Saturday, February 8, 2014

Tendo la ndoa; Tiba mbadala ya maradhi ya moyo, ubongo na maumivu ya kichwa.

Ikumbukwe kuwa utafiti hauchochei watu kufanya mapenzi kiholela, bali unajikita kwa  wanandoa pekee.  

"Kwa mfano, tendo la ndoa linaondoa msongo wa mawazo iwapo unayetenda naye unampenda na  amekupa maandalizi mazuri. Sidhani kama alimradi utende hilo tendo na yeyote litakusaidia,” anasema mtaalamu huyo.

Ingawa tendo la ndoa lisipofanywa kwa kuzingatia kanuni na taratibu, sambamba na umakini, linaweza kusababisha maradhi, lakini kwa wanandoa, tendo  hilo linatajwa kuwa na manufaa mengi  kiafya tofauti na faraja ya kawaida iliyozoeleka kwa wengi.
Imefahamika kuwa tendo hili likifanyika ipasavyo husaidia kuondoa msongo wa mawazo, maradhi ya moyo, maumivu ya kichwa yasiyokoma na kupunguza kasi ya saratani ya tezi dume.
 Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Muhimbili (Muhas), Dk Yahya Kishashu anasema inategemea tendo linafanywa na nani na mhusika yupo kwenye mazingira gani.
“Kwa mfano, tendo la ndoa linaondoa msongo wa mawazo iwapo unayetenda naye unampenda na  amekupa maandalizi mazuri. Sidhani kama alimradi utende hilo tendo na yeyote litakusaidia,” anasema mtaalamu huyo.

Mazoezi
Si hivyo tu, utafiti uliofanyika Canada  hivi karibuni umebainisha kuwa kufanya tendo la ndoa kwa kipindi cha dakika 25 kwa wanamume kunachoma kalori 100 na kwa wanawake kalori 69.
Tendo hilo likifanyika kwa nusu saa, linaweza kupunguza kalori za mwili kuliko kutembea kwenye mashine ya mazoezi ya ‘treadmill’.
“Ni sawa na kucheza mpira wa tenisi au kutembea ukipanda mlima kwa dakika 20 au kucheza gofu kwa kasi kwa dakika 33 au zoezi la yoga kwa dakika 40,” sehemu ya utafiti hiyo inasema.
 Utafiti huo wa Canada ulishabihiana na kampeni  iliyofanywa na Taasisi ya Moyo ya Uingereza ambayo ilisema kuwa  dakika 30 za tendo la ndoa kwa siku ni muhimu kama mazoezi ya kutembea kwa mashine.
Kwa undani zaidi utafiti huo ulichambua na kusema kuwa, tendo la ndoa, lina manufaa  kwa moyo na mapafu.

Tiba kwa moyo, mapafu na ubongo
Inaelezwa kuwa tendo la ndoa, linasaidia kuondoa msongo wa mawazo hivyo kupunguza hatari ya maradhi ya moyo.
Si hivyo tu, bali tendo hilo husaidia mapafu kufanya kazi yake vyema, kuingiza na kutoa hewa chafu.
Kitaalamu, upo mchakato uitwao ‘Neurogenesis’ ambao husaidia kulinda seli za ubongo zinazokufa kutokana na uzee. Kuna eneo kwenye ubongo linaloitwa ‘hippocampus’ ambalo ni eneo linalotengeneza kumbukumbu.
“Kazi kubwa inafanyika kwenye ubongo, wakati wa tendo la ndoa, kiasi kikubwa cha viamsha raha huanzia kwenye ubongo na kuleta taarifa kwenye maeneo mengine ya mwili.
Ndiyo maana watu wengi hupotea kiufahamu wakati wa kilele” anasema Dk Gosh, ambaye ni mtafiti.
Hata hivyo, wanaume ambao wanaendelea na tendo la ndoa mara kwa mara hadi wanapofikisha miaka 50 na zaidi, kwa maana ya kutoa mbegu za kiume mara kumi kwa mwezi, wapo katika hatari ndogo ya kupata saratani ya tezi dume.  Inaelezwa kuwa mbegu za kiume hazitakiwi kukaa mwilini kwa muda mrefu.Zinatakiwa zitolewe mara kwa mara ili kuzifanya seli mpya zizalishwe. Ni kama kusafisha mpira, inasaidia kusitisha ujenzi wa seli za zamani ambazo zaweza kuwa chanzo cha saratani.
Kwa wanawake, tendo la ndoa husaidia kuundwa kwa misuli ya nyonga ambapo misuli hiyo ikiwa imara huondoa hatari ya kushindwa kuzuia mkojo,(urine incotinence) jambo linaloathiri mwanamke mmoja kati ya wanne wenye umri wa miaka zaidi ya 50.
“ Wakati wa tendo la ndoa, kwa kawaida sakafu ya nyonga za mwanamke hubana na kuachia. Hii husababisha misuli hiyo kuwa imara’ anasema mtafiti huyo.

Kama ungependa kusoma habari hii kiundani basi tembelea http://www.mwananchi.co.tz/Tendo-la-ndoa--Tiba-mbadala-ya-maradhi-ya-moyo--ubongo-/-/1596774/2196600/-/3p5i0c/-/index.html
kama huwezi andika url hiyo basi bofya hapa

CREDIT:MWANANCHI.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top