake anakuwa amevunja sheria gani…sioni kosa
lolote endapo mtu ameeleza nia yake baada ya kujiona anazo sifa, uwezo
hiyo ni haki kikatiba,” alisema
Hata hivyo, Sadifa anasema kosa analoliona na
ambalo ni kinyume na kanuni za chama ni kwa mtu kujipitisha na kuanza
kusaka kuungwa mkono ingawa alikiri kuwa kwa yeye kama mwenyekiti hakuna
aliyejitokeza kuomba amuunge mkono.
Anaongeza kusema kuwa kauli iliyotolewa na Makonda si ya Jumuiya kwa kuwa UVCCM haimuungi mkono mgombea yeyote.
“Msemaji wa UVCCM ni mmoja kitaifa na ndiyo mimi,
hakuna msemaji mwingine…yaliyosemwa na Makonda ni yake mwenyewe na siyo
msimamo wa jumuiya,” anasema.
Anaongeza kuwa ingawa Makonda anayo haki ya
Kikatiba kutoa maoni yake lakini siyo sahihi wala busara kwa mwanachama
kumsema mwanachama mwingine hadharani, badala yake mambo hayo yangepaswa
kujadiliwa kwenye vikao vya ndani vya chama.
Wito kwa wanaCCM
Sadifa anatoa wito kwa makundi yote yanayoibuka na
yaliyopo ndani ya chama hicho kutulia kwa kile alichosema muda wa
kampeni haujafika na kwamba hali hiyo ikiendelea itasababisha chama
kushindwa kumpata mgombea safi maana wote watakuwa wameshachafuka.
“Ushauri wangu ni kwa wanaCCM wote kuwa watulivu
kwa faida ya chama…kuchafuana au kuharibiana ni kukiharibia chama kwani
wakati ukifika tutashindwa kumpata mgombea safi,” anasema Sadifa.
Kauli ya Msekwa:
Kauli ya Msekwa:
Wakati malumbano hayo yakiibuka, Makamu Mwenyekiti mstaafu wa
CCM, Pius Msekwa anawaonya wanachama wa chama hicho wenye nia ya
kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu ujao kuzingatia kanuni
za chama hicho, vinginevyo watahukumiwa kwa mujibu wa kanuni zenyewe.
Msekwa anasema kutangaza nia kabla ya wakati ni
kukiuka kanuni za chama ambazo zinaeleza wazi kuwa wagombea wa nafasi
mbalimbali watajitangaza baada ya chama kutoa ratiba yake.
Anasema CCM inaongozwa kwa mujibu wa kanuni na
katiba yake na kwamba katika jambo hili linaloibuka sasa kanuni ndiyo
zinayohusika ambazo zinaeleza wazi mgombea afanye nini na kwa wakati
gani.
“Mimi mwenyewe nilishiriki kuandika hizi kanuni,
utakapofika wakati, chama kitatoa ratiba yake na kila mwenye nia atakuwa
na uhuru wa kueleza nia yake, lakini kutangaza kugombea sasa kabla ya
wakati ni kukiuka kanuni za chama na ni kosa kubwa,” anasema Msekwa.
Msekwa anatoa angalizo kwa wale wanaodhani kuwa
kwa kuvunja kanuni wanakivuruga chama, badala yake wahusika wanafanya
makosa yatakayowaathiri wenyewe.
Hii si mara ya kwanza kwa Msekwa kukemea makundi
ndani ya chama hicho, akiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, wakati akiwahoji
watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho, alipata kusema makundi ya
wanaowania urais, yanakivuruga chama na kuwa hakitawavumilia
wanaochochea migogoro hiyo kwa masilahi yao binafsi.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment