Monday, February 3, 2014

Kisa cha Mchungaji Mtikila kupigwa hiki hapa.

Kiongozi wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila amenusurika kifo na mtu mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Mikidadi, ambaye yupo mahututi katika Hospitali ya Temeke,  baada ya kushambuliwa na watu wanaodaiwa kuwa na mzozo wa ardhi eneo la Kurasini, jijini Dar es Salaam.
  
Hapa anaonesha picha za X-Ray .
Mchungaji Mtikila alikumbwa na mkasa huo Ijumaa wiki iliyopita baada ya kufika katika eneo hilo kwa nia ya kutaka kuwaondoa watu hao wa familia tatu tofauti ambao wanaishi katika eneo hilo.
Kipigo hicho ambacho kimemsababishia majeraha ya kisogoni na hata kushonwa nyuzi tatu kichwani, kuvimba usoni na maumivu makali mwilini yalitokana na kipigo kutoka kwa familia mbili tofauti zinazoishi katika eneo hilo ambao wanapinga kuhama.

Mtikila alisema, mara baada ya kufika eneo hilo, alikwenda katika nyumba ya kwanza  na kuwakuta walinzi ambao walikubali na kuondoka katika eneo hilo kwani tayari notisi walikuwa nayo na walikuwa wanatambua kuwa wanatakiwa kuondoka.Alisema baadaye walikwenda katika nyumba ya pili ambayo anaishi mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Rubein Sanga ambaye hata hivyo vitu vyake vingi akuwa amekwisha vihamisha.
Alisema wakiwa mbele ya nyumba hiyo gari la polisi lilifika na wakiwa hawana hili wala lile vijana ambao anawataja kuwa ni wa Sanga walianza kuwashambulia kwa kutumia nondo na kila aina ya silaha za jadi.
“Walinipiga sana hadi nikapoteza fahamu na wakawa wanasema huyo Mtikila bebeni na mumchome moto, walitaka kuniua kwani walinikwida tai hadi ikakatika,” alisema.


Pia katika sakata hilo, Mtikila anadai kupoteza simu mbili, pesa taslimu Sh400,000 na Dola za Marekani 2,000 na siku ya tukio na alifika hapo akiwa ameongozana na watendaji wa Dawati la Msaada wa Kisheria katika taasisi yake ya Liberty Fund International.
Kamanda wa Polisi Temeke, Engbert Kiondo alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa wanalifanyia uchunguzi na taarifa kamili itatolewa kesho Jumanne.
Chanzo:Mwananchi.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top