Thursday, December 4, 2014

LAVEDA ARUDI BIG BROTHER AFRICA -BBA.


MWANADADA aliyewakilisha Tanzania katika shindano la BIG BROTHER 2014 ‘HOTSHOTS’ nchini Afrika Kusini. Irene Neema Vedastous 'La Veda' ameitwa tena ili kushuhudia fainali za kinyang’anyiro hicho.
Mrembo huyo amepanda pipa juzi saa 8 mchana kuelekea Sauz ambapo atakaa kwa muda wa wiki moja.

Akizungumza na paparazi, La Veda alisema ameitwa Sauz japo bado hajajua anaenda kufanya nini hasa japo anaamini hataingia kwenye jumba la BBA kama mshiriki.
‘’Nimeitwa BBA ila si kwa maana ya kushiriki bali kama mmoja wa washiriki ili kushuhudia fainali za BBA zinazotegemea kufanyika hivi karibuni.
Ninafurahi kwa sababu nitakutana na washiriki wenzangu, kama nikibahatika kupata nafasi ya kuimba, wimbo wangu mpya wa LET IT GO, nitafanya makubwa sana maana muda mwingi na akili yangu nimeviwekeza kwenye muziki, nitakuwa Sauz kwa wiki moja kisha nitarejea nyumbani kujipanga zaidi kimuziki" Alisema La Veda.
Aidha La Veda amemtakia kila la heri mshiriki mwenzie Idris Sultan ashinde na amewaomba Watanzania kumuombea kwani ushindi wake ni ushindi wa Watanzania wote.
Irene Neema Vedastous 'La Veda'.

Former BBA Winner Dillish Mathews goes topless in Ova Himba Cultural attire.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online