Saturday, July 5, 2014

UKISIKIA PIGO BASI NDO HILI: NEYMAR HATAENDELEA NA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA.


 STAA wa timu ya Brazil, Neymar hataendelea na michuano ya Kombe la Dunia 2014 baada ya kuvunjika mfupa unaoshikana na uti wa mgongo wakati wa mechi yao na Colombia usiku wa kuamkia leo.


Neymar akitolewa nje ya uwanja wakati wa Robo Fainali dhidi ya Colombia.


Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya.

Staa huyo mwenye mabao manne mpaka sasa kwenye michuano hiyo, alitolewa uwanjani dakika tatu kabla ya mechi yao dhidi ya Colombia kumalizika.

Neymar akiwa chini baada ya kuvunjika mfupa.

Katika mechi hiyo, Brazil walishinda mabao 2-1 na kutinga Nusu Fainali ambapo watakutana na Ujerumani Julai 8 mwaka huu.

Neymar akipatiwa huduma ya kwanza.
Kwa mujibu wa taarifa za daktari wa timu ya Brazil, Neymar atakaa nje kwa takribani wiki nne.

Wapenzi wa soka nchini Brazil wakiwa nje ya hospitali aliyopelekwa Neymar.


Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top