Thursday, August 7, 2014

MABAUNSA wa Baa; WATOA KICHAPO KIKALI KWA WAREMBO KISA KUPOMBEKA HADI JUA LINACHOMOZA.

 
BALAA! Siku chache tu baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, warembo wawili ambao majina yao hayakufahamika haraka wamejikuta wakila kichapo kutoka kwa mabaunsa kufuatia kuchelewa kutoka ndani ya baa waliyokuwa wakipombeka.

Akilia baada ya kula kichapo.

Tukio hilo la aina yake lilijiri Agosti 5, mwaka huu katika baa hiyo mpya iliyopo Sinza ya Afrikasana jijini Dar es Salaam.

Ilidaiwa kuwa, warembo hao waliambiwa mapema kuwa ifikapo alfajiri wasionekane kwenye eneo la baa hiyo lakini wao waliendelea kupombeka  mpaka jua linachomoza ndipo mabaunsa walipowaondolea uvivu kwa kuwapa kipigo.

Mmoja wa warembo hao ambaye alionekana kukerwa na kitendo cha mwenzake kupigwa hadi kutokwa damu aliwalalamikia mabaunsa hao kuwa hawajawatendea haki kwa kuwafukuza kama mbwa na kipigo juu.Akitokwa na damu juu ya jicho la upande wa kulia baada ya kuchezea kichapo kikali.

MTOTO ANUSURIKA KUBAKWA KIBAHA; MTUHUMIWA ATOA ELFU 20000/= KUYAMALIZA.

Kwa vile hawakuwa na nguvu za kupigana na mabaunsa hao, warembo hao waliporomosha matusi ya nguoni na kujaza watu waliokuwa wakienda makazini asubuhi hiyo.

Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, hasa wanaume walisikika wakipongeza kitendo cha warembo hao kuchezea kichapo wakisema wamezoea kukesha eneo hilo mpaka kunakucha.
Mashuhuda hao walikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa wanahisi warembo hao wanajihusisha na biashara ya ‘udada poa’.

Baadhi ya wananchi wakishuhudia mkasa huo.

“He! Wamezoea hao! Ni sawa mabaunsa wawaoneshe kazi. Watu gani wapo baa hadi muda huu wa asubuhi kweupe?” alisikika mmoja wa mashuhuda hao.

Yaliyomkuta Agnes Masogange ndani ya uwanja wa ndege Juzi HAYA.

Kilio kikubwa cha mabaunsa hao kilikuwa ni kutaka kusimamia heshima ya baa hiyo kwa vile wateja wanaofika hapo ni wenye heshima zao.

“Msije tena hapa, sisi hatuwataki muda wa asubuhi wala mchana, tulishasema sana lakini hamsikii, mnataka kutukimbizia wateja siyo?” alisema mmoja wa mabaunsa hao.

Wakishauliana jinsi ya kumsaidia mwenzao.

Mwisho wa sakata hilo, warembo wengine walitafuta usafiri wa Bajaj na kumbeba mwenzao aliyepigwa sana mpaka kutoka manundu na kuondoka huku wakiendelea kuvurumisha mitusi kwa mabaunsa hao na kusema wanakwenda kutoa taarifa kwenye Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar.

KATANGAZE! Aunt Ezekiel Afumaniwa na Dansa wa Diamond Ambaye ni Mme wa Mtu waki Du Nyumbani Kwa Wema Sepetu.

Mapaparazi wetu waliifuatilia Bajaj hiyo na kuiona inaelekea maeneo ya Sinza ya Mapambano  badala ya polisi.

Baadhi ya wateja wa baa hiyo walisema wakati wa Mfungo wa Ramadhan, warembo walipungua eneo la baa hiyo lakini sasa wamerudi tena ambapo sasa wanapatikana kuanzia saa moja jioni hadi jua linapochomoza kesho yake!


Bonyeza Like HAPO JUU USHINDE ZAWADI YA BAHATI NASIBU WAWEZA SHINDA HADI MILLION MOJA.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top