Friday, August 1, 2014

SEKESEKE LA IDD; MMOJA ANUSURIKA KUBAKWA NA MWINGINE AMWAGIWA MAJI YA MOTO.

HILI kweli ni sekeseke la Idd el Fitr. Wakati changudoa mmoja akinaswa na kumwagiwa maji na wananchi waliochoshwa na vitendo vya ukahaba vinavyofanywa jirani na makazi yao, msichana mwingine aliokotwa akiwa amelewa chakari na kudhaniwa kuwa na mapepo, maeneo ya Sinza Afrikasana jijini Dar Jumanne hii.

changudoa anaswa na njemba na kumwagiwa maji ya moto.

Katika tukio la kwanza lililotokea Idd Mosi, wakazi wa maeneo ya Afrikasana, waliamua kuweka mtego na kumnasa changudoa aliyekutwa na mteja wake wakimaliza haja zao uchochoroni, wakiwa wametandika boksi chini.

“Yaani tumechoshwa na hawa machangudoa, inafikia hatua tunashindwa kulala kwa sababu ya miguno yao ya kimapenzi, hata watoto wanashtuka usingizini kwa sababu ya mambo hayo, ni hatari kwani wanaweza kujifunza ufuska, tumeamua kuwanasa leo jamani na itakuwa fundisho kwao,” alilalamika mmoja wa majirani hao.

Huku timu ya Operesheni Fichuo Maovu (OFM) ya Global Publishers ikiwa ‘beneti’ na majirani hao, ilishuhudia wawili hao wakikamatwa na kupewa adhabu ya kulowanishwa kwa maji ya moto ambapo nguo zao zililoa chapachapa.

Wakati changudoa huyo akipewa adhabu hiyo ili liwe fundisho kwa wenzake wanaokesha pembezoni mwa barabara ya Shekilango, msichana mwingine anayedhaniwa kuwa alilewa kupita kiasi, alikutwa akiwa amezungukwa na watu nje ya baa maarufu ya Corner.Changudoa huyo akijuta baada ya tukio hilo.

Kundi kubwa la watu lilimzunguka mwanamke huyo kutokana na vitendo vyake kuashiria alikuwa amelewa bwii, wengine wakiamini alikuwa na mapepo hivyo kutaka kujua namna ya kumsaidia.

“Huyu dada jamani itakuwa majini yake tu yanamsumbua, si unajua watu wengine majini yao hayapendezwi na ulevi uliozidi kiwango, maana mtu mwenyewe haeleweki, tukimshika kumsaidia anataka kuturukia sasa sijui tufanyaje,” alisikika kijana mmoja akisema.

Hata hivyo, baadhi ya vijana waliokuwa eneo hilo walionekana kupanga mbinu za kumchukuwa msichana huyo na kwenda kumfanyizia, kitu kilichoshtukiwa na mabaunsa wa baa hiyo ambao walimpandisha kwenye Bajaj na kumkimbiza Kituo cha Polisi Mabatini ambako baada ya askari kuwasikiliza, walishauri apelekwe hospitalini.Binti anusurika kubakwa baada ya kulewa chakali.

Alipelekwa Hospitali ya Palestina ambako baada ya kupimwa, alionekana kunywa pombe kali kupindukia, hivyo kuwekewa dripu.

IMEANDALIWA NA: Chande Abdallah, Gladness Mallya, Shani Ramadhan, Mayasa Mariwata, Deogratius Mongela na Denis Mtima.




Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya. 

ISOME NA HII

Binti afanyiwa mchezo mchafu chooni baada ya kulewa vibaya akiwa Night Club.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top