Tuesday, October 7, 2014

Umeisikia hii ya Viboko Kutembezwa makaburini Sengerema?? Hii HApa

Wajukuu wa marehemu Sabina Ngalu wa Mwanza wamecharazwa viboko na watoto wa marehemu baada ya kung’ang’ania kaburini wakitaka wapewe fedha.

Chanzo cha wajukuu hao zaidi ya 10 kucharazwa bakora ni kung’ang’ania ndani ya kaburi lililokua limeandaliwa kwa ajili ya kuhifadhi mwili wa marehemu wakitaka wapewe ng’ombe mmoja au sh.100,000 kama zinavyotaka mila za kabila la kisukuma.

Gazeti la MTANZANIA ambalo lilikua shuhuda katika eneo hilo lilisema kitendo hicho kilimkera Padri Nicodemus Mayalla aliyekua eneo hilo huku akiwataarifu polisi kuhusu vurugu hizo hata hivyo kaka mkubwa wa marehemu aliamua kuchukua fimbo na kuanza kuwachapa.

Kitendo cha kuwachapa kiliamsha hasira zaidi kwa wajukuu hao ambao nao walijibu kwa kurusha michanga wakiwa ndani ya kaburi hadi waombolezaji walipoamua kuchanga na kuwapa fedha hizo ndipo walipotoka.

Hata hivyo Padri huyo aligoma kurejea eneo la makaburi kuongoza ibada hadi hapo watoto hao watakaporudisha fedha hizo na kuomba radhi,jambo ambalo lilitekelezeka.

DIAMOND AMKUBALI PETIT MAN; ASEMA ANASTAHILI KUWA MME WA DADAAKE.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top