MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amezuiwa kunywa pombe baada ya kuangushiwa maombi mazito na kushauriwa kubadilika kitabia.
Chanzo makini kimepenyeza habari kuwa, juzikati Maya alifika katika kanisa moja lililopo Mbezi jijini Dar na kuombewa kisha mchungaji wa kanisa hilo akamzuia kunywa pombe.
“Kazuiwa lakini najua kwake itakuwa mtihani, sidhani kama ataacha kweli,” kilisema chanzo hicho.
Alipotafutwa Maya, alikiri kuombewa lakini alipotajiwa suala la kuzuiwa pombe na kama ataweza kweli kuacha, alikata simu ghafla.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment