Saturday, June 21, 2014

Madaktari wasio na Mipaka, Medicine San Frontiers wamesema Ugonjwa wa Ebola haudhibitiki tena.

Raia anayeugua ugonjwa w Ebola

Afisa mwandamizi wa shirika la madaktari wasio na Mipaka Medicine San Frontiers ameelezea kuwa mkurupuko wa ugonjwa wa Ebola katika mataifa matatu ya magharibi hauwezi kudhibitika.

Mkurugenzi wa Oparesheni katika shirika hilo Bart Janssens ameliambia shirika la habari la A.P kwamba ugonjwa huo utasambaa hadi katika mataifa mengine iwapo hakutakuwa na mwitikio wa kimataifa.

Ugonjwa wa Ebola tayari umesababisha vifo vya takriban watu 330 nchini Guinea,Sierra leone na Liberia.

Bwana Janssens amesema kuwa shirika la MSF limefikia kikomo cha uwezo wake wa kukabiliana na ugonjwa huo.

Chanzo; BBC/SWAHILI.

Ungependa stori kama hizi zisikupite na zikufikie wakati wowote? niko tayari kukutumia wakati wowote iwapo utajiunga na mimi kwa kubonyeza Like hapo juu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top