Wagombe hao
Msanii wa CCM Ally Bin Ahamed maarufu kwa jina la mpemba asilia akitoa mashairi ya kuipongeza CCM
Wagombea nao wakijifariji kwa makofi ya wajumbe
KAIMU Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga amewasihi wajumbe wa mkutano huo kumchangua mgombea anayoonekana kukubalika kwa asilimia 60 kwa wapiga kura.
"Falsafa ya chama kwanza, mtu baadaye lazima tuipime vizuri, tunahitaji ushindi na ili tupate ushindi lazima tuangalie wananchi wanataka nini," alisema.
Akifungua mkutano huo, Mtenga aliwataka wagombea ndani ya chama hicho wawe na utamaduni wa kukubali matokeo kwa afya ya chama.
Alisema wagombea wote tisa waliojitokeza katika kura hizo za maoni wana sifa za kuwa wabunge na akawataka wajumbe kutumia busara zaidi wakati wakifanya uamuzi.
Alisema mchakato wa kura za maoni ndani ya chama hicho umecchukua siku mbili hali itakayosaidia kukinusuru chama na mipasuko.
“Tulikuwa na kawaida ya kufanya kura za maoni kwa zaidi ya mwezi mmoja; hali hiyo ilikuwa ikiwaacha wagombea katika majeraha makubwa ya matumizi ya fedha,” alisema.
Alisema majeraha hayo yamekuwa yakichangia hasira kwa wagombea walioshindwa ambao badala ya kukisaidia chama kipate ushindi, hufurahia kinapopoteza nafasi.
Alisema kwa mtaji walionao, CCM wana hakika na ushindi wa kishindo katika jimbo hilo lililoachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa.
KAIMU Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga amewasihi wajumbe wa mkutano huo kumchangua mgombea anayoonekana kukubalika kwa asilimia 60 kwa wapiga kura.
"Falsafa ya chama kwanza, mtu baadaye lazima tuipime vizuri, tunahitaji ushindi na ili tupate ushindi lazima tuangalie wananchi wanataka nini," alisema.
Akifungua mkutano huo, Mtenga aliwataka wagombea ndani ya chama hicho wawe na utamaduni wa kukubali matokeo kwa afya ya chama.
Alisema wagombea wote tisa waliojitokeza katika kura hizo za maoni wana sifa za kuwa wabunge na akawataka wajumbe kutumia busara zaidi wakati wakifanya uamuzi.
Alisema mchakato wa kura za maoni ndani ya chama hicho umecchukua siku mbili hali itakayosaidia kukinusuru chama na mipasuko.
“Tulikuwa na kawaida ya kufanya kura za maoni kwa zaidi ya mwezi mmoja; hali hiyo ilikuwa ikiwaacha wagombea katika majeraha makubwa ya matumizi ya fedha,” alisema.
Alisema majeraha hayo yamekuwa yakichangia hasira kwa wagombea walioshindwa ambao badala ya kukisaidia chama kipate ushindi, hufurahia kinapopoteza nafasi.
Alisema kwa mtaji walionao, CCM wana hakika na ushindi wa kishindo katika jimbo hilo lililoachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa.

0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment