Tuesday, August 19, 2014

MAULID KITENGE ATUA RADIO EFM RASMI BAADA YA KUONDOKA RADIO.

Mtangazaji mahiri wa habari za michezo, Maulidi Baraka Kitenge akisaini mkataba wa kazi na kituo cha radio kiitwacho EFM 93.7 kilichopo Kawe jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa vipindi wa Radio EFM, Dickson Ponela.

Mtangazaji mahiri wa habari za michezo, Maulidi Baraka Kitenge akipeana mikono na Mkurugenzi wa vipindi wa Radio EFM, Dickson Ponela wakati wa kubadilishana mikataba baada ya kusainishana jioni hii katika makao makuu ya radio hiyo, yaliopo Kawe jijini Dar es Salaam.
MTANGAZAJI mahiri wa habari za michezo wa siku nyingi Maulidi Baraka Kitenge amejiunga na kituo cha radio kiitwacho EFM 93.7 kilichopo Kawe jijini Dar es salaam leo.

Kutokana na tafiti ya Ipsos ya mwaka 2013, inasemekana kuwa mtangazaji huyo wa zamani wa kituo cha Radio One, ndiye mtangazaji bora wa michezo nchini Tanzania.

Masogange Releases Another Killing Photo to Attact you for her Business that Shows Off Her Blessed Assets.


Mkurugenzi wa vipindi wa Radio EFM, Dickson Ponela, ameeleza kufurahishwa kwake kwa mtangazaji huyo kinara kuhamia katika kituo hicho.

“Mpaka sasa Kitenge ameisha saini mkataba na kituo chetu na anatarajiwa kusikika hivi karibuni katika kipindi cha michezo hapa EFM”, alisema mkuregenzi huyo.

Kitenge au jezi nambari tisa mgongoni, amejiunga na magwiji waliobobea katika fani hiyo akiwemo Dizo One, Dennis Sebo, Sos B, Kanky Mwaigomole na Dj Majay.





HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

 PICHA NA VIDEO ZA SHILOLE AKIWA MZIWANDA KITANDANI ZAVUJA MTANDAONI, JIONEE MWENYEWE HAPA.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top