Mtangazaji mahiri wa habari za michezo, Maulidi Baraka Kitenge akipeana mikono na Mkurugenzi wa vipindi wa Radio EFM, Dickson Ponela wakati wa kubadilishana mikataba baada ya kusainishana jioni hii katika makao makuu ya radio hiyo, yaliopo Kawe jijini Dar es Salaam.
MTANGAZAJI mahiri wa habari za michezo wa siku nyingi Maulidi Baraka Kitenge amejiunga na kituo cha radio kiitwacho EFM 93.7 kilichopo Kawe jijini Dar es salaam leo.
Kutokana na tafiti ya Ipsos ya mwaka 2013, inasemekana kuwa mtangazaji huyo wa zamani wa kituo cha Radio One, ndiye mtangazaji bora wa michezo nchini Tanzania.
Masogange Releases Another Killing Photo to Attact you for her Business that Shows Off Her Blessed Assets.
“Mpaka sasa Kitenge ameisha saini mkataba na kituo chetu na anatarajiwa kusikika hivi karibuni katika kipindi cha michezo hapa EFM”, alisema mkuregenzi huyo.
Kitenge au jezi nambari tisa mgongoni, amejiunga na magwiji waliobobea katika fani hiyo akiwemo Dizo One, Dennis Sebo, Sos B, Kanky Mwaigomole na Dj Majay.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment