Sunday, July 20, 2014

TAMKO LA CHADEMA KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA.

 Mhe.Freeman Mbowe!

"Mchakato wa Katiba ni mchakato wa Kisiasa.
Mchakato ukiharibiwa, hutengeneza Ombwe.
Makundi mbalimbali yamekuwa yakitoa wito ili kuokoa mchakato wa Katiba.
Rai ya kututaka UKAWA kurudi bungeni, bado haijazingatia yale yaliyotufanya tutoke Bungeni.
Viongozi wa UKAWA tumekaa na kujadili kwa kina.

Ni uwendawazimu kurudi bungeni kwa mazingira yale yale.
UKAWA tumechukua nafasi kuziba Ombwe la uongozi wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.
Tuna ushahidi wa namna CCM wanavyopanga kuvuruga mchakato wa Katiba.

Sisi tutapanga namna ya kuandaa Plan B.
Hatuko tayari kwenda kwenye uchaguzi Mkuu mwakani kwa Sheria hizi hizi.

Siku ya Jumapili baada ya vikao hivi, tutatoka na maazimio na tutaongea na vyombo vya Habari.
Tutakaa na kujadili kwa kina kwenye vikao hivi vya leo na kesho, pamoja na agenda nyingine, lakini ni lazima tutoke na maamuzi mazito.

Tunamtaka Rais aache tabia ya ukigeugeu.
Tunamtaka Rais kwa muda mchache aliobakia madarakani, ajifunze hata kwa kujilazimisha, aache tabia ya unafiki".
Mhe.Mbowe ameyasema hayo kwa niaba ya Chama katika hotuba yake fupi ya ufunguzi wa vikao vya Kamati Kuu ya CHADEMA vinavyoendelea hivi sasa katika Ukumbi wa Mbezi Garden Hotel iliyopo Mbezi Beach Jijini Dar Es Salaam.

Mhe.Tundu Antipus Lissu,
Mjumbe Kamati Kuu,
CHADEMA.
18/07/2014.
Ahsanteni sana!!!


Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top