Monday, August 25, 2014

Marcio Maximo amfuata Phiri jukwaani na kumuomba urafiki.

 Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo akiwa na kocha mkuu wa Simba Patrick Phiri.

KOCHA Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, amemvaa kocha wa Simba Patrick Phiri na kumuomba urafiki huku akimtangazia vita hadharani.

Simba na Yanga zote zipo Zanzibar zikijiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na makocha hao wenye viwango vya hali ya juu, walikutana jana kwenye Uwanja Amaan, wakati Yanga ilipokuwa ikiivaa Shangani kwenye mechi ya kirafiki, kabla ya Simba nao kuvaana na KMKM saa 2:30 usiku.

Phiri alikuwa jukwaani wakati Maximo anaingia uwanjani, lakini Mbrazili huyo alishindwa kujizuia na kwenda jukwaani moja kwa moja ambapo alimfuata Phiri na kumpa mkono, kisha akamkumbatia na kumueleza maneno ya kutisha.

“Habari bwana, mambo yanasemaje, naomba tuwe marafiki mimi na wewe. Lakini tukiwa uwanjani kwenye dakika tisini itakuwa vita kali na urafiki tutauweka pembeni,” alisema Maximo huku Phiri akimsikiliza kwa umakini wa hali ya juu.

Kuonyesha kuwa Phiri amekubaliana na kocha huyo wa zamani wa Taifa Stars, alikuwa akitingisha kichwa kila kocha huyo alipokuwa akizungumza naye.
Hii ni mara ya kwanza makocha hao wanakutana baada ya wote kuingia mikataba na timu zao miezi michache iliyopita.

HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top