Friday, January 3, 2014

Wanakwaya wa RC Arusha walipukiwa na kitu kinachozaniwa kuwa ni bomu mkesha wa mwaka mpya.


 
Wanakwaya kadhaa wa kanisa katoliki la Mt Kalory maeneo ya USA River mkoani arusha wamelipukiwa na kitu kinachozaniwa kuwa ni bomu na wamelazwa katika hospitali ya Misheni ya Tengeru.
Sita kati yao ni majeruhi na mmoja hali yake ni mbaya.
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas amezungumza na  na waandishi wa habari, akithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kulifuatilia kufaham chanzo cha tukio hilo.

"Taarifa nimezipata lakini uchunguzi unaendelea kujua chanzo na muhusika sambamba na ukweli wa mlipuko huo ili kujua kama kweli ni bom na ni la aina gani".
 

Wakizungumza na mtandao huu, kwa nyakati tofauti katika hospitali ya Tengeru iliyopo wilayani Arumeru, baadhi ya majeruhi wa tukio hilo walisema kuwa siku ya mkesha wa kuupokea mwaka 2014 walipokuwa wakitoka kanisani (Kanisa katoliki parokia ya USA river) waliweza kusikia mlio mkubwa wa kitu kama bom la kurusha ndipo baadhi yao walioangukiwa na bom hilo kuweza kujeruhiwa vibaya na kuanguka chini huku wakivuja dam nyingi sehem mbalimbali za mwili.

Kwa upande wake Askofu mkuu wa kanisa la katoliki jimbo kuu la Arusha, Josephat Lobulu akizungumzia tukio hilo alisema kuwa ni tukio la kulaaniwa, hivyo ameliomba jeshi la polisi kushughulikia jambo hilo.



Alisema kuwa amesikitishwa na tukio hilo, lakini yeye kama mtumishi wa Mungu anapaswa kuwaombea wote walioathrika na tukio hil ikizingatiwa wamepatwa na tukio hilo mita chache tu kutoka katika nyumba ya Mungu (Kanisani).

Tutazidi kukujuza repoti kutoka polisi ikitolewa.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online