Tuesday, August 19, 2014

MASTAA BONGO MUVI WASUSIA HITIMA.


Bango likionyesha picha na majina ya wasanii wa filamu na maigizo waliotangulia mbele ya haki lililowekwa katika viwanja vya Karimjee wakati wa Hitima hiyo iliyofanyika miki iliyopita. 
Aliyekuwa mgeni rasmi kwenye hitima hiyo, Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuia ya Wazazi (CCM), Abdalah Bulembo akitoa neno wakati wa shughuli.
Baadhi ya waalikwa waliokuwa wamekaa meza kuu.

   Sehemu ya wasanii na watu wengine waliohudhuria shughuli hiyo.

Mwenyekiti wa kundi la Bongo Movie Unity, Steve Mengere akitoa neno la shukurani wa watu waliojitokeza kwenye hitima hiyo.

Watoto wa kiume walioshiriki kuimba Kaswida

 Watoto wa kike walioshiriki kuimba Kaswida

Wasanii mastaa wa filamu Bongo juzi kati walisusia hitima iliyoitishwa kwa ajili ya kisomo cha wenzao waliotangulia mbele ya haki na kufanya Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, kuwapiga dongo kuwa kama ingekuwa shughuli ya pombe na uvaaji wa nusu utupu, wangekuwa wengi.

Dudu Baya: Sijabahatika kumpata mwanamke ninayemtaka, nakutana na machizi tu.


Hitima hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Karimjee, Posta jijini Dar na kuhudhuriwa na baadhi ya wasanii na wageni wengine waalikwa, akiwemo Mwenyekiti Taifa wa Jumuia ya Wazazi wa CCM, Abdalah Bulembo.

“Nimetumia muda mwingi sana kuwataarifu watu kuwa leo kuna hitima ya kuwaombea wenzetu waliotangulia mbele za haki, lakini ushirikiano wao umekuwa mdogo ila ingekuwa sherehe ambayo ina bia, yaani vitu vya anasa watu wangekuja wengi hadi viti visingetosha,” alisema Steve Nyerere.

Naye mgeni rasmi, Bulembo aliwaasa wasanii wa Bongo Muvi waliohudhuria hitima hiyo kutowatenga ambao hawakuhudhuria, badala yake washirikiane nao na kudumisha upendo na umoja ili kuondoa  matabaka.

Baadhi ya mastaa waliohudhuria hitima hiyo Johari, Wastara, Odama, Nisha, Eshe Buheti, JB, Richie, Baba Haji, Cloud, Masanja Mkandamizaji, Mzee Chilo na Mhogo Mchungu.
Imeandaliwa na: Chande Abdallah, Mayasa Mariwata, Rhoda Josiah, Gladness Malya na Shakoor Jongo.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

SEXIEST PHOTOS OF KIM KARDASHIAN WALKING ON STREET WITHOUT UNDERWEAR.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top