Tuesday, January 21, 2014

kanisa la kilokole la wala nyasi laingia Dar,lipo Upanga.Wengi wataka kujiunga nalo.

Kanisa hilo ambalo makao yake makuu ni Afrika Kusini linaloitwa Rabboni Centre Ministries limeingia nchini na lipo maeneo ya Upanga jijini Dar.
Baadhi ya wananchi waliozungumza nana mwandishi wetu   walisema wanatamani kujiunga.

“Mimi nataka kujiunga na kanisa hilo kwa sababu tunataka wokovu,” alisema mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Amos.

Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Frida Mandade alisema ana hamu ya kujiunga na kanisa hilo kwa sababu zake binafsi.

Kanisa la Rabboni Centre Ministries lina makao yake makuu Pretoria nchini Afrika Kusini na linaongozwa na mtu anayejiita Mchungaji na Nabii Daniel Lesego ambaye alilianzisha mwaka 2002.

Wakati wa mfungo waumini wa kanisa hilo wametajwa kuwa huwa wanaishia kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo kwa imani kuwa Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top