Thursday, July 3, 2014

H.BABA AUGUA DENGUE NA KULAZWA MUHIMBILI. MKEWE JOTO LAMPANDA ALIZANI YALE YALE KUMBE DENGU.

KUTOKANA na hivi karibuni mumewe, Hamis Baba ‘H. Baba’ kuugua ugonjwa wa homa ya Dengue ‘Dengi’ na kulazwa Muhimbili, msanii wa filamu Bongo, Flora Mvungi amesema alijikuta kwenye wakati mgumu kuhofia mumewe angepoteza maisha.

 
 Msanii wa filamu Bongo, Flora Mvungi akiwa na Hamis Baba ‘H. Baba’.

 Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Flora alisema ni Mungu tu mumewe kupona kwani alikuwa katika hali mbaya ambayo mpaka yeye kama mkewe alikuwa na hofu kubwa ya kifo haswa ukizingatia vifo vya wasanii vilivyotokea mfululizo.

“Nilipoona wasanii wenzangu wakifariki dunia na mume wangu kuzidiwa mpaka kulazwa Muhimbili, nilikuwa nina hofu kubwa ya kifo lakini namshukuru Mungu amepona na tunaendelea na maisha kama kawaida, dengue noma sana,” alisema Flora.

Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top