Monday, February 3, 2014

Mambo ya kupapalikia White Man; Shilole akubali yule mwanaume siyo na hana mpango nae tena.

Yeleuuuwi! Siku chache baada ya msanii wa sinema na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kujinadi na mchumba wa Kizungu aliyejulikana kwa jina moja la Ankar, siri imefichuka kwamba jamaa huyo ni mwanaume tata.

Kikizungumza na paparazi wetu kutoka London, Uingereza, wikiendi iliyopita, chanzo hicho makini kilisema mwanaume ambaye hivi karibuni Shilole alijinadi kuwa ni bwana’ke siyo kwani huko London baadhi ya watu wanamfahamu kama mwanaume tata kijinsia.

“Yule jamaa anapenda sana kukaa na wanawake, sijawahi kumuona na wanaume wenzake, kazi kukata tu mauno na wanawake. Nilishangaa sana Shilole kusema eti ni mchumba’ke wakati hapa London (Uingereza) ni maarufu sana kwa kushiriki pati za wanawake.
WAPENZI: Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na 'mchumba wake', Ankar.
“Maskini Shilole, pale imekula kwake, hakuna chochote,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya kunyetishiwa habari hizo, Paparazi wetu alimtafuta Shilole ambapo alikuwa na haya ya kusema:
Jamani imeniuma sana kwani nilikuwa sijui, nimeligundua hilo baada ya kuambiwa na watu, nilipigiwa simu kutoka Uingereza kwamba yule mwanaume siyo hivyo sina mpango naye tena kwa kweli,” alisema Shilole anayetamba na kideo cha Nakomaa na Jiji.
SOURCE:GPL 
  

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top