Tuesday, January 7, 2014

IMF yaionya kenya kuhusu kuharakisha mpanga wa sarafu moja katika EAC

 Manager mkurugenzi wa shirika la fedha duniani IMF Christine Lagarde ameionya Kenya na washirika wake kuhusu kuharakisha mpango wa kuwa na sarafu moja katika nchi za Afrika mashariki.

Amesema lazima masuala ya msingi yajadiliwe na kufikiwa kwa makubaliano ya kwa pamoja kabla ya kucukua uamuzi wa kutengeneza sarafu hizo ambazo zitatumika katika nchi zote za jumija ya Afrika mashariki.

Amewaambia wakenya ambao ndio vinara wa uchumi kwa EAC na ndio fedha yao inathamani zaidi katika EAC kuwafahamisha wanachama wengine wa EAC juu ya mpango huo na kujadili matatizo yaliyowahi kutokea katika matifa mengine walipoamua kuwa na sarafu moja kama EURO ambayo ilipoanzishwa ilipata changamoto kubwa licha ya kutengamaa kwa sasa.

Kenya inaushawishi mkubwa katika EAC na tayari nchi tatu yaani  Uganda,Rwanda na Kenya wameanza kutengeza vitambulisho vya EAC ambapo raia wa nchi moja atasafiri hadi nchi nyingine bila ya passport ilimradi tu ana kitambulicho hicho.


Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top