Monday, August 25, 2014

Rais wa shirikisho la soka Afrika Hayatou ameagiza hatua kali kuchukuiwa kufuatia mchezaji wa Algeria kupigwa jiwe nakufa uwanjani.


Rais wa shirikisho la soka barani Afrika Issa Hayatou ameonya kuwa Afrika haitatumika kama chimbuko la utovu wa nidhamu.

Bwana hayatouy ameyasema hayo baada ya mshambulizi wa JS Kabylie kutoka Cameroon Albert Ebosse kupurwa na jiwe kichwani akafa katika ligi ya Algeria.

Hayatou ameagiza hatua kali za kisheria kuchukuliwa ilikukabiliana na utovu wa Usalama.

Ebosee mwenye umri wa miaka 24, aligongwa kichwani baada ya timu yake kushindwa mabao 2-1 na USM Alger mjini Tizi Ouzou.

Hayatou amesema hawezi ruhusu zimwi la utovu wa usalama kukita mizizi Afrika

Mamlaka nchini humo imeagiza kufungwa wa uwanja wa 1st Novemba 1954 .

Ebosse alikuwa mfungaji bora msimu uliokamilika akiwa na jumla ya mabao 17 tangu awasili nchini humo kutoka Malaysia.

Rais wa ligi kuu ya Algeria Mahfoud Kerbadj, alisema kuwa kifo chake ni msiba mkubwa kwa soka ya nchi hiyo.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top