Tuesday, October 7, 2014

Mama amkata mwanaye paja na kuchoma mishikaki mwili uliobaki, soma mkasa mzima hapa.

Mwanamke mmoja Kilimanjaro amekamatwa na polisi akidaiwa kumkata mtoto wake mwenye umri wa miaka nane nyama ya paja na kuichoma mithili ya mshikaki.

Mwananmke huyo aliyetajwa kwa jina la Dafrosa Massawe anadaiwa kufanya unyama huo mwishoni mwa wiki na majirani wanasema mama huyo alifanya hivyo akiwa amelewa.

Kamanda wa Polisi Kilimanjaro Koka Moita alisema mwanamke huyo ataendelea kushikiliwa hadi uchunguzi wa tuhuma hizo utakapokamilika kabla ya kupelekwa mahakamani.

Akizungumza na Gazeti la MWANANCHI katika hospitali ya Kibosho mtoto huyo alisema hafahamu kosa alilofanya hadi mama yake ambaye ni mtengenezaji wa pombe za kienyeji kumfanyia kitendo hicho.

Alisema mama yake alirudi nyumbani usiku na kumkuta amekaa na kumsalimia kisha akamwomba chakula wakati akijua hakuna na baadae aliingia jikoni na kuchukua kisu kisha kumkata nyama kwenye paja lake baada ya kumwambia alishinda na njaa siku nzima.

Alisema baada ya kuikata aliichoma kama mshikaki na ilipoanza kufuka moshi na kutoa harufu aliitoa jikoni na kumwekea mtoto huyo puani ili avute harufu yake.

TOT NA WAKALI WA HIP HOP WAPAGAWISHA MASHABIKI DARLIVE.



HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top