Wednesday, March 19, 2014

Alikichokisema Jaji Joseph Warioba kuhusu mapendekezo ya serikali tatu katika Muungano hiki.


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesisitiza kuwa mapendekezo ya serikali tatu katika Muungano ni ya wananchi na taasisi mbalimbali, na wala si matakwa ya tume yake.


Akiwasilisha Rasimu ya Pili ya Katiba wakati wa kikao mahsusi cha Bunge Maalum mjini Dodoma, Jaji Warioba alieleza kuwa nusu ya wananchi waliotoa maoni yao kuhusu Muungano walitaka uwepo wa serikali tatu.


Kati ya wananchi 38,000 waliotoa maoni yao kuhusu Muungano, 19,000 walizungumzia suala la muundo, huku zaidi ya nusu wakitaka marekebisho ya kikatiba yatakayowezesha uwepo wa serikali tatu.

“Kwa upande wa Bara, asilimia 61 [ya wale waliotoa maoni juu ya Muungano] walipendekeza muundo wa serikali tatu,” alisema Jaji Warioba. “Kwa upande wa Zanzibar, [asilimia] 60 walipendekeza Muungano wa mkataba.”
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top