Mshambuliaji mpya wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi.
Na Hans Mloli
SIKU chache baada ya Yanga kutangaza kuwa na mpango wa kwenda Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), kumshitaki mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi, mchezaji huyo ameibuka na kusema: “Hata Yanga waende kushitaki wapi, mimi sina wasiwasi hata kidogo.”
Yanga imeamua kuchukua uamuzi huo baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF ya kumuidhinisha Okwi kuitumikia Simba huku ikidai kuwa bado ana mkataba na Wanajangwani hao.
“Mimi sasa hivi sitaki tena kuwazungumzia hao Yanga, nipo Simba na nina furaha kuwa hapa, kama wanakwenda Fifa hata wafike mpaka Cas (Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Michezo) watajua wenyewe lakini sidhani kama huko kunaweza kubadili chochote, waende tu watajua wenyewe.”
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment