Kocha Mkuu wa Yanga, Mbrazili, Marcio Maximo,akisisitiza jambo.
Na Wilbert Molandi
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mbrazili, Marcio Maximo, ametamba kuwa, siku nane zilizobaki kabla ya kukabiliana na Azam FC, zinamtosha kabisa kuifunga timu hiyo.
Timu hizo zinatarajiwa kujitupa uwanjani Septemba 14, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mchezo wa Ngao ya Jamii.
Hadi kufikia leo Jumamosi zitakuwa zimebaki siku nane kufikia mechi hiyo ya Ngao ya Jamii, ambayo kila timu inahitaji ushindi ili iweke heshima.
Maximo alisema, safu ya ushambuliaji pekee ndiyo yenye upungufu inayohitaji maboresho pekee, ambayo anaamini hadi kufikia mechi hiyo atakuwa ameiboresha.
Aidha, alisema kuwa, safu ya ulinzi haina matatizo ambayo katika mechi nne za kirafiki alizocheza imeruhusu bao moja pekee dhidi ya Shangani huku ya kiungo ikitengeneza nafasi nyingi za mabao ambazo washambuliaji wake wamekosa.

Aliongeza kuwa, katika ligi kuu ana ‘deby’ mbili ambazo ni dhidi ya Simba na Azam FC mara atakapokutana nazo kwenye mechi mbalimbali.
“Timu yangu sehemu yenye upungufu ni moja pekee ya safu ya ushambuliaji ambayo yenyewe inatengenezewa nafasi nyingi za kufunga na kushindwa kuzitumia vyema.
LUNDENGA NA MISS TANGA WAZICHAPA KAVU KAVU KISA KIKIDAIWA NI MICHEPUKO.
“Nimeanza kuiboresha safu hiyo ya ushambuliaji katika mazoezi ya leo (jana) na kuendelea kesho (leo) na hadi kufikia siku hiyo ya mechi na Azam FC tayari nitakuwa nimeiimarisha vyema katika kufunga mabao.Safu ya ushambuliaji ya Yanga inaundwa na Geilson Santos Santana ‘Jaja’, Jerry Tegete, Said Bahanuzi, Husein Javu na Hamis Kiiza.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment