Monday, August 11, 2014

JACK PATRICK AYEYUKA GEREZANI NDUGU WAHAHA, HOFU YA KUNYONGWA YATANDA.


Jacqueline Fitizpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ akiwa Chini ya ulinzi mkali China.
Nini kinaendelea? Video Queen wa Bongo anayeshikiliwa na jeshi la polisi nchini China kwa msala wa madai ya kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’, Jacqueline Fitizpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ anadaiwa kuyeyuka gerezani.

Kwa mujibu wa ‘mtu wetu’ aliyeambatana na rafiki zake Jack kwenda kumuona gerezani, Macau, Hong Kong nchini humo, walijikuta wakipigwa na butwaa kuambiwa hakuna mtu kama huyo gerezani hapo hivyo kuibua hofu kuwa huenda amenyongwa.

Yaliyomkuta Agnes Masogange ndani ya uwanja wa ndege Juzi HAYA.

Uchunguzi wetu gerezani hapo ulibaini kwamba tofauti na hofu ya rafiki zake, kuna uwezekano Jack amehamishiwa gereza lingine lililopo nje kidogo ya Mji wa Macau.Chanzo chetu hicho kilidai kwamba habari za ndani zilieleza kwamba Jack amehamishwa gereza hivyo kwa maelezo zaidi watu wanaokwenda kumtembelea waende kwenye ofisi za gereza hilo alilokuwa awali watapewa maelekezo wapi alipo mtu wao.


Video Queen wa Bongo, Jacqueline Fitizpatrick Cliff ‘Jack Patrick’.


“Unajua watu wanaokwenda kumtembelea Jack gerezani ni Watanzania walioko huku China kwa shughuli maalum hasa za sanaa, kama vile sarakasi au maigizo, wengine wote wanaogopa, wanajua wanaweza kukamatwa.

“Tulipokwenda na mazagazaga yetu tuliambiwa Jack amehamishwa gereza na inaonekana aliomba mwenyewe ila hatujui ni kwa nini alifanya hivyo,” kilisema chanzo hicho.Hivi karibuni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, John Haule alitoa taarifa na kutaja jumla ya watuhumiwa waliokamatwa kwa kesi za madawa ya kulevya ambapo alisema kuwa kuna Watanzania wengi wapo kwenye magereza mbalimbali China.

“Katika magereza ya China hadi Februari (mwaka huu) tulipewa taarifa kwamba wapo Watanzania 177 magerezani na kati ya hao 15 wamehukumiwa kunyongwa kutokana na baishara hiyo ya madawa ya kulevya,” ilisema taarifa hiyo ya katibu mkuu.

Jack alikamatwa Macau, Hong Kong, mwaka jana hivyo kesi yake inaendelea kuunguruma. Tofauti na Beijing ambao huwa wananyonga watu wanaojishughulisha na unga, Hong Kong ni kifungo cha miaka kadhaa tu.



Bonyeza Like HAPO JUU USHINDE ZAWADI YA BAHATI NASIBU WAWEZA SHINDA HADI MILLION MOJA. 

PASTOR MYAMBA Afunga Harusi ya Kufuru! KAMATI PEKE YAKE ILIMZAWADIA Million 250;Dada Mtu Nae Million 100.Wapambe ....

 

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top