Wazazi wa zaidi ya wasichana 200 waliotekwa nyara na wapiganaji wa kundi la Boko Haram nchini Nigeria wamekataa wito wa kukutana na rais wa taifa hilo Goodluck Jonathan.
Hakuna sababu zozote zilizotolewa na wazazi hao.
Baadi wanamkosoa rais Goodluck kwa uamuzi wake wakisema umeshinikizwa na Malala
Mnamo siku ya Jumatatu mwanaharakati mdogo wa elimu Malala Yousafzai kutoka Pakistan alimsihi Rais Jonathan kukutana na wazazi wa wasichana hao.
Awali shirika la kimataifa la Human Rights Watch lilisema kuwa zaidi ya raia 2,000 wameuawa nchini Nigeria mwaka huu na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Vifo hivyo vinaripotiwa kutokea katika mashambulizi yaliyofanywa katika zaidi ya miji sabini na vijiji Kaskazini mwa Nigeria.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment