Wednesday, October 22, 2014

APIGWA RISASI MCHANA KWEUPE, MAGOMENI JIJINI DAR ES SALAAM!

Mtu asiyefahamika akiwa ndani ya gari lake mara baada ya kupigwa risasi tumboni. Kushoto kwake ni mwanamke aliyekuwa naye garini.

....wapita njiawakijaribu kutoa msaada kwa mtu huyo.

Muonekano wa nyumba wa gari hilo.

Mtu mmoja ambaye hakuweza kujulikana jina lake mara moja amepigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi na kuporwa mkoba uliyokuwa garini ambao haukujulikana ulikuwa na nini ndani yake. Tukio hilo limetokea leo majira ya mchana maeneo ya Magomeni Mikumi jirani na kwa Sheikh Yahaya jijini Dar es Salaam. Mtu huyo alipigwa risasi tumboni akiwa kwenye gari yake Toyota Mark II (GX 100) yenye namba za usajili T487 AZW. Kwenye gari hiyo, alikuwemo mwanamke mmoja akiwa amekaa kwenye kiti cha mbele cha abiria ambaye hakujeruhiwa.

LUNDENGA AONYESHA UTHIBITISHO WA UMRI WA MISS TANZANIA 2014 KAMA ILIVYO KWENYE CHETI CHAKE CHA KUZALIWA.



HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top