Monday, October 20, 2014

STEVE NYERERE AFUTWA RASMI UANACHAMA BONGO MOVIE.


Mshtuko! Siku chache baada ya kujiengua kwenye nafasi ya uenyekiti katika Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ anadaiwa kufutwa uanachama wa klabu hiyo.

Aliyekuwa mwenyekiti katika Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.

Chanzo cha ndani ya klabu hiyo kimepenyeza madai kuwa, wameamua kumvua uanachama Steve kwani wanaona ni ‘kirusi’ ndani ya klabu kutokana na mwenendo wake.

“Steve amekuwa akiwashawishi baadhi ya memba wajiunge na upande wake, tofauti na umoja wa Bongo Movie Unity, viongozi wameamua kumfuta kabisa uanachama,” kilisema chanzo na kuongeza:
“Amewatangazia wenzake vibaya juzikati alivyokwenda Dodoma kwenye sherehe za kukabidhiwa kwa Rasimu ya Katiba Iliyopendekezwa kwa kuwaambia viongozi wa serikali kwamba wasanii ambao hawakwenda mjini humo ni Ukawa wakati si kweli.”

Katibu wa Bongo Movie Unity,William Mtitu akiwa ndani ya Ofisi za Global.

Baada ya chanzo chetu kujiridhisha na data hizo za ndani, mwanahabari wetu alimtafuta Steve Nyerere ili kujua anazungumziaje juu ya ishu hiyo ya kuenguliwa klabuni na mtazamo kuhusu suala hilo, alipopatikana alikuwa na haya ya kusema:

“Mimi ni mwanachana wa Bongo Muvi kama nimefutwa sijui lakini ni mwanachama. Kuhusu kuwasemea nilipokuwa Dodoma, ningewasemea mimi kama nani? Sina cheo cha kuwasemea wenzangu.
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na tafrani kubwa Bongo Muvi huku madai mengi yakielekezwa kwa Steve.

Mwanafunzi wa darasa la sita wa shule ya msingi ya Themi iliyopo jijini Arusha Abakwa na watu sita.



HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online