
BENKI Kuu ya Tanzania imetoa toleo jipya la sarafu ya shilingi 500 itakayoanza kutumika Oktoba 2014 itakayokuwa mbadala wa Noti ya shilingi 500 inayoonekana kuchakaa haraka.
Noti ya 500 inayotumika sasa.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Huduma za kibenki wa benki hiyo Bw. Emmanuel Boaz wakati wa mkutano na waandishi wa habari.
“Noti ya shilingi 500 hupita kwenye mikono ya watu wengi zidi na ndiyo inayotumika zaidi kwenye manunuzi ya kawaida hivyo kuchakaa haraka ndio maana tumeamua kutoa toleo la sarafu itakayoanza kutumika mapema mwezi wa 10 mwaka huu.”alisema Boaz.
Akitaja sifa za sarafu hiyo mpya Boaz amesema kwanza umbo lake ni la duara lenye michirizi pembezoni na kipenyo cha milimita 27.5 na uzito wa gramu 9.5.
KUTANA NA Sexy Lady Ella Ciku Who Beat Vera Sidika And Other Hotties To Represent Kenya At The Big Brother Africa!!
Sifa nyingineni kuwa ina rangi ya fedha na imetengenezwa kwa madini aina ya chuma na Nickel na kwa upande wa mbele ina sura ya Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Sheikh Abeid Aman Karume na kwa nyuma ina taswira ya mnyama nyati akiwa mbugani.Pia Boaz alibainisha kuwa sarafu hiyo kwa upande wa nyuma ina kivuli kilichojificha ambacho huonesha thamani ya sarafu ya 500 au neno BOT inapogeuzwa geuzwa.

Kwa upande wa matumizi Boaz amesema sarafu hiyo itakapoanza kutumika itatumika sambamba na noti za shilingi 500 hadi zitakapokwisha kwenye mzunguko.
Benki Kuu ya Tanzania ndiyo chombo chenye jukumu la kutoa sarafu na noti halali (legal tender) zinazotumika nchini ambapo katika kutimiza jukumu hili Benki kuu hutengeneza noti na sarafu zenye uwiano mzuri wa thamani (denomination) unaozingatia uwezekano wa zile zenye thamani kubwa kuweza kugawika katika zile zenye thamani ndogo.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment